Mwenyekiti wa Chadema Iringa Mjini Frank Nyalusi asema huu ndio wakati muafaka wa Tundu Lissu kuwa Mwenyekiti Taifa, vinginevyo ni majanga

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Iringa Mjini Mh Frank Nyalusi amesema yuko Dar es Salaam kwa shughuli moja tu ya kuhakikisha Tundu Antipas Lissu anakuwa Mwenyekiti wa Chadema.

Nyalusi amemwambia Mwandishi wa Jambo Media kwamba Siasa za Tanzania kwa sasa hazitaki tena kiongozi anayeongea kwa kubembeleza hisani bali Kiongozi anayeongea na Kutenda na huyo si mwingine ni Lissu.

Nyalusi amesema wenyeviti wengi wamesafiri Kutoka majimboni na mikoani kuja kumshawishi Tundu Lisu atangaze kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa.

Source: Jambo TV
 
Ila msigombane kama NCCR MAGEUZI pale Tanga kwenye mkutano wao na ndio ikawa mwisho wa zama za chama hicho kutamba kwenye siasa za nchi hii. Mzee Cheyo wa UDP naye aliletewa za kuleta na kina Jidulamabambasi wakiutaka uenyekiti wa chama hicho nacho kikapoteza umaarufu. Njoo TLP ya Mrema na CUF ya Maalim Seif ni yaleyale kama ya wakati huu kwa CHADEMA. Vyama vinakufa kisiasa kwa kutokusikilizana pamoja. Wenzao CCM wanadunda tu na kofia mbili za mwenyekiti wao, yeyote atakayejitokeza anahangaisha chama atashughulikiwa kisawasawa atulie
 
Ila msigombane kama NCCR MAGEUZI pale Tanga kwenye mkutano wao na ndio ikawa mwisho wa zama za chama hicho kutamba kwenye siasa za nchi hii. Mzee Cheyo wa UDP naye aliletewa za kuleta na kina Jidulamabambasi wakiutaka uenyekiti wa chama hicho nacho kikapoteza umaarufu. Njoo TLP ya Mrema na CUF ya Maalim Seif ni yaleyale kama ya wakati huu kwa CHADEMA. Vyama vinakufa kisiasa kwa kutokusikilizana pamoja. Wenzao CCM wanadunda tu na kofia mbili za mwenyekiti wao, yeyote atakayejitokeza anahangaisha chama atashughulikiwa kisawasawa atulie
 
Waambieni uchaguzi ni mwakani na zimebakia siku tu. Wenzao wanajifua huko wenyewe bado mambo yao hayajakaaa sawa.
 
Hana nidhamu kabisa.
 
Naunga mkono hoja. CCM wamewaonea wapinzani vya kutosha sasa anatakiwa mtu mbabe wa kupambana na uonevu na asiyeogopa kufa. Mbowe apumzike ameshachoka!
 
Waambieni uchaguzi ni mwakani na zimebakia siku tu. Wenzao wanajifua huko wenyewe bado mambo yao hayajakaaa sawa.

Tofautisha uchaguzi na uchafuzi. Tanzania hakuna uchaguzi wa kuhangaisha akili. Acha CCM ajifurahishe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…