Mwenyekiti wa UVCCM aliyesema Peter Zacharia katekwa na watu wasiojulikana, apandishwa kizimbani

Mwenyekiti wa UVCCM aliyesema Peter Zacharia katekwa na watu wasiojulikana, apandishwa kizimbani

Kamanda kachemka kesi ya kumfurahisha Mkuu hiyo itaisha hivyo hivyo...
 
Hii CCM haingalii sura ya mtu acha sheria ichukue mkondo
Chanzo cha tukio na ulichoandika hapa hakieleweki
Inasikitisha sana mkuu wa mkoa anatoa taarifa za uongo eti walienda kujaza mafuta wakati sheli ilishafungwa
Mkinyimwa hela mnaforce kupata hela sio
 
Siasa ya sasa kwa hapa Tanzania hairuhusu kukojoa huku umesimama ni lazima uchutame hata kama ni mwanaume.
 
Chanzo cha tukio na ulichoandika hapa hakieleweki
Inasikitisha sana mkuu wa mkoa anatoa taarifa za uongo eti walienda kujaza mafuta wakati sheli ilishafungwa
Mkinyimwa hela mnaforce kupata hela sio
Utetezi wao unaokuja siku zote ni kana kwamba mtu anayeandika kwenye maji yanayotiririka akitaraji atayaona maandishi yake.
 
Angalau sasa ametufahamisha watu wasiojulikana ni akina nani!
 
Sasa wanamshtaki kwa kosa lipi wakati zakaria hajapandishwa kizimbani,je kama zakaria atasema walitaka kumteka na akawazidi nguvu itakuaje?
Wangesubiri zakaria ashindwe kwanza kesi ndio wadeal Nae.
 
Unaposhangilia sheria kandamizi kwa sababu unafikiri zitamkandamiza mpinzani tu, kuna siku utajikuta zinakukandamiza hata wewe.
 
Danganya toto, watafuta kesi....... Nolle Prosequi ............ ndiyo inawalinda CCM
Mkuu habari nilizo nazo toka Tarime ni kuwa sasa hivi kuna mtifuano mkali kati ya chama chao na bwana mkubwa aliyetoa lile tamko kuwa walifuata mawese pale na ghafla wakashambuliwa watu wao.
Chama chao kinasema hawakubali uongo huo wakati mashuhuda walioona tukio lile wanasema ukweli ulio zagaa mjini pote hivyo kukubaliana na uongo huo in kukimaliza chama chao hapo na mkoa mzima.
Ajabu ni kuwa kwenye jambo hili WAKURYA wameweka utikadi pembeni na kusimamia ukweli.
Bita ni bita mura!
 
Namba za kirumi tamu kuzisoma eise!! ccm mbele kwa mbele
 
Sasa wanamshtaki kwa kosa lipi wakati zakaria hajapandishwa kizimbani,je kama zakaria atasema walitaka kumteka na akawazidi nguvu itakuaje?
Wangesubiri zakaria ashindwe kwanza kesi ndio wadeal Nae.
Panic baba! Huwa mtu akikumbwa na panic anaweza kunyea suruali akidhani kavua kwa vile kachutama tuu
 
Tarime. Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Wilaya ya Tarime, Godfrey Francis atapandishwa kizimbani muda wowote leo Julai 2, 2018 baada ya kukamilika kwa mahojiano na polisi.

Francis anatuhumiwa kutoa taarifa za uwongo katika mitandao ya kijamii kuhusu sakata la kukamatwa kwa mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Zakaria, Peter Zakaria.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe amethibitisha kukamilika kwa mahojiano ya awali kuhusu tuhuma zinazomkabili kiongozi huyo na kusema atasomewa mashtaka wakati wowote kabla ya shughuli za mahakama kumalizika leo.

"Kweli tutamfikisha mahakamani kujibu tuhuma dhidi yake. Kazi ya Polisi ni kuhoji, kupeleleza na kufikisha mahakamani tuhuma zozote za jinai. Tumetimiza na kukamilisha wajibu huo," amesema Kamanda Mwaibambe.

Kiongozi huyo ambaye juzi alihojiwa na polisi kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 6:00 mchana tayari yuko katika ukumbi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Tarime akisubiri kusomewa mashtaka.

Akizungumza na MCL Digital leo Julai 2, Francis amethibitisha kuwa alitakiwa kuripoti polisi leo na alipofika akaelezwa kuwa anapelekwa mahakamani.

"Ndio hivyo nasubiri kusomewa mashtaka; natuhumiwa kusambaza taarifa za uongo kupitia mitandao ya kijamii kuhusu tukio lililomtokea Zakaria (Peter Zakaria). Tunamsubiri hakimu bado ana mashauri mengine," amesema Francis.

Habari zaidi, soma=>Tarime, Mara: Mmiliki wa mabasi ya Zacharia awapiga risasi maafisa wa Usalama wa Taifa, ashikiliwa na Polisi

Chanzo: Mwananchi

UPDATES:

Tarime. Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Wilaya ya Tarime, Godfrey Francis leo Jumatatu Julai 2, 2018 amepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Tarime, kushtakiwa kwa kosa la kusambaza taarifa za uwongo kwa njia ya mtandao wa kijamii.

Taarifa hizo ni kuhusu kukamatwa kwa mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Zakaria, Peter Zakaria.

Kiongozi huyo ambaye jana alihojiwa na polisi kwa saa kadhaa amesomewa mashtaka na mwendesha mashtaka wa polisi, Kazeni Mrita.

Mbele ya hakimu mkazi Veronica Mugendi, Mrita amedai mshtakiwa amesambaza taarifa hizo mchana wa Julai Mosi, 2018 kwa kuandika kuwa Zakaria alitaka kutekwa na watu wasiojulikana ambao hata hivyo aliwazidi nguvu kwa kuwajeruhi wawili kati yao.

Francis anayetetewa na wakili Onyango Otieno ameachiwa kwa dhamana hadi Jalai 30, 2018 shauri hilo litakapotajwa.

Ametimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja amesaini hati ya dhamana ya Sh2 milioni.
KWANI ALIPOTOA TAARIFA WAO WALIKUWA WAMESHASEMA KUWA WAKO NAYE? KAMA SIVYO ALIKUWA SAHIHI.
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Back
Top Bottom