Hivi tatizo la mzee Mengi ni nini? Kuwataja akina Rostam, Manji, Jeetu, Subash na Tanil kuwa ni mafisadi wakubwa? Amekosea wapi ktk hili? Namshangaa mwandishi mmoja ambae ni kijana kujiingiza ktk mkumbo huu. Hakuna hoja za kueleweka ulizozitoa ktk makala yako. Nakushauri achana na jambo hili, limekuzidi kimo. Kama bosi wako kakulazimisha kuandika, basi ukatafute hoja za kuandika, kile ulichokisema hakifanani na tunavyokujua. Njaa mbaya sana. Najuuuuuta kuisoma makala yako.