gimmy's
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 3,312
- 3,345
Nawasalimu wanajamvi wote hapa javini,
Kwanza naomba nianze kwa kunukuu maneno ya waziri wa fedha Mr Mwigulu alietuambia watanzania kwamba,"kama mtu anataka kuhamia Burundi kwasababu ya tozo kwenye miamala na ahame".
Ndugu zangu leo nimelazimika kupoteza muda wangu ili mradi tu nikwepe kulipa kodi ya dhuluma iliowekwa na serikali kwenye miamala ya simu ili kuumiza wananchi.
Japo najua Mr mwigulu hakuniona ili aone kwamba sitahama nchi kwenda Burundi lakini najipa moyo hata kama sio direct lakini ujumbe utafika na nimesusia kulipa hii kodi ya dhuluma,haiwezekani na haitawezekana kwa mtanzania wa kawaida kulipa pesa nyingi kiasi hiki,
Mr Mwigulu wewe baki na kiburi chako na sisi tuache na umasikini wetu,
Ninyi wanasiasa mnatuambia sisi tulipe kodi zenye kuumiza wakati ninyi kuanzia spika,raisi,waziri mkuu,wabunge,majaji wote hamlipi kodi.
Mnatuhamasisha tulipe hizi tozo ili mjenge barabara halafu kesho wabunge wanakuja kutafutia kura barabara tulizojenga wenyewe kwa tozo za kuumiza ilihali wabunge hawalipi kodi kabisa.
Nataka ujumbe huu ufike kwa mama mh Samia, kama kweli aliwapima mawaziri wake urefu wa mabega kama alivyosema pindi anawaapisha,basi ampime Mr mwigulu leo aone namna mabega yake yalivyo panda juu.
Asante.
Kwanza naomba nianze kwa kunukuu maneno ya waziri wa fedha Mr Mwigulu alietuambia watanzania kwamba,"kama mtu anataka kuhamia Burundi kwasababu ya tozo kwenye miamala na ahame".
Ndugu zangu leo nimelazimika kupoteza muda wangu ili mradi tu nikwepe kulipa kodi ya dhuluma iliowekwa na serikali kwenye miamala ya simu ili kuumiza wananchi.
Japo najua Mr mwigulu hakuniona ili aone kwamba sitahama nchi kwenda Burundi lakini najipa moyo hata kama sio direct lakini ujumbe utafika na nimesusia kulipa hii kodi ya dhuluma,haiwezekani na haitawezekana kwa mtanzania wa kawaida kulipa pesa nyingi kiasi hiki,
Mr Mwigulu wewe baki na kiburi chako na sisi tuache na umasikini wetu,
Ninyi wanasiasa mnatuambia sisi tulipe kodi zenye kuumiza wakati ninyi kuanzia spika,raisi,waziri mkuu,wabunge,majaji wote hamlipi kodi.
Mnatuhamasisha tulipe hizi tozo ili mjenge barabara halafu kesho wabunge wanakuja kutafutia kura barabara tulizojenga wenyewe kwa tozo za kuumiza ilihali wabunge hawalipi kodi kabisa.
Nataka ujumbe huu ufike kwa mama mh Samia, kama kweli aliwapima mawaziri wake urefu wa mabega kama alivyosema pindi anawaapisha,basi ampime Mr mwigulu leo aone namna mabega yake yalivyo panda juu.
Asante.