Mwigulu amkingia kifua mkurugenzi fisadi



Mkuu wewe ujatoa siri za vikao
 
enzi za sokoine wahujumu uchumi walikuwa wanazitupa baharini na kuzitelekeza, sasa huyu fisadi wa majina ya wazalendo anapiga blah blah eti wanaescrow walipe kodi siku 30, kumbe ilikuwa janja ya kupewa helicopta ya mikutano!
 
Mleta unatumia vibaya usichana wako
 
Huwezi ukawa kiongozi ndani ya Chama cha mafisadi na wewe usiwe fisadi,ni viumbe vya majini pekee ndivyo vinavyoweza kuishi maji ya chumvi visiwe na chumvi.
 
Copy and paste kutoka uzi kama huu Mwigulu anasema,

Ndg wana jf.
Salaam. Naandika kujibu uzushi wenye malengo ya kuchafuana kisiasa na usiozingatia maadili ya uongozi kwenye uzi wenye kichwa cha habari hapo juu.
Kwanza maelezo yanasema nimemtuma RC Kone akazime maazimio ya madiwani yenye lengo la kumwondoa DED. Hii sio kweli, madiwani katika kikao chao bila uwepo wangu walikubaliana kumwita RC na walimtuma Mwenyekiti wa Halmashauri Just Makala akiwa na madiwani wakiwa watatu mpaka Singida wala sio kwa simu kwenda kumwomba aende Iramba kukutana nao. Wala sio mbunge aliyemtuma RC kwenda Iramba kukutana na madiwani. Walimpomkuta RC ndipo wakapanga kikao hicho tangu jtatu kuwa wakutane ijumaa yaani leo.


Pili, madiwani walimwomba RAS kupitia kikao chao cha ijumaa aende Iramba jumapili kabla ya RC. Wala hakuwa mbunge aliyeomba RAS na RC akazime maazimio.
Tatu, mimi sina record ya kubeba wahalifu na wala sijamtisha Diwani hata mmoja.

Ninachowambia madiwani nawambia na wana jf na watanzania, mimi ni kiongozi wa kitaifa nashiriki vipi kumhamisha mtu aliyeiba? Yaani ni wilaya ipi anakofaa mtu aliyeiba? Mimi kiongozi wa Kitaifa kwanini niwapelekee wilaya mwingine mtu ambaye ni mwizi? Nawambia madiwani wangu tuweke tuhuma hadharani na ushahidi hadharani ili ikothibitika ameiba afukuzwe sio azimio la kumhamisha. Hii kuhamisha ndio inayosababisha wizi nchi nzima cos wezi wanaiba eneo wanaacha legacy wanahamia eneo lingine kwenda kusuka kikosi cha wezi na baadae wanaiba wana hama tena mwisho nchi nzima kunakwepo mtandao wa wezi. Kamahuku ni kulinda wezi basi nadhani aliyeandika hanijui vizuri yeye antumwa tu akidhani hiyo inanichafua. Msimamo wangu sio kuazimia kuhamisha mwizi bali asomewe tuhuma ushahidi utolewe ikithibitika afukuzwe.
Ndg wana jf ukimhamisha mwizi akaendelea kuwa mtumishi ataanza kutumia kodi za umma, gari la umma, mafuta na posho fedha za walipakodi kuja Iramba kujibu. Tuachane na fikra za kizamani kuwaza kuhamisha mhalifu na mwizi bali hatua zichukuliwe palepale alipoiba
Says
Mwigulu Nchemba
 
Tuntemenke sa_ga upo mkuu?toka uanye kumphotoa picha mhe umenawiri sana mkuu?ila tabia ya usalit haitokuacha
 
Mwigulu hana mamlaka ya kuwatisha madiwani.kisheria madiwani wana haki ya kukataa utendaji mbovu wa mkurugenzi wa halmashauri hivyo wasiogope waendelee na mipango yao.
 
Mwigulu amejibu.
Ila nashangaa amepataje details zote kama hahusiki ?
Pia nampongeza kwa majibu japo sio majawabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…