Mwili wa bondia wakwama MOI, deni la Sh milioni 6 latajwa, mabondia wajichangachanga

Mwili wa bondia wakwama MOI, deni la Sh milioni 6 latajwa, mabondia wajichangachanga

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Hadi kufikia asubuhi ya leo Ijumaa Februari 11, 2022 mwili wa aliyekuwa bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Vincent Mbilinyi umeshindwa kutolewa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya mazishi kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kuna deni la Sh milioni sita za matibabu yake.

Mbilinyi ambaye alifikwa na umauti juzi Februari 9, alfajiri akiwa hospitalini hapo kwa zaidi ya miezi miwili akipatiwa matibabu kufuatia ajali ya bodaboda aliyopata Desemba 3, 2021.

Ndugu zake ambao walikuwa wakimuuguza muda mwingi wameshindwa kulipia gharama za matibabu aliyokuwa akipatiwa, ndiyo maana walifuatilia taratibu za kutoa mwili huo hospitali hapo kwa ajili ya mazishi lakini hawakufanikiwa.

Baadaye taarifa za mtandao wa @bongoboxingsafari ukaeleza kuwa kuna jitihada zinafanyika zikiongozwa na mwamuzi wa ndondi, Chaulembo Palasa na mwalimu wa mchezo huo, Super D lakini bado hakuna uhakika wa kuupata mwili.

Inaelezwa kuwa waliambiwa angalau wawe na Sh milioni mbili kisha ndiyo wapeleke maombi badala ya kwenda mikono mitupu, na tayari wameandika barua ya kupata msamaha wa deni hilo kwenda kwa mkurugenzi wa MOI.

------------------------

Ofisa Habari MOI, Parrick Mvungi alipoulizwa kuhusu hilo, alisema: “Ni kweli huo mwili upo, ndugu zake walikosea wakaenda kuomba katika uongozi wa Muhimbili, hivyo kukawa na mkanganyiko kidogo, lakini walielekezwa wakaja MOI.

“Jana nilionana nao wale viongozi wa ngumi na ndugu wa huyo bondia, nikawaelekeza utaratibu wanaotakiwa kuufanya, walikosea tu taratibu. Nafikiri wakikamilisha utaratibu watakabidhiwa, Serikali imeshasema hatutakiwi kuzuia mwili kisa mgonjwa alikuwa anadaiwa. Naamini wakikamilisha taratibu inavyotakiwa watakabidhiwa mwili wao."

Mbilinyi.JPG


GEDC0286.jpg
 
RIP
Wamuhurumie tu,huyu mpiganaji wa mtaani tu mil 6 parefu sana.
Gharama za matibabu Muhimbili sio rafiki.
Prof Jay nae anaomba msaada na ubunge wote aliotumikia.
 
Sio mabondia tu asilimia kubwa ya watu maalufu wanaishi nje ya Maisha yao halisi
 
RIP
Wamuhurumie tu,huyu mpiganaji wa mtaani tu mil 6 parefu sana.
Gharama za matibabu Muhimbili sio rafiki.
Prof Jay nae anaomba msaada na ubunge wote aliotumikia.
Jay hajaomba msaada ni mashabiki na wadau wamehitaji wenyewe kuchangia chochote kwenye matibabu yake ni baada ya kuskia jamaa anapurusha karibia tsh 4m per day kwa kujitibia.
 
jay hajaomba msaada......ni mashabiki na wadau wamehitaji wenyewe kuchangia chochote kwenye matibabu yake.....ni baada ya kuskia jamaa anapurusha karibia tsh 4m per day kwa kujitibia.....

Familia yake kupitia mkewe na mdogo wake wameomba kishikwa mkono...
 
baada ya sisi mashabiki na wadau wa mume wake kumshinikiza afungue milango ya watu tuchangie chochote kwenye matibabu ya mwanetu

“Jay ni mtu wa watu, sababu ya kuamua kuzungumza hadharani ni kwa kuwa ana mashabiki wengi, tukaona hatumtendei haki, tunaomba watu waungane nasi zaidi tumuingize kwenye maombi yetu ili apone, lakini suala la pesa nalo ni muhimu pia,” alisema Grace.
 
Sasa kama professor yeye hawezi mwenyewe kugharamikia matibabu sembuse bondia ambaye ata hajawai lipa million 11
 
jay hajaomba msaada......ni mashabiki na wadau wamehitaji wenyewe kuchangia chochote kwenye matibabu yake.....ni baada ya kuskia jamaa anapurusha karibia tsh 4m per day kwa kujitibia.....
Ok yes hajaomba msaada straight ila ndugu wameongea kiutaalam zaidi kwamba hatuombi ila mwenye nacho anaweza kutuma.
 
Back
Top Bottom