Dada Evarm, sio wanaume tu waio waaminifu... siku hizi dunia imeisha kabisa tena sana, Mimi ni mwnaume na yaliyokukuta wewe yamenikuta pia tena yalikuwa mabaya sana... msichana wangu alikuwa anakuja nyumbani kwangu na simu zinapigwa kama zilivokuwa zinapigwa za huyo mtu wako, ukiuliza story ni zile zile ulizopewa wewe, udanganyifu..udanganyifu... baadae nikaagwa kuwa mchumba wangu anaenda kwa mjomba wake mahali fulani, alipofika huko mawasiliano yakawa mgogoro, anapatikana dk 5 au kumi tu kwa siku nzima, kumbe yupo kwa mwanaume mwingine na ni X wake wanakula raha...mungu hamfichi mnafki, siku ya sku yule mwanaume akashuku akanipigia simu kuuliza kwa nini namsumbua mtu wake? maelezo alopewa ni kuwa mimi jamaa tu flan nasoma na huyo mdada na eti ninamtaka ila yeye hanitaki, lakini akinipigia simu honey na sweete kama kawa... baada ya mambo kubumbuluka dada akajihami kwa kunipigia simu na kunitukana matusi ya nguoni kuwa mi si kitu wala nini, na wakati huo nilikuwa namsaport kulipa gharaza zake kadhaa za chuo maana alikuwa anasoma na pia nilikuwa namsomesha mdogo wake chuo nikijua naanda familia yangu ya baadae.
Yule X alipokutana na haya akamfukuza akamwambia hamtaki, akarudi kwangu akalia sana eti shetani alimpitia na sijui kwa nini alisema vile na kunitukana.... lazima niseme mimi ni mtu wa ajabu maana nilimsamehe na tukaaza upya uhusiano japo alinipunguzia kasi ya kumpenda lakini bado nilijituma kwake...
Nataka nikuambie kitu nilichojifunza, huyu dada hakubadilika hata na aliendelea kunisumbua kila kukicha na wanaume, kila siku usiku hata wa manane ni simu za wanaume zenye mandhari ya mapenzi pamoja na sms amabazo zikiingia tu zinafutwa, niliumia sana na kujitahidi kueleaza hisia zangu kwake juu ya ninavyojisikia, akiniumiza ataliaa na kusema amekosa na hatarudia lakini hazipiti siku mbili kesi ni ile ile... alinitesa na alinitesa sana maana mimi sio mtu ninayekata tamaa haraka.. kila siku nilijipa moyo labda kesho mungu atamdadilisha lakini haikuwa hivyo zaidi ya miaka 3 aliendelea kunitesa tangu nilivo mrudia baada ya kutoka kwa X wake....hatimaye mwishoni nilipiga moyo konde ni kasema IMETOSHA!!! NikaQuit.
Sasa dada amechoka umri unaenda na wale walokuwa wanamdanganya hawapo tena na hakuna wa kumuoa...ananisumbua kila siku na namwambia haitakuja kutokea mimi kumwoa hapa duniani.. analia lakini mimi moyo ni mtupu juu yake, sina feelings zozote!! Am done with her..
napenda kukuambia:-
1. kama mtu ameanza kukufanyia hayo sasa hataacha milele, maana wengine wanafanya haya ndivyo walivyoumbwa ndivyo walivyo!!! ataendelea kukudanganya tuuuu huko mbeleni, ameshaonja asali atataka kuchonga mzinga, so please usifanye kosa la kumrudia hata utajuta
2. inauma sana na najua inauma...ilinichukua mwaka mzima tangukumwacha na japo kaunza kusahau, lakini kama ukiwa na nia utaweza kumsahau...njia rahisi kata mawasilianao nae, usiruhusu akupigie simu wala akutumia email tangu sasa..
3. usiingie kwenye mahusiano mapema sasa hivi...jipe muda kuponya moyo wako na baada ya muda miezi 6 au mwaka ukiwa umepona jaribu kuanza mahusiano mapya...ukiingia sasa hutasahau mana wingu la ulichofanyiwa litakuwinda popote uendapo, so please don't make that mistake.
4. mda mwingine ukianzaisha uhusiano usijitoe kwa asilimia 100% kwa mwanaume, binadamu wote (wake kwa waume) wakijua wanapendwa ndivo walivo na wanadhani no way out for you...penda ila pia jiwekee msimamo fulani ambao mtu wako ataunote..usikubali akutese hata..
All in all pole sana, yanawakuta wengi na mimi ni mhanga mmoja wapo...katika kipindi hiki Omba sana mungu hata kama imani yako ni ndogo maana MKe/Mme bora hutoka kwa bwana... anaweza kuchelewa kujibu lakini ukiomba kwa imani atajubu..
Pole na narudia tena Pole sana..