Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Eh kumbe kuna wanasiasa wanaifanya Tanzania kama geto? Hawa si wa vyama vya upinzani kweli?
Mh namuona kama Lissu, Lema na wengineo linawahusu sana
===============
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Songwe, Fatma Hussein, anasema anakerwa na baadhi ya wanasiasa ambao wanaifanya Tanzania kama ‘gheto’ na siyo makazi rasmi kutokana na familia zao kuishi nje ya nchi.
Fatma ameyasema hayo leo Februari Mosi, 2025 alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari mjini Songwe, kwa lengo la kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha mkutano ulimalizika hivi karibuni wa Nishati Afrika.
Amesema wanasiasa hao ndio vinara wa kuchochea na kutoa lugha zinazolenga kudhoofisha utulivu wa nchi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Soma Pia: Songwe: Matukio Yanayojiri Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Ameeleza wanapozungumzia suala la uchaguzi, wanazungumzia amani na utulivu wa nchi, "Mtu asiye kuwa na familia hapa nchini anajua hata akivuruga mambo, yeye familia yake ipo salama na kesho ataka tiketi anaondoka, ndio maana nasema lazima Watanzania tuwe makini na hawa watu," amesisitiza Fatma.
Mh namuona kama Lissu, Lema na wengineo linawahusu sana
===============
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Songwe, Fatma Hussein, anasema anakerwa na baadhi ya wanasiasa ambao wanaifanya Tanzania kama ‘gheto’ na siyo makazi rasmi kutokana na familia zao kuishi nje ya nchi.
Fatma ameyasema hayo leo Februari Mosi, 2025 alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari mjini Songwe, kwa lengo la kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha mkutano ulimalizika hivi karibuni wa Nishati Afrika.
Amesema wanasiasa hao ndio vinara wa kuchochea na kutoa lugha zinazolenga kudhoofisha utulivu wa nchi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Soma Pia: Songwe: Matukio Yanayojiri Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Ameeleza wanapozungumzia suala la uchaguzi, wanazungumzia amani na utulivu wa nchi, "Mtu asiye kuwa na familia hapa nchini anajua hata akivuruga mambo, yeye familia yake ipo salama na kesho ataka tiketi anaondoka, ndio maana nasema lazima Watanzania tuwe makini na hawa watu," amesisitiza Fatma.