Elections 2015 Mwigulu Nchemba: Huu Unyama Una baraka zote za Dr. Slaa na genge lake

Elections 2015 Mwigulu Nchemba: Huu Unyama Una baraka zote za Dr. Slaa na genge lake

naona unajitahidi kuwaambia wananchi kinachoendelea hapa nchini kwa kuwaambia kuwa timu uliyonayo ya wahanga wa kipigo ni matokeo ya vurugu za cdm sasa ukishawaambia usisahau kuwaambia pia kuna wabunge haines kiwia na machemli wana majeraha makubwatu vichani mwao kwaajili ya kukatwa mapanga na ccm pia usisahau kuwaeleza jinsi ulivyowalipua cdm kwa bomu pale soweto na kusababisha watu wanne kupoteza maisha na wengine zaidi ya mia moja kubaki na vilema vya maisha pia usisahau kuwaambia wananchi uliyotengeneza ile video feki ya lwakatare pia uwaambie kuwa huyo tesha alimwagiwa tindikali na kada wa cdm henri kileo na mlimfikisha mahakamani lakini mahakama ikamwona hana hatia sema yote usiache hata moja hata kama lile la olasiti ulilipua wewe waambie tu mwisho watakuonea huruma wataichagua ccm hukumbuki ulipomleta tesha arusha na kuwaonyesha wananchi kazi mbaya ya cdm ulivyopata kura nyingi?? hadi ukazoa majimbo yote manne ya uchaguzi usiogope wewe sema hata kalenga utapata.:israel:
 
Mkuu wanalipwa. Take this one; pale maeneo ya mwananyamala kwa mama zakari upande wa kulia kuna mtaa una gereji bubu... Mtaa ule kuna makada-wa CCM ni almost siku ya nne leo wanapita nyumba hadi nyumba kwa malengo yafuatayo: mosi ni kujua wanachama wa ccm ni wangapi na pili wanashawishi kama si mwanachama uchukue kadi ya ccm. Kazi hii hufanywa na mjumbe na kijana toka ofisi za ccm m/nyamala ujiji pale. Wanaongozana na mwanamke ambaye anajitambulisha ni mhanga wa siasa chafu za chadema kwa lile Bomu la Arusha. Hama mkono mmoja na upande wa uso kama ameungua. Yeye hujieleza kwanza na ndipo mjumbe hukuomba ujiunge ccm. Sijui kama ni mkakati wa uchaguzi wa serikali za mtaa au lah! That lady anakunja fedha pale ofisi za ccm ujiji.

Duuh,ama kweli umasikini ni dhambi kubwa. Lakini yupo mwenye sisi viumbe(MUNGU) atatutetea dhidi ya dhuluma na unanyanyasi huu wa ccm.
 
ukibishana na mjinga na wewe pia utakuwa mjinga na kukosa hekima na busara, poor mwigulu ni kama dekio au fagio la chooni, unajua wakati mwingne kwel ccm inatia huruma sana na hasira sana bac sisi werevu tupotezee huu ujinga wa hao watu nina imani kubwa na watanzania watawapuuza hao vicha wenye uchu na madaraka

hivi huyu si ni mjumbe wa bunge maalum la katiba na muda huo wenzie wapo kwenye semina ya kujadili kanuni jamani..?ina maana ccm haina watu wengine wa kufanya kampeni..then inasikitisha kuona mtu anaejinasibu kua ni mchumi daraja la kwanza na pia naibu waziri wa wizara nyeti anafanya siasa za udhalilishaji wa utu wa mwanadamu...hakika hii dhambi ni kubwa sana
 
Hakuna aibu kwa CCM kama hiyo ya kutumia ulemavu wa watu kama mtaji kwao. Hata hao walemavu ni hopeless kukubali kutumika hivyo. Yawezekana CCM ingeshinda kalenga ila kwa mtaji huo pamoja na muwaji mwigulu nawahakikishieni ccm kalenga hamtashinda ili idhihirike kuwa ni nani anayeratibu mauwaji ya Watanzania hususa wanaCHADEMA.
 
Siasa za jinsi hii ndizo zinazidi kuchochoea zaidi vita.Kwa maana nyingine Mwigulu anabariki vita
 
Hawa jamaa wanaotembezwa na ulemavu wao namna hiyo sijui hata wanajisikiaje mioyoni mwao! Unawezaje kumruhusu mwanasiasa kutumia ulemavu wa kiwango hicho kama mtaji wake kisiasa wakati huo huo ukiwa unaonyeshwa kama picha mbele za watu? Au kwa wenzetu hawa kwao hii ni ajira kwa maana kwamba wanajiingizia kipato kwa kuonyeshwa hadharani namna hiyo?

kama CDM walivyoufanya msiba wa mwangosi kuwa mtaji wa kisiasa! ngoma droo.
 
Mwigulu unacho kifanya sii cha kistaarabu kugeuza matatizo ya watu siasa ,,.unalaana wewe
 
Chadema ni sawa na Alshabaab tu.

Viongozi wao wanatumia maisha ya watu kama mtaji wa siasa
Kuna ushahidi gani uliopo hapo, Kwa hiyo mnataka CDM waje na CD za Mwangosi, Yule mwenyekiti wa USA river aliyechinjwa na vijana wa CCM, na pia waje na picha za mabomu ya Arusha. Mwigulu usitumie matukio kama hayo kwanza ni mwiko kutumia mwanadamu kama kielelezo cha kile unataka kufikisha.
 
Angewaeleza jinsi polisi walivyotoa ushahidi mahakamani kuwa alikodisha kundi la kufanya Vurugu kule Singida kijiji cha ndago kwenye mkutano wa CHADEMA na kusababisha mauaji ya kijana mmoja mtoto wa kiongozi mwenzake wa CCM

Naona kihehere na kisebusebu kimekupungua siku hizi...maana wee jamaa ulizidi umbea mpaka basi
 
Back
Top Bottom