Mwongozo wa ufugaji wa kisasa wa Mbuzi wa nyama na maziwa

Mwongozo wa ufugaji wa kisasa wa Mbuzi wa nyama na maziwa

Nimezungumza hayo kutokana na niliyoyaona kwa wengi wanaofuga mifugo mingi nimeona moshi nimeona Tanga, unapokuwa na mbuzi hamsini wahuni wanaofanya ujangili wanaweza kuwauza mbuzi wako wakiwa zizini kwako yaani wanajua tu una mbuzi 100 maana yake 100 * 50000 ni milioni tano, wenyewe wanataka mil 2 za bia na umalaya hivyo wanachukua tu gobore lao au bastola yao na gari kubwa kuja kuzoa na wewe ili usiwasumbue wanakumiminia tu fasta, nimeona wengi wakifa. lazima uput into consderation haya mambo. kama watu wanavunja nyumba ili waibe simu ya tochi wapate pesa ya unga itakuwa vipi kwa hela lililojaa mbuzi na kondoo ambao soko lake lnatisha hasa kwa maeneo ya mjini.

Sasa mleta mada unataka akufundishe mpaka namna ya kulinda mifugo yako?
 
Kwa mara nyingine tena, leo nimeona haja ya kuanzisha mada nyingine na tujadiliane kwa pamoja juu ya ufugaji wa mbuzi baada ya kujadili kwa muda mrefu ile mada ya ufugaji wa kuku.

Ufugaji wa mbuzi hapa Tanzania ni fursa adhimu ambayo Watanzania wengi hawajaiona. Ni ufugaji ambao wenyewe kama mfugaji atazingatia kanuni na misingi ya ufugaji Bora, ni rahisi sana mfugaji kujiondoa kutoka kwenye umasikini na kuwa tajiri. Kitu cha msingi na muhimu ni kwamba,mfugaji lazima awe na eneo pamoja na mtaji wa kuanzia.

Mbuzi wanatakiwa kufugwa shambani. Shamba ambalo mbuzi wanatakiwa wafugwe linapaswa liwe na sehemu ambayo mbuzi wanaweza kwenda kuchungwa na pia kuwe na chanzo cha maji. Mbuzi kitabia hupenda kulala juu hivyo mabanda yao yanapojengwa lazima yainuliwe juu. Mabanda ya mbuzi si ghari,kwani hujengwa simple.

Mbuzi kwa mwaka wao huzaa mara mbili na ukipata ile mbegu ya wanaozaa mapacha faida yake huwa ni kubwa zaidi, itategemea na mtaji wa mfugaji, lakini kama mfugaji ataweza kuanza na mradi wa mbuzi 50 inakuwa vizuri zaidi. Ukiwanunua mbuzi 50@ tsh.50,000/= utapata Milioni 2 na nusu, madume 2 kila moja likanunuliwa kwa tsh 75000/= kwa madume mawili itagharimu tsh laki moja na nusu. Usafirishaji wa mbuzi hauzidi laki tatu na nusu. Kwa hiyo itajikuta ukiwa na milion 5 utaweza kuanza na mradi wa ufugaji wa mbuzi majike 50 na madume mawili,pamoja na kuwajengea sehemu ya ya kulala.

Kama nilivyoainisha hapo awali, mbuzi kwa mwaka wao huzaa mara 2, hivyo kama kila mbuzi atazaa hebu chukulia kila mbuzi atazaa mbuzi mmoja tu, ingawa kuna wengine watazaa mapacha hasa ukipata ile mbegu ya mbuzi wanaozaa mapacha, mwishoni mwa mwaka utakuwa na idadi ya mbuzi 100 wapya waliozaliwa na ukujumlisha na mtaji ule wa mbuzi 50 utakuwa na jumla ya mbuzi 150, hii ni ndani ya mwaka mmoja, pata picha utakuwa na mbuzi Idadi gani baada ya miaka 3 hasa ukizingatia kuwa wale watoto wa mbuzi watakapofikia miezi 8 utaanza kuwapandisha nao watazaa nk. Ili kufikia malengo, inashauriwa kuwa mbuzi wa mtaji wanaonunuliwa lazima wawe na umri mmoja ili kusudi waweze kupata mimba kwa wakati mmoja na waweze kuzaa kwa wakati mmoja pia.

Magonjwa ya mbuzi mengi yanafahamika na ni rahisi kudhibitika,hivyo mbuzi si rahisi kufa hovyo.

Toka mbuzi anapata mimba mpaka anazaa,hutumia muda wa wiki miezi mitano yaani siku 150.

Kwa sababu hili pia ni eneo langu nilililolisomea, nawaruhusu kwa wale wote wenye Interest na uanzishaji wa Mradi huu wa ufugaji wa mbuzi kuuliza swali lolote lihusulo ufugaji bora wa mbuzi nami nitajibu.Lengo likiwa ni lile lile la kusaidiana kama Watanzania ili kuondokana na hili lindi la umasikini.

Karibu kwa majadala.

Kwa mbuzi 50 unatakiwa uwe na eneo la ukubwa gani la kuwalishia?
 
Hawa mbuzi ni mbuzi bora walioboreshwa, wanapatikana dodoma. Ni matokeo ya cross breed iliyofanyika kati ya mbuzi wa kienyeji wa dodoma na exotic breed.Hivyo wengi wa uzao wao huzaa mapacha. Mbuzi hawa huuzwa tsh elfu 50, wakiwa na umri wa miezi 5.

Mkuu unaweza kuelekeza Vzr ni DODOMA sehemu gani wanapatikana hao Mbuzi? ikibidi mawasiliano yao! Nadhani utakuwa umesaidia wengi wanaopita humu JUKWAANI cmbaya pia naww ukiweka mawacliano yako km hutajali
 
Kama una mtu uganda wanaoatukans kwa wingi tu ni hela yako tu
 
Kuwa na mabanda ya mbuzi yaliyo inuliwa hakuchangiwi na magonjwa hatari yanayo_wasumbua?
 
Kwa mara nyingine tena, leo nimeona haja ya kuanzisha mada nyingine na tujadiliane kwa pamoja juu ya ufugaji wa mbuzi baada ya kujadili kwa muda mrefu ile mada ya ufugaji wa kuku.

Ufugaji wa mbuzi hapa Tanzania ni fursa adhimu ambayo Watanzania wengi hawajaiona. Ni ufugaji ambao wenyewe kama mfugaji atazingatia kanuni na misingi ya ufugaji Bora, ni rahisi sana mfugaji kujiondoa kutoka kwenye umasikini na kuwa tajiri. Kitu cha msingi na muhimu ni kwamba,mfugaji lazima awe na eneo pamoja na mtaji wa kuanzia.

Mbuzi wanatakiwa kufugwa shambani. Shamba ambalo mbuzi wanatakiwa wafugwe linapaswa liwe na sehemu ambayo mbuzi wanaweza kwenda kuchungwa na pia kuwe na chanzo cha maji. Mbuzi kitabia hupenda kulala juu hivyo mabanda yao yanapojengwa lazima yainuliwe juu. Mabanda ya mbuzi si ghari,kwani hujengwa simple.

Mbuzi kwa mwaka wao huzaa mara mbili na ukipata ile mbegu ya wanaozaa mapacha faida yake huwa ni kubwa zaidi, itategemea na mtaji wa mfugaji, lakini kama mfugaji ataweza kuanza na mradi wa mbuzi 50 inakuwa vizuri zaidi. Ukiwanunua mbuzi 50@ tsh.50,000/= utapata Milioni 2 na nusu, madume 2 kila moja likanunuliwa kwa tsh 75000/= kwa madume mawili itagharimu tsh laki moja na nusu. Usafirishaji wa mbuzi hauzidi laki tatu na nusu. Kwa hiyo itajikuta ukiwa na milion 5 utaweza kuanza na mradi wa ufugaji wa mbuzi majike 50 na madume mawili,pamoja na kuwajengea sehemu ya ya kulala.

Kama nilivyoainisha hapo awali, mbuzi kwa mwaka wao huzaa mara 2, hivyo kama kila mbuzi atazaa hebu chukulia kila mbuzi atazaa mbuzi mmoja tu, ingawa kuna wengine watazaa mapacha hasa ukipata ile mbegu ya mbuzi wanaozaa mapacha, mwishoni mwa mwaka utakuwa na idadi ya mbuzi 100 wapya waliozaliwa na ukujumlisha na mtaji ule wa mbuzi 50 utakuwa na jumla ya mbuzi 150, hii ni ndani ya mwaka mmoja, pata picha utakuwa na mbuzi Idadi gani baada ya miaka 3 hasa ukizingatia kuwa wale watoto wa mbuzi watakapofikia miezi 8 utaanza kuwapandisha nao watazaa nk. Ili kufikia malengo, inashauriwa kuwa mbuzi wa mtaji wanaonunuliwa lazima wawe na umri mmoja ili kusudi waweze kupata mimba kwa wakati mmoja na waweze kuzaa kwa wakati mmoja pia.

Magonjwa ya mbuzi mengi yanafahamika na ni rahisi kudhibitika,hivyo mbuzi si rahisi kufa hovyo.

Toka mbuzi anapata mimba mpaka anazaa,hutumia muda wa wiki miezi mitano yaani siku 150.

Kwa sababu hili pia ni eneo langu nilililolisomea, nawaruhusu kwa wale wote wenye Interest na uanzishaji wa Mradi huu wa ufugaji wa mbuzi kuuliza swali lolote lihusulo ufugaji bora wa mbuzi nami nitajibu.Lengo likiwa ni lile lile la kusaidiana kama Watanzania ili kuondokana na hili lindi la umasikini.

Karibu kwa majadala.

Mkuu kweli wewe ni hazina kwangu. Nipo kwenye mandalizi ya mipango ya ufugaji wa kuku na hao mbuzi. Nikiwa tayari nitakusumbua sana mkuu. ingawa kwenye kuku nimeanza mdogomgogo.
 
Mkuu kweli wewe ni hazina kwangu. Nipo kwenye mandalizi ya mipango ya ufugaji wa kuku na hao mbuzi. Nikiwa tayari nitakusumbua sana mkuu. ingawa kwenye kuku nimeanza mdogomgogo.
Ndandidzi,
Usijari mkuu, tuko pamoja chochote utakachokwama au kuhitaji kufahamu kuhusu ufugaji wa kuku na mbuzi nijulishe nitakusaidia.
 
Kuwa na mabanda ya mbuzi yaliyo inuliwa hakuchangiwi na magonjwa hatari yanayo_wasumbua?
Pamoja na kuzuia kuenea kirahisi magonjwa, Ki tabia mbuzi huhitaji kulala kwenye mabanda yaliyoinuliwa juu,hawapendi kulala chini kama ilivyo kwa ng'ombe.Vilevile mbuzi hawapendi mvua,ukiona mvua inakaribia kunyesha ni muhimu mbuzi wakarudishwa haraka bandani kwao.
 
Ni kweli kwamba ukiwa na beberu mwenye asili ya uzao wa mapacha basi hata majike atakaowapanda watazaa mapacha hta kama hawana asili ya kuzaa mapacha?
 
Mkuu mimi nipo kwenye hatua za mwisho ktk maandalizi ya ufugaji. Nimeplan nianze na kuku baadae nguruwe na hata hao mbuzi make ni rahisi sana kuwafuga.

Shida yangu mimi ni kujua ni umbali gani natakiwa kutenganisha mabanda yao hawa mifugo ili kusiwe na muingiliano wa magonjwa iwapo nitawafuga wote katika eneo moja hasa nikiwa na maana ya kuhimili ulinzi na monitoring ya maendeleo yao?
 
Zanstan asante sana kwa kujitoa. Mungu akubariki. Naulizia gharama ya kusafirisha hao mbuzi hamsini ni kutoka Dodoma kwenda wapi? Dar itakuwa kiasi gani? Asante sana
 
Zanstan asante sana kwa kujitoa. Mungu akubariki. Naulizia gharama ya kusafirisha hao mbuzi hamsini ni kutoka Dodoma kwenda wapi? Dar itakuwa kiasi gani? Asante sana

Mama Joe Karibu sana mjasiria Mali, hiyo bei ni kutoka dodoma hadi Dsm
 
Vipi kuhusu kondoo? Je kuna tofauti yoyote kati ufugaji wa Mbuzi na Kondoo? Je, ufugaji wa Kondoo hauna tija kibiashara kama ule wa Mbuzi?

Asante!
 
Vipi kuhusu kondoo? Je kuna tofauti yoyote kati ufugaji wa Mbuzi na Kondoo? Je, ufugaji wa Kondoo hauna tija kibiashara kama ule wa Mbuzi?

Asante!
MahinaVeterani,

Ufugaji wa Kondoo hauna tofauti na ufugaji wa mbuzi na ndio maana jamii nyingi huchanganya pamoja wanyama hawa wakati wa kufugwa kwao. Kondoo na Mbuzi hushabiana kwa mambo mengi sana lakini lililokubwa ni kuwa wote mimba zao huchukua miezi 5 toka kushika mpaka kuzaa.Pia magonjwa anayopata Kondoo ndiyo hayo hayo anayopata Mbuzi.

Kuhusu masoka ni tabu kidogo ukilinganisha na nyama ya mbuzi,kama unavyojua jamii yetu si watu wengi sana wanaopendelea kula nyama ya Kondoo ukilinganisha na nyama ya mbuzi. Mara nyingi masoko ya Kondoo hupatikana kwenye Mahoteli makubwa.
 
Zantsan nashukuru kwa bandiko hili

Nikiangalia mbuzi zaidi ya 200 naona uhitaji wa shamba kubwa sana ambalo si rahisi kupata dar.
Pengine hapo ndio penye gharama kubwa.

Ninakusudia kuanzisha mradi wa kufuga mbuzi tatizo langu ni eneo....
Pia nasikia ukifuga mbuzi maeneo jirani na Dar kuna wezi huwa wanaweza kuvamia na kukomba mbuzi wa kutosha maana kuna soko.

Mashamba yanapatikana mikoani shida inakuja kwamba bei ya mbuzi mikoani iko chini.....ukitaka kuwauza Dar inabidi kuweka gharama ya usafiri.

Kimsingi ninatatizwa sana ingawa mtaji wa kuanzia tayari ninao

Sijui kama una uzoefu wowote kuhusu hofu zangu!!
 
Last edited by a moderator:
Zantsan nashukuru kwa bandiko hili

Nikiangalia mbuzi zaidi ya 200 naona uhitaji wa shamba kubwa sana ambalo si rahisi kupata dar.
Pengine hapo ndio penye gharama kubwa.

Ninakusudia kuanzisha mradi wa kufuga mbuzi tatizo langu ni eneo....
Pia nasikia ukifuga mbuzi maeneo jirani na Dar kuna wezi huwa wanaweza kuvamia na kukomba mbuzi wa kutosha maana kuna soko.

Mashamba yanapatikana mikoani shida inakuja kwamba bei ya mbuzi mikoani iko chini.....ukitaka kuwauza Dar inabidi kuweka gharama ya usafiri.

Kimsingi ninatatizwa sana ingawa mtaji wa kuanzia tayari ninao

Sijui kama una uzoefu wowote kuhusu hofu zangu!!

RealMan,

Kuhusu wezi ni tatizo ambalo linaweza kudhibitika. Namna gani utadhibiti wezi ni kuwa lazima uajiri mlinzi ambaye atakuwa anakulindia wakati wa usiku, kama unavyojua huu ni mradi na unahusisha pesa nyingi za uwekezaji hivyo ni muhimu wakati unapanga bajeti ya huo mradi wako ukajumuisha gharama za mlinzi.

Kuhusu kufugia mikoani hakuna shida yeyote kwani wakati wa kuuza utakodi canter na utawapakia mbuzi wako tayari kuwapeleka sokoni Dar au kwenye miji mikubwa. Gharama za usafiri ni ndogo sana kwa kila mbuzi na mara nyingi huwa haizidi tshs. 5000/=

Kama utaona kufugia mikoani kutaongeza gharaza za usafiri au labda siyo mzoefu kwenye usafirisha wa wanyama na kwenda kuwauza Dar unaweza ukatafuta shamba Mkuranga au Babagamoyo ambako wafugaji wengi nimewasaidia kuwaanzishia miradi yao ya mbuzi na Kuku huko na kwamba hali ya usalama ni kubwa tu ukilinganisha na maeneo yaliyo jirani zaidi na Dar.
 
Hawa mbuzi ni mbuzi bora walioboreshwa, wanapatikana dodoma. Ni matokeo ya cross breed iliyofanyika kati ya mbuzi wa kienyeji wa dodoma na exotic breed.Hivyo wengi wa uzao wao huzaa mapacha. Mbuzi hawa huuzwa tsh elfu 50, wakiwa na umri wa miezi 5.

Huko Dodoma wamejaa tele kila kona ama unawafuata wapi?

Contacts?
 
Back
Top Bottom