Mwili wa Mwanaume waokotwa mitaa ya Jangwani, inadaiwa alishambuliwa, kuuawa kisha kutupa

Ajaliwe pumziko jema.
Maisha tumedhaminiwa tu na mwenyezi Mungu, tuyathamini sana maisha maana kuishi ni mara moja tu.
 
Ukikosa gari baada ya saa 4 usiku usipite pale bora ulale barazani Kariakoo
Hivi mantiki ya kuua mtu ili uibe ipo wapi?

Mimi nakumbuka 2013 wakati natoka Club saa nane usiku mitaa ya Sinza, kuna majamaa yaliniotea, yalikuwa kama 6 hivi kwenye bajaji, nilistukia roba ya hatari toka kwa nyuma, aisee wale jamaa walijua nimeshakata moto, maana mi nilikuja kushtuka baadae nimetelekezwa barabarani, sina simu wala wallet.., daah.., sio poa aisee
 
Pole sana aisee!
 
Chanzo waulizwe haohao polisi ukweli wanaujua.

Kuna kipindi 2000s Dodoma yalizuka sana mauaji na matukio kama haya ya maiti kutupwa makorongoni!

Baadae za mnyepe ikafahamika kuwa ilikuwa ni michezo ya Damas Mallya(DM Hotel) kipindi cha IGP Mahita, Dom Zelote na DSM Tiba ndani ya mbanyu!

(Huu uliitwa utatu mtakaTIFU, wazee walifanya vurugu nyingi sana hawa. Untouchable kingkongs )
 
Inasikitisha sana usikute jamaa anatokea mikoani familia duni kaja Dar kwa kutafuta maisha bora na kusaidia familia yake.
 
Sasa hivi ni tajiri mkubwa dodoma.
 
Huenda pia hata ni mtu mlevi au mgonjwa alianguka na kupoteza uhai

Mazingira alipoonekana ndiyo tatizo ,sidhani kama alikuwa anatembea vichakani ,pale jangwani hakuna shortcut ya kutoka mkwajuni au muhimbili uje kutokeza jangwani maana ni swamp areas.
 
Kipindi cha zelote dom majambazi na vibaka wale wasumbufu wa mitaa wababe wababe sugu walipotea sana maana ilikua ni mnamalizana kimyakimya tu watu wanashangaa haupo tu kitaa
 
Umezingua,ungepiga picha,Unaweza Kuta ni mtu ambaye ana undugu na mwana jf
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…