SI KWELI Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amepelekwa Afrika kusini kwa ajili ya matibabu

SI KWELI Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amepelekwa Afrika kusini kwa ajili ya matibabu

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Wakuu salaam, Naomba msaada juu ya uhalisia wa taarifa hii inayosambaa mtandaoni kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe ni mahututi na amepelekwa Afrika kusini kwa ajili ya matibabu.

1728230083548.jpeg
 
Tunachokijua
Freeman Mbowe ni Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA ambaye alikuwa ni moja kati ya waasisi wa chama hicho mwaka 1992 na mwaka 2005 alikuwa mgombea wa urais kupitia tiketi ya CHADEMA, lakini pia mwaka 2010 hadi 2020 alikuwa mbunge wa jimbo la Hai mwaka.

Mnamo Oktoba mosi 2024, Freeman Mbowe alihudhuria katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo Mahakama hiyo ilitegemewa kutoa uamuzi mdogo juu ya dhamana ya Boniface Jacob, ambaye hivi karibuni ameshinda uenyekiti Kanda ya Pwani ndani ya CHADEMA.

Kumekuwepo na taarifa inayosambaa mtandaoni ikieleza kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe yupo katika hali mahututi na amesafirishwa kwenda nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu.

Je uhalisia wa taarifa hii ni upi?
Ufuatiliaji wa JamiiCheck kupitia vyanzo vya kuaminika umebaini kuwa taarifa hiyo si ya kweli na haijatolewa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.

Aidha Mkurugenzi wa ltifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje, John Mrema kupitia ukurasa wake rasmi wa mtandao wa X amekanusha juu ya uwepo wa taarifa hiyo akiwataka watu kuipuuza kwani ni uzushi na haina ukweli wowote.

Kadhalika mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kanda ya kaskazini Godbless Lema ameikanusha taarifa hiyo kuwa si ya kweli na kwamba ipuuzwe kwani Freeman Mbowe yupo nyumbani kwake Machame wakipanga mipango ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji.​
Hata ingekua mimi kwa usaliti ule wa wanachama tunakubaliana mtandaoni watu elfu 1 + tukutane kuandamana alafu kwenye maandamano naenda peke yangu hilo tukio kila nikilikumbuka lazima presha iwe inashuka
Hahahaha lazima pressure ipande wakina Erythrocyte walimuuza Mwenyekiti.
 
Waseme tumuombee dua la uponyaji isije taarifa ya ghafla kama mwendazake john
 
Hivi Jf mmeshindwa kuthibitisha kama hii habari ni ya uongo au ukweli ikiwa ni uongo uzi ukafutwa?
 
Moderator wamelala uzi upo page ya 3 sasa
 
Back
Top Bottom