Mwenyekiti wa Walimu Wasio Na Ajira (NETO) Joseph Paulo anadaiwa kukamatwa na polisi mkoani Geita

Hili ni kweli kabisa.
Watu wanatakiwa kujua dunia ya sasa hauwezi kutumia mbinu zilizotumiwa na wakina Lenin, Marx au wale wa Luddism. Hichi ni muhimu sana kujua stadi ya kudai na kupokea haki yako.
 
Very true
 
Hiyo sababu ya pili ni ya Ukandamizaji tu. Nsons kwa awamu hii ndiyo imeanza kuwa sababu ya kuwashikila watu kinyume cha sheria.

Watu wanaotoka hadharani kuomba ulinzi kuwa maisha yao yako hatarini huwa hawapewi huo ulinzi.
Tuishi na sababu ya kwanza tu kiongozi
 
Umejitahidi kuandika Big Up japo nawe ni wa mlengo ule
Mtu yoyote ambaye hajawahi kushiriki kuanzisha mgomo shule, hawezi kufanya hilo jambo akafanikiwa. Hiyo ni haiwezekani lazima atazingua tu maana hana alichowahi kujifunza na wala haioni hatari iliyo mbele yake.
 
Kwahiyo Mobout Sese seko ni sawa na chama letu pendwa sii ndio
 
Hamna njia nzuri ya kuanzisha jambo cha msingi wameanza kudai wanachokiamini
Zipo Mkuu, kwa kadiri ya imani.yako ilivyo soma vitabu vya imani yako kujifunza namna watu walizidai haki zao au kusisitiza mambo fulani fulani. Wote waliojifanya manunda walikufa vifo vya ajabu sana.

Mimi ni Mkristu, najifunza kupitia biblia namna watu waliozingua utawala walipata mapigo na namna waliotumwa na Mungu kuonya walivyoonya kwa adabu na unyenyekevu.

Huko unapata namna yakufanya stadi tofauti tofauti za maisha, mfano Yohana Mbatizaji kama sio ununda wake asingekatwa kichwa, pia manabii waliomuongoza Mfalme Daudi kama sio adabu zao basi wasingeweza kuishi muda mrefu. Walitumwa na Mungu na bado wakawa na adabu sembuse wewe mwanadamu unayetumwa na hisia zako unakosa adabu lazima ukipate kipindi kigumu cha maisha.

Ni mambo magumu.
 
Mtu hana ajira inakua ndio fursa kwao kumnyanyasa uzuri malipo yapo hapa hapa Duniani..
 
Kama chawa wameshamiri kila.koma,tutapata wapi haki za kiraia
 
kidumu sana,inabidi tuibipu serikali kwa maandamano ya amani.
"haki na usawa kwa maendeleo endelevu"
 
Nina uhakika hata jalada lake hawajaliandika kosa lake ni nini?
Hii ndo Tanzania kujengea wanachi wake hofu serikali inaweza sana!

Mwenye ajira anamuonea wivu asiye na ajira hadi anaamua kumkata 😁
 

Attachments

  • IMG_6274.jpeg
    132.8 KB · Views: 1
Mambo huanza hivi hivi - watu washajichokea na hawa CCM.
 
kUmekucha na dogo ataendelea kuwa NETO daima milele maana serikali yetu haijazoea kuona walimu wajasiri kama yeye
 
Jina lenyewe la KAHEZA unaweza kulikosa ndani ya mikoa ya Tanzania isipokuwa hapo nchi jirani.
 
We ni mjinga sana vijana kama nyie ni hasara kwa taifa nikuulize hao waliomuua yohana mbatizaji waliishi milele
 
Wanataka wampoteze na wapote Neto. Pole sana kwake
 

Unajidanganya Sana ndugu.

Duniani kote kabisa uzoefu unaonyesha kwamba Umma haujawahi kushindwa jambo lolote lile pale umma huo unapoamua kwa dhati kabisa ya mioyo yao kutekeleza jambo hilo.

Rejea yale machafuko yaliyotokea katika nchi za kiArab kati ya Mwaka 2011 hadi 2015 kule Tunisia, Libya, Misri, n.k.
Mlipuko wa Vuguvugu lile hatari ulianzia nchini Tunisia, sababu zikiwa ni UKOSEFU WA AJIRA KWA VIJANA.
Rejea pia kule nchini Bangladesh, Mwaka jana wa 2024 Waziri Mkuu wa nchi hiyo Hasinna lilimkuta jambo huko nchini Bangladesh hadi akalazimika kuokoa nafsi na kukimbilia nchini India, hadi leo hii tunapojadili suala hili bado yupo huko India. Sababu ya yote haya ni UKOSEFU WA AJIRA KWA VIJANA.

Aidha, hata mlipuko wa Generation Z kwa majirani zetu wa hapo Kenya, sababu ni UKOSEFU WA AJIRA KWA VIJANA

Hivyo Basi, suala hili la Ukosefu wa Ajira kwa Vijana MUST BE HANDLED WITH GREAT CARE!
The Regime of this country Must be very careful in dealing with this Problem of the Youth Unemployment.
Matumizi ya nguvu kubwa hayana nafasi kwenye suala la Utatuzi wa tatizo hili, badala yake AKILI KUBWA, HEKIMA na BUSARA ndiyo silaha sahihi zinazopaswa kutumika katika kutatua Mgogoro huu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…