Mwitikio wa Serikali na Wengine juu ya Mengi kutaja mafisadi!

Hivi tatizo la mzee Mengi ni nini? Kuwataja akina Rostam, Manji, Jeetu, Subash na Tanil kuwa ni mafisadi wakubwa? Amekosea wapi ktk hili? Namshangaa mwandishi mmoja ambae ni kijana kujiingiza ktk mkumbo huu. Hakuna hoja za kueleweka ulizozitoa ktk makala yako. Nakushauri achana na jambo hili, limekuzidi kimo. Kama bosi wako kakulazimisha kuandika, basi ukatafute hoja za kuandika, kile ulichokisema hakifanani na tunavyokujua. Njaa mbaya sana. Najuuuuuta kuisoma makala yako.
 
Hawa wanaowatetea watuhumiwa wa ufisadi waliotajwa na mzee Mengi wanataka kutuambia kuwa yale aliyoyasema ni uongo? Ni mtanzania gani asiyejua kuwa watu hao wanaiba hela za watanzania? Hivi ni biashara gani wanazifanya hata zikawaingizia hela kiasi hicho? Bahati mbaya, wote hao wana asili inayofanana.
Leo ametokea mtu anatutetea, tunasimama na kumtupia madogo... shame on us! When shall we wake up and stand for our rights?
 
Hivi ktk akili zako timamu unaamini kuwa Mengi ana shida hata akafikia kuiba Benz? Unajua mtu ukiwa muongo kwa nafsi yako, kamwe hutakuwa mkweli kwa mwenzio. Tuwe wakweli kwa nafsi zetu jamani. GT, vipi? Nawe ni miongoni mwao? Siku zenu zinakaribia, ni pale watanzania watakapoamua kuamua.
 
Mengi kusema kweli amekwenda mchomo ,ni kawaida kwa walioshitakiwa hutakiwi tena kuwataja taja ,aidha kama kuwataja wanaweza kuvuka basi mengi atakuwa amepoteza ushaidi au atakuwa amewasaidia kuvuka,inategemea na mawakili na naona serikali imelisitukia hilo ,na ndio pale niliposema hawa mafisadi wanajuana ila wanapokuwa mbele ya macho ya wananchi kila mmoja anamtolea mijicho mwenziwe na kurapu awezavyo isitoshe na kutoa hukumu kabisa ,Mengi ameyafanya hayo ,hivyo ,Wakili anaweza kuwatetea wateja wake kupitia kauli za Mengi si hasha wakashinda kesi na baadae wakamlipa mengi kwa mlango wa nyuma. Tunabaki hapa kucheza pachanga.
 
Mwiba, mzee Mengi hajatoa ushahidi hadharani. Huyo wakili ataanzia wapi? Kama angekuwa ametoa ushahidi, tena hadharani, basi hicho unachowaza kingeleta maana ktk hoja hii, lakini kwa pale alipoishia, bado anabaki ndani ya mstari. Alichokifanya ni kuwaumbua tu.
 
Katika hivi vita vinavyotukabili dhidi ya ufisadi, lazima tuwe tayari kuyapiga vita mafisadi kwa njia zozote zile zilizo ndani ya uwezo wetu. Kama wewe ni mwanasiasa, tumia uwanja wa siasa na hasa mikutano ya hadhara kuwaanika mafisadi kama alivyofanya Dr. Slaa Mwembe Yanga. Kama wewe ni mfanya biashara tumia vyombo vyako vya habari kuwaanika hadharani hawa wahujumu kama alivyofanya Mengi. Kama wewe ni kiongozi wa dini, tumia uwanja wako ndani ya kanisa au msikiti kulaani ufisadi unaoiathiri jamii. Kama wewe ni mwana JF, tumia hii forum kuwakandia wezi bila kuwaonea haya kama tunavyofanya wengi wetu hapa.

Kwa nchi kama Tanzania ambapo uhalifu unaoendeshwa na hawa mapapa unafumbiwa macho na mamlaka husika, ni ruksa kutumia silaha zozote - ziwe za jadi au za kisasa, kuyashambulia hawa manyang'au. Wanaweza wakawa na nguvu kuishinda dola lakini kamwe hawawezi kuwa na nguvu kuwashinda wananchi waliochoka kunyanyaswa. Wanaweza wakawa wameiweka serikali mfukoni, lakini kamwe hawawezi kuziba midomo ya wazalendo watakapoamua kulinda maslahi ya taifa lao. Wanaweza wakakiteka chama tawala kinachounda serikali lakini hawana ubavu wa kupambana na wananchi watakapochoka kuzugwa. Wanaweza kutamba kwa muda lakini lakini tambo zao zitafikia ukingoni siku uvumilivu wa wazalendo utakapofikia kikomo.
Kuna siku mafisadi na vikaragosi vyao
Ndani ya serikali
Ndani ya CCM
Ndani ya bunge
Ndani ya mahakama
Ndani ya vyombo vya dini
Ndani ya vyombo vya habari
Na ndani ya JF
Watapokea adhabu yao wanayostahili
Ya kuchomwa moto kama vibaka.​
 
Kinachonishangaza mimi ni kuona kuwa, waliotuhumiwa kuwa mafisadi ni wafanya biashara, lakini wanaojitokeza kuwatetea ni viongozi waandamizi Serikalini, kwani kuna uhusiano gani kati ya viongozi hao wa Serikali mafisadi? Alichokisema hadharani Mengi ndicho kilichopo ktk vichwa vya watanzania. Kipimo cha haya niyasemayo ni kidogo sana, mchukue Rostam au mwingine yeyote kati wale waliotajwa, mwambie atembee kw miguu mitaa ya Kariakoo kwa muda wa dakika 10, halafu mchukue mzee Mengi, nae afanye hivyo hivyo, matokeo yake kila mmmoja wetu anajua, Mengi atabebwa kwa kushangiliwa na hao mafisadi wataishia mikononi mwa wananchi.
 
Kama ni kweli Sofia Simba na George Mkuchika wametoa kauli hizo kama zilivyoandikwa ktk vyombo vya habari, basi wamejimaliza kisiasa. Wakitaka kujipima kwa kauli hizo, basi wafanye ziara sehemu wanazoishi walalahoi wenzangu, au wakahani msiba ktk maeneo hayo na watu wakawatambua...
 

Katika hili mimi naungana na mtoa hoja kuwa ukimchunguza kuku hautakula nyama yake, ni kweli kila mtu anayo mapungufu ya aina fulani.hatuwezi kusema mengi ni msafi tutakuwa tunajidanganya.Lakini pamoja na kutokuwa msafi anapozungumzia swala ambalo viongozi wetu waliopewa dhamana ya kulikemea wanaliogopa yeye akajitoa mhanga hatuna budi kumshukuru,Mbona wahusika wakuu wamekaa kimya? nikosa kuwadharau watanzania kwa vigezo vya kuwafikiria kuwa hawajui mambo. Hawa watu tunaodhania hawajui wanajua mambo mengine hata Rais wanchi hayajui.kwa hiyo Manyerere mchango wako ni mzuri utufanye tupanue ulingo wa kufikiri na zaidi tusimame na watu wanaotetea masilahi ya wananchi. kuwa na vyombo vya habari si issue hata rostam anavyo tena anaweza kuwa anavitumia kwa siri jambo ambalo ni unafiki atoke wazi ajitete kukaa kimya kunaashilia mambo, Tusingefurahia viongozi wetu ambao tunawalipa kwa pesa zetu ndo wawe mstari wa mbele kushambulia wananchi kwani wao pia hawawezi kuacha serikali ichukue mkondo?Nazidi kusema siwezi kushangaa kwa sofia kuchemsha anapomsema Mengi kwa wale msiomjua fyatilieni mtamjua ni mama wa jinsi gani?.Mengine hatuyasemi hapa jamvini kwani ni mambo ya mtu binafsi,kama ambavyo Mengi si msafi ndo Sofia asivyo msafi pia pamoja na wengine wengi.
 
Naye Lipumba wa CUF kaingilia sakata hili -- na kama ilivyokuwa kwa mitambo ya Dowans -- amejikita upande wa mafisadi. Katika sakata la Dowans alijikuta alikamata pabaya kwani Hatimaye serikali imekacha kununua Dowans.

Huyu kiongozi wa CUf nilikuwa namheshimu sana lakini naona tayari ameharibiwa na RA kupitia kwa Jussa ambaye ni swahiba wa RA. Inasikitisha kuona Profesa hataki kukubali kwamba chama chake - CUF - kilitoka kapa huku bara (hata kiti kimoja cha ubunge hakikupata -- wala kiti cha udiwani ktk mkoa wa Dar) kutokana na mapesa waliyotumia CCM kutoka ufisadi wa EPA, radar, NSSF, ndege ya urais etc.
 

Kipima pembe je Fisi akiwa hakimu mbuzi ana sheria?
 



Lipumba si mzee wa kuganga njaa!! Hana issue siku hizi.
 
NILIKUWA DODOMA WAKATI WA UCHAGUZI WA UWT NA SOPHIA SIMBA ALIKUWA AKIGAWA KATI YA Sh 150,000 na 200,000 KWA WAJUMBE, JE, HUYO ANAWEZA KUPIGA VITA RUSHWAA? UNADHANI ATAWATENGA WALIOMPA FEDHA ZA KUGAWA?

Sofia aliwagawia akina mama wenzie kiasi cha fedha kadha je inapokuwa wakati wa kuhonga akina baba nadhani huwapa mamilioni.....!!!!, lakini mnamjua Sofia tangu alipoanza kusoma cheti cha sheria hata kwenda mlimani kuchuakua sheria. Watanzania tunajua mengi lakini itafika wakati babu atataka kusema.
 
Najaribu kujiuliza, hivi ile fensi aliyotaka kujenga Mengi kwa marehemu baba wa Taifa bado ipo vile vile au imejengwa? Vile vibanda vya askari pale mlangoni vimekarabatiwa au bado vimebaki vile vile? Hivi suala la kukopa Bank ambalo ni mkataba kati ya Bank na mkopaji ni kosa la jinai? Hapa ndipo ninapokuwa na mashaka na Bwn. Manyerere. Kama sikosei, Fensi imejengwa na vibanda vimefanyiwa ukarabati. Nadhani Mengi alitaka kupaboresha nyumbani kwa baba wa Taifa. Hebu tutafute ufisadi wa mzee huyu Mengi, suala la kukopa Bank ni la kimkataba, kama Bank hawaridhiki na mteja wao, wana haki ya kuchukua hatua za kisheria. Hivi Manyerere hajawahi kusikia habari za EPA, RICHMOND, RADAR, BoT, TICS, DOWANS na kadharika? Hivi ni kipi kati hivi viaua uchumi wa nchi? Bank kukopwa na Mengi au kashfa za EPA, RICHMOND, RADAR, BoT, TICS, DOWANS? Je, ni wapi alijaribu kuwafahamisha watanzania madhara yake?
 
Kahinda, kama kungefanyika uchunguzi kt uchaguzi ule wa UWT, basi watu wengi sana wangeumbuka. Sitaki kusema mengi mengi, lakini kwa kifupi, Sofia na baadhi ya viongozi waandamizi ktk Serikali hii wamemtia aibu kubwa sana JK na chama chake. Tumshukuru Mungu kwa ushujaa, ukomavu wa kisiasa, upendo kwa nchi yake na uvumilivu wa hali juu aliouonesha mgombea aliyeporwa kura zake na kumpa ushindi wa matata saana Bi. Sofia. Kama angethubutu kusema kuwa hakubali matokeo yale, basi Dodoma na ndani ya chama pasingetosha.
 
Hata kama Mengi angekuwa ni ufisadi wa aina yake kama huyu Manyerere anavyodai bado TWO WRONGS DOES NOT MAKE A RIGHT. Twambie Bw Manyerere na wenzake wote wanaojaribu kufunika hao waliotajwa na Mengi na kuwa spokesperson wao je NI KWELI WATU HAWA NI MAFISADI PAPA AU NI WATU SAFI? Mbona issue yenyewe inayozungumzwa ni mafisadi wanaotafuna nchi yetu. Je watu hawa waliotajwa ni safiii? Kama Mengi naye ni fisadi basi wanaomjua wamtaje, na sio kutueleza kuwa alikopa fedha NBC akashindwa kulipa akaweka mawakili ili wamtetea asichukuliwe hatua. Sasa huo ni ufisadi? Hayo ni yale yaliyotajwa kuwa ni ufisadi wa Mbowe kukopa na kutolipa kwa wakati kisha kuweka mawakili. Labda watwambie huo ni uzembe wa kibiashara au ni mipango mibaya au hawakuwa makini walipobuni miradi yao lakini huwezi kutwambia huo ni ufisadi. Je ROSTAM na hao wenzake NI SAFI? Nakumbuka story moja nyani walipomlalamika binadamu kuwa anawaonea kwa kuwakamata kwa mitego na kuwapiga na kuwaua. Jibu la mwanadamu lilikuwa rahisi sina ugomvi na nyani ila napambana na wezi wa mahindi yangu. Bahati mbaya kila ninapoweka mtego wa kunasa wezi wa mahindi yangu nakuta walionaswa ni nyani. Sasa hata kama si wabaguzi ila kama kila mara issue za ufisadi papa zikitokea tunakuta ni kina Patel sasa tusemeje. Hawa wanacorrupt system nzima. Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania, Ahsanteni ndugu wana JF
 
Hata kama Mengi angekuwa ni ufisadi wa aina yake kama huyu Manyerere anavyodai bado TWO WRONGS DOES NOT MAKE A RIGHT. Twambie Bw Manyerere na wenzake wote wanaojaribu kufunika hao waliotajwa na Mengi na kuwa spokesperson wao je NI KWELI WATU HAWA NI MAFISADI PAPA AU NI WATU SAFI? Mbona issue yenyewe inayozungumzwa ni mafisadi wanaotafuna nchi yetu. Je watu hawa waliotajwa ni safiii? Kama Mengi naye ni fisadi basi wanaomjua wamtaje, na sio kutueleza kuwa alikopa fedha NBC akashindwa kulipa akaweka mawakili ili wamtetea asichukuliwe hatua. Sasa huo ni ufisadi? Hayo ni yale yaliyotajwa kuwa ni ufisadi wa Mbowe kukopa na kutolipa kwa wakati kisha kuweka mawakili. Labda watwambie huo ni uzembe wa kibiashara au ni mipango mibaya au hawakuwa makini walipobuni miradi yao lakini huwezi kutwambia huo ni ufisadi. Je ROSTAM na hao wenzake NI SAFI? Nakumbuka story moja nyani walipomlalamika binadamu kuwa anawaonea kwa kuwakamata kwa mitego na kuwapiga na kuwaua. Jibu la mwanadamu lilikuwa rahisi sina ugomvi na nyani ila napambana na wezi wa mahindi yangu. Bahati mbaya kila ninapoweka mtego wa kunasa wezi wa mahindi yangu nakuta walionaswa ni nyani. Sasa hata kama si wabaguzi ila kama kila mara issue za ufisadi papa zikitokea tunakuta ni kina Patel sasa tusemeje. Hawa wanacorrupt system nzima. Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania, Ahsanteni ndugu wana JF
 
1.
Kweli, Mengi hakuonekana tena kwa Mwalimu, labda wakati wa msiba. Tangu siku hiyo, nikawa nataka kujua sababu za mtu huyu kuchukiwa na Mwalimu.


- Hii habari sio ya kweli,nimeshuhudia Mwalimu akisafiri na Mengi katika ndege yake ya serikali mara chungunzima, na besides wakati huo Mengi bado alikuwa ni Mwenyekiti wa lile shirika la Accounts la taifa alikuwa na access na Mwalimu, all the times. Mara kwa mara Mengi alikua na tabia ya kuomba ride kwenye ile ndege ya Mwalimu, hakuna hata siku moja Mwalimu, alimfukuza ndani ya ile ndege, infact alikuwa akimuona tu anamuita hata kama yuko nyuma aje karibu na ataongea naye mpaka mwisho wa safari, kwa hiyo hili la fensi sio kweli kwa sababu kisheria linaangukia kwenye bajeti ya Ikulu, ambayo Mwalimu hakuwa na say nalo na kama kweli fensi ilikuwa imechoka ni uamuzi wa usalama wa taifa kuitengeneza sio Mengi.

- Ni kichekesho kikubwa sana kwamba Mengi, anaweza kuingilia kazi ya usalama wa taifa kwa kuwakumbusha kwamba fensi ya Mwalimu haifai na hata bosi wa usalama kwenda kwa Mwalimu na kumfikishia ujumbe wa Mengi, that is hillarious! Enzi hizi aliyekua anaongoza usalama wa rais alikua Mwangota, hivi huyu mwandishi anamfahamu au alishawahi kumsikia? Maana huyu alikuwa na tabia ya kuwalamba vibao viongozi magoi goi, sasa kama kuna usalama wa kumfikishia ujumbe wa Mengi Mwalimu then, basi alikuwa ni huyu Mnyaki, kwanza angeanza kumla vibao Mengi mwenyewe, kwa kumuingilia kazi yake, hai-make make a sense at all!



2.
Mwalimu alikuwa “kiona mbali”. Pengine alijua kwamba akiruhusu Mengi amjengee hiyo fensi, baadaye yangekuwa matangazo kuanzia kwenye televisheni, redio hadi magazeti anayoanzisha kama uyoga.


- Mwalimu alikuwa kiona mbali sana ndio maana aliona mbali sana kwa kutupatia Mr. Clean bin Kiwira, what a kiona mbali!

3.

- Another joke, hivi Mengi alichukua hela NBC au alikopa kama wananchi wengine wanavyoruhusiwa kukopa na kurudisha? Yes it is a fact kwamba Mengi alikopa hela toka bank na kuzifanyia biashara, huku akitoa ajira kwa wananchi ambao hata serikali ya Mwalimu ilikuwa imeshindwa kuwapa ajira, is that a crime?

- Kukwepa kulipa inakubaliwa kwa sababu za kisheria, sio blah! blah! hivi huyu muandishi hajasikia kuwa benki za US zimeshindwa kulipa madeni na zimelipiwa na serikali, sasa hapa cha ajabu ni kipi? Kama biashara haizalishi mkopaji ana haki kisheria kuifahamisha benki aliyokopa kwamba wampe break mpaka atakapokaa sawa, mbona Donald Trump anafanyiwa kila wakati, I mean kama ni kumchafua Mengi basi watafute angalau convincing facts, badala ya hizi pwagu na pwaguzi ambazo sio siri ni pathetic!

FMES
 
Can I make up a story about Nyerere na maoni yake juu ya Rostam? where by I'm the only witness!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…