Mwenyekiti wa Chadema Njombe: Nahisi CCM wana tawi lao huku

Mwenyekiti wa Chadema Njombe: Nahisi CCM wana tawi lao huku

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Njombe, Rose Mayemba amesema anahisi CCM wana tawi lao CHADEMA. Kupitia mtandao wa X mwenyekiti huyo amenukuliwa akisema "Kwa fedha nilizoshuhudia zikimwagwa USIKU kucha,nikikumbuka fedha zilivyokuwa zinamwagwa Njombe, naanza kuhisi CCM wana tawi lao huku kwetu"

1000019553.jpg
 
Hivi leseni yake ya kuuza mkaa kwa nini huwa wanai-renew?
 
Tetesi toka Twitter (Dr Slaa aliizungumzia hilo suala) zinasema kuna asali ya 12B imekuwa injected chamani. Kadri siku zinavyoenda ninaanza kuamini zile tetesi toka Twitter za 12B.
 
Wakati wa uchaguzi wa Kanda ya Nyasa, Lissu alisema kuwa Abduli amepenyeza pesa nyingi ili mtu wake ashinde. Baada ya kushindwa uchaguzi, mtu aliyekuwa anampigia debe akatimkia kwa mama yake Abduli. Sasa ni nani alikuwa anapenyezewa hizo pesa za Abduli? Na huyo huyo ndie alikuwa anapigiwa debe na Rose! Hii ni gaslighting ya hali ya juu. Katika hili, alitakiwa achukue video au hata picha za hayo matukio ili azitumie kama ushahidi. Au atuambie alichukua hatua gani na nani walikuwa wanatoa hizo rushwa.

Hawa wanatumia falsafa ya Goebbels aliyesema " Make the lie big, make it simple, keep saying it and eventually they will believe it". Na ukitaka uaminike zaidi, ijenge kwenye kaukweli kadogo. Hapa kwetu hamna uchaguzi ( hata wa monita wa chekechea ) ambao hauna tuhuma za rushwa. Ndio maana ukitaja rushwa unaaminika kwa sababu ipo katika kila uchaguzi na watanzania wameikubali hali hio.

Amandla...
 
Back
Top Bottom