Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wa CCM Magufuli, yaliyotokea Tarime ni aibu tupu

Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wa CCM Magufuli, yaliyotokea Tarime ni aibu tupu

Na Ghati Chacha

HII sio Chama Cha Mapinduzi(CCM) ninachokijua na kukulia kwa zaidi ya miaka 30. Chama kilichosimama mstari wa mbele katika kuwakomboa wananchi na unyonge wao, Chama kinachosimama mbele kupinga rushwa hadharani.

Naamini na nitaendelea kuamini CCM ni taasisi kubwa na yanayoendelea kufanyika katika Mkoa wa Mara hasa majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini ni jambo linalopaswa kukemewa na kila mpenda maendeleo na kukitakia mustakabali Chama katika kuyasisimamia maendeleo ya wananchi.

Yaliyofanywa na washindi wa kura za maoni katika majimbo ya Tarime ni wizi mkubwa na yanapaswa kukemewa kwa nguvu zote kwani haikubaliki na haitakiwi kwa CCM kushiriki kwenye ulanguzi wa kura kama uliofanywa na kina Jackson Kangoye kwa Tarime Mjini.

Kiongozi anayenunua kura hafai hata kupendwa kwani anakuwa ni mtu anayeleta dharau kwa wananchi na anaamini kura yake imetokana na rushwa na sio kitu kingine chochote.

Kwani kilichotokea Tarime ni kuuza utu pasipokuwa na sababu za msingi uliotekelezwa na watendaji kwa ajili ya masilahi binafsi ya watu wachache ambao wanakiharibu Chama kwa jimbo la Tarime Mjini ambalo viongozi wanafanya mambo ya ovyo pasipokuwepo uimara na ubora wa kuleta maendeleo kwa jamii husika.

Hivyo mbunge wa namna hiyo, hafahi na hawezi kuleta maendeleo kwa wananchi kwa kuwa anaamini huu wakati wa kurudisha hela yake na sio kuleta maendeleo jimboni.
Wanasema katumwa na mkulu
 
Hakuna jimbo ambalo rushwa haikutolewa, kilichofanyika ni kuzidiwa kete tu.
Ccm na rushwa ni sawa na mwalimu na chaki, mwanafunzi na kalamu.
 
Magufuli hawezi kufumbia macho rushwa

Umesema kweli. Magufuli hawezi kufumbia macho rushwa. Lakini wengine rushwa kama kawaida. CCM wanampa kazi nguvu sana Rais wetu. Angelikuwa na watu sahihi, wenye nia kama yake na uzalendo kama alionao, bila shaka sasa hivi tungekuwa mbali sana.
 
Na Chacha John

Habari Mwenyekiti wangu na Rais Dk. John Magufuli, pole sana na kazi kubwa ya kuwakomboa watanzania hasa kutokana na kazi kubwa ya kuleta maendeleo makubwa katika miaka mitano ya utawala wako.

Mheshimiwa Rais na Mwenyekiti, tunapenda kukueleza wasaidizi wako uliowapa majukumu katika mkoa wa Mara hasa katika wilaya ya Tarime wanafanya mambo ya ovyo na hata kushindwa kusimamia taratibu na sheria katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Kitendo ambacho wanakuwa ni sehemu ya wanamikakati ya kuchuuza na kulaghua kura kwa wajumbe ili waweze kupanga safu za wagombea ambao wako imara na wenye kuleta mafanikio kwenye jamii.

Kitendo walichofanya watendaji wa Chama hasa katika jimbo la Tarime Mjini ni fedheha kubwa hasa kwa kushiriki kusambaza fedha ili kushinikiza Jackson Kangoye ashinde ni hatari sana kwa mustakabali wa Chama.

Chama kinapaswa kuishi kwa kusimamia maadili na hata kwenda na kasi ya Rais na Mwenyekiti wa Chama, Dk. John Magufuli ambaye yuko mstari wa mbele katika kuleta maendeleo kwa jamii na kuwaondolea madhira makubwa yaliyokuwa nayo.

Uimara na ushupavu wa Rais Dk. Magufuli unapaswa kwenda sanjari na kupata wagombea sahihi kwenye majimbo. Wagombea ambao wanatanguliza mbele maslahi ya Chama na wala si maslahi binafsi kama walivyofanya Tarime Mjini kuhakikisha wanapelekea wanasiasa maslahi ambao hawana uwezo wa kuleta maendeleo kwa jamii yetu.

Mheshimiwa Rais, kilichofanyika Tarime Mjini ni jambo la hatari hasa kwa mgombea kushirikiana na watendaji kununua kura kwa kiasi cha sh. 80000 na sh. 100000 jambo ambalo ni hatari kwa mtu huyo kuleta maendeleo kwa wananchi.

Kitendo hicho kinatokana na mtu huyo atatumia muda mwingi kurejesha hela yake na si kuwatumikia wananchi, kwa kuwa sasa ni wakati wa wananchi kupata watu wanaokaribia usafi wako ambao umeingia Ikulu bila ushikaji au kwa fedha ya mtu bali umeingia Ikulu kwa dhamira moja ya kuwatumikia watanzania na ndio kitu kinachoonekana sasa.

Mheshimiwa Rais, naandika barua hii ya wazi kukueleza ya kwamba kinachoendelea Tarime ni mchezo wa hatari na tunapenda kukueleza tumaini kubwa la wanachama wa CCM ni kwako katika kutupa mwelekeo kwa kuwa wewe ni kiongozi madhubuti na mwenye dira thabiti ya kuleta ya maendeleo kwa Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti na Rais, rushwa ndani ya mchakato wa uchaguzi na kabla ya uchaguzi ndio imeamua mshindi kwa Tarime Mjini na wala si nguvu ya hoja katika kuleta maendeleo kwa jamii ya WanaTarime.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakuomba sana utuokoe na hii dhahama tuliyofanyiwa Tarime kwa fedha ndio kuonekana muamuzi wa matokeo ya kumpata mgombea na si nguvu ya hoja ambayo iwe chachu ya kupata mgombea bora wa ubunge kwa jimbo hilo la Tarime ambalo kuongozwa na upinzani inatokana na hujuma inayofanywa na watendaji wa CCM.
Ccm haifai kabisa twende CHADEMA.
 
Na Chacha John

Habari Mwenyekiti wangu na Rais Dk. John Magufuli, pole sana na kazi kubwa ya kuwakomboa watanzania hasa kutokana na kazi kubwa ya kuleta maendeleo makubwa katika miaka mitano ya utawala wako.

Mheshimiwa Rais na Mwenyekiti, tunapenda kukueleza wasaidizi wako uliowapa majukumu katika mkoa wa Mara hasa katika wilaya ya Tarime wanafanya mambo ya ovyo na hata kushindwa kusimamia taratibu na sheria katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Kitendo ambacho wanakuwa ni sehemu ya wanamikakati ya kuchuuza na kulaghua kura kwa wajumbe ili waweze kupanga safu za wagombea ambao wako imara na wenye kuleta mafanikio kwenye jamii.

Kitendo walichofanya watendaji wa Chama hasa katika jimbo la Tarime Mjini ni fedheha kubwa hasa kwa kushiriki kusambaza fedha ili kushinikiza Jackson Kangoye ashinde ni hatari sana kwa mustakabali wa Chama.

Chama kinapaswa kuishi kwa kusimamia maadili na hata kwenda na kasi ya Rais na Mwenyekiti wa Chama, Dk. John Magufuli ambaye yuko mstari wa mbele katika kuleta maendeleo kwa jamii na kuwaondolea madhira makubwa yaliyokuwa nayo.

Uimara na ushupavu wa Rais Dk. Magufuli unapaswa kwenda sanjari na kupata wagombea sahihi kwenye majimbo. Wagombea ambao wanatanguliza mbele maslahi ya Chama na wala si maslahi binafsi kama walivyofanya Tarime Mjini kuhakikisha wanapelekea wanasiasa maslahi ambao hawana uwezo wa kuleta maendeleo kwa jamii yetu.

Mheshimiwa Rais, kilichofanyika Tarime Mjini ni jambo la hatari hasa kwa mgombea kushirikiana na watendaji kununua kura kwa kiasi cha sh. 80000 na sh. 100000 jambo ambalo ni hatari kwa mtu huyo kuleta maendeleo kwa wananchi.

Kitendo hicho kinatokana na mtu huyo atatumia muda mwingi kurejesha hela yake na si kuwatumikia wananchi, kwa kuwa sasa ni wakati wa wananchi kupata watu wanaokaribia usafi wako ambao umeingia Ikulu bila ushikaji au kwa fedha ya mtu bali umeingia Ikulu kwa dhamira moja ya kuwatumikia watanzania na ndio kitu kinachoonekana sasa.

Mheshimiwa Rais, naandika barua hii ya wazi kukueleza ya kwamba kinachoendelea Tarime ni mchezo wa hatari na tunapenda kukueleza tumaini kubwa la wanachama wa CCM ni kwako katika kutupa mwelekeo kwa kuwa wewe ni kiongozi madhubuti na mwenye dira thabiti ya kuleta ya maendeleo kwa Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti na Rais, rushwa ndani ya mchakato wa uchaguzi na kabla ya uchaguzi ndio imeamua mshindi kwa Tarime Mjini na wala si nguvu ya hoja katika kuleta maendeleo kwa jamii ya WanaTarime.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakuomba sana utuokoe na hii dhahama tuliyofanyiwa Tarime kwa fedha ndio kuonekana muamuzi wa matokeo ya kumpata mgombea na si nguvu ya hoja ambayo iwe chachu ya kupata mgombea bora wa ubunge kwa jimbo hilo la Tarime ambalo kuongozwa na upinzani inatokana na hujuma inayofanywa na watendaji wa CCM.
Hayo yaliyofanyika kuna Jimbo la uchaguzi ambalo mgombea wa CCM hajafanya hivyo??
 
Acha ya Majimbo ya Tarime, Jimbo la Rorya ndilo lililotia aibu kubwa ya rushwa. Walioshika namba 1,2,3 wote wameshinda kwa kutoa rushwa. Tunawataka watu wa Usalama na Takukuru watoe ripoti isiyokuwa na upendeleo kuhusu uchaguzi wa Jimbo la Rorya.
 
Na Ghati Chacha

HII sio Chama Cha Mapinduzi(CCM) ninachokijua na kukulia kwa zaidi ya miaka 30. Chama kilichosimama mstari wa mbele katika kuwakomboa wananchi na unyonge wao, Chama kinachosimama mbele kupinga rushwa hadharani.

Naamini na nitaendelea kuamini CCM ni taasisi kubwa na yanayoendelea kufanyika katika Mkoa wa Mara hasa majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini ni jambo linalopaswa kukemewa na kila mpenda maendeleo na kukitakia mustakabali Chama katika kuyasisimamia maendeleo ya wananchi.

Yaliyofanywa na washindi wa kura za maoni katika majimbo ya Tarime ni wizi mkubwa na yanapaswa kukemewa kwa nguvu zote kwani haikubaliki na haitakiwi kwa CCM kushiriki kwenye ulanguzi wa kura kama uliofanywa na kina Jackson Kangoye kwa Tarime Mjini.

Kiongozi anayenunua kura hafai hata kupendwa kwani anakuwa ni mtu anayeleta dharau kwa wananchi na anaamini kura yake imetokana na rushwa na sio kitu kingine chochote.

Kwani kilichotokea Tarime ni kuuza utu pasipokuwa na sababu za msingi uliotekelezwa na watendaji kwa ajili ya masilahi binafsi ya watu wachache ambao wanakiharibu Chama kwa jimbo la Tarime Mjini ambalo viongozi wanafanya mambo ya ovyo pasipokuwepo uimara na ubora wa kuleta maendeleo kwa jamii husika.

Hivyo mbunge wa namna hiyo, hafahi na hawezi kuleta maendeleo kwa wananchi kwa kuwa anaamini huu wakati wa kurudisha hela yake na sio kuleta maendeleo jimboni.
Huu ni uongo fitna umetumwa na walioshindwa kura za maoni, sasa endelea kumpigia Majungu mshindi wa kura za maoni kisha kamati kuu warejeshe jina la mshindi wa kura 1 ili chadema watetee jimbo lao
 
Acha ya Majimbo ya Tarime, Jimbo la Rorya ndilo lililotia aibu kubwa ya rushwa. Walioshika namba 1,2,3 wote wameshinda kwa kutoa rushwa. Tunawataka watu wa Usalama na Takukuru watoe ripoti isiyokuwa na upendeleo kuhusu uchaguzi wa Jimbo la Rorya.
Khaaa.hzo ndo pumba kabisa.ngoja tuwataftie feni za magazet ya buku
 
Wajumbe wameweka maslahi binafsi mbele
ccm kote Tanzania nzima wajumbe wamekula pesa misaada ya wagombea wote hakuna asiyetoa pesa ingawa wanazidiana katika dau, kama ni tuhuma za Rushwa ni ccm yote inanuka Rushwa, tunawashukuru ccm endeleeni kuwapiga vita ccm wenzenu ili chadema waletewe ccm dhaifu wapate kushinda chaguzi bila usumbufu
 
Huenda huko Dodoma kukaja kuwa na Aibu kubwa kwa kupokea majungu kisha kuwakata watu kwa uonevu
 
Huenda huko Dodoma kukaja kuwa na Aibu kubwa kwa kupokea majungu kisha kuwakata watu kwa uonevu
Msiamin sana hayo wadau mana naona mnatokwa na mapovu kwel yan.hyo threda imepoastiwa ili tujue na cyo kushndana kwa mafombou
 
Back
Top Bottom