My personal Top 10 list ya movie za kusikitisha nilizobahatika kuona

My personal Top 10 list ya movie za kusikitisha nilizobahatika kuona

1. Where hands touch .
2. The pursuit of happyness
3. Tears of the sun
4. Kuna movie ya naijeria sijui ghana nimeangalia nikiwa mdogo mdogo, siikumbuki jina; Mama mmoja amefariki ameacha mtoto wa kike na wa kiume wadogo, Baba akaoa mke mwingine, akawa anawatesa wale watoto, mwisho wakafukuzwa kwao, sijui walitoroka wakawa wanatangatanga mtaani. Nilikuwa nalia, nikajifunza kumuombea mama yangu aishi miaka mirefu 😀 now she’s 60 of age.
Haha hiyo where hands touch inahusu nini??
 
Wakuu kwema

Mbele yenu nina list ya drama ambazo zilinisikitisha me personally baada ya kuziangalia, ziko nyingi but nimezi-compress hadi nimetoka na kumi tuu, ambazo naamini ukienda kuziangalia hutotoka empty handed.

Honourable mentions;
All Quiet on the Western Front
The Boy in the stripped pajamas
Grave of Fireflies
The Pianist
Hatchi: A dog's tale
Life is beautiful

Tuanze;
10. 12 Years a Slave
True story kuhusu black American aliekuwa ni mtu huru kabisa, but akaingizwa kweny utumwa(slavery) kimakosa, na kupitia miaka 12 ya mateso bila kuonana na mke na watoto.


9. The Green Mile
Inahusu injustice and sufferings alizopitia main character ambaye alihukumiwa kifo kwa kosa la mauaji ya watoto wawili wakike.

Hii movie inathibisha 100% ule msemo wa "Don't judge a book by its cover"


8. Requiem for a dream
Inahusu addiction and obsession, ninachoipendea hii movie haija-base tuu na madawa ya kulevya, kweny hii movie utaona obsessions mbalimbali pamoja na obsession za wanawake za kupungua uzito, obsession za kuonekana kwenye TV na jinsi hizo obsession zilizokuja kuharibu maisha ya hawa characters kiakili, kiafya na kiuchumi.

The ending ya hii movie ilisikitisha sana jinsi maisha ya hawa characters yalivobadilika kutoka kuwa watu wa kawaida wenyew afya njema wanaojielewa, hadi kuwa katika situation mbaya sana.


7. Good Will Hunting
Will Hunting ni kijana mwenye uwezo mkubwa wa akili lakini anasumbuliwa na changamoto nyingi za maisha zitakazo mpelekea kukutana na Dr Sean (psychiatrist) ambaye atakae kuja kuwa mtu wa muhimu zaidi kukutana nae maishani mwake.

Nilichoipendea hii movie ni kwamba it's unpretentiously philosophical, haina mafunzo ya ku-force, ipo very realistic kuhusu maisha na ipo simple, na waandaaji wa hii movie hawajaweka misemo ya kifikra au yaki-falsafa ya kuwaumiza watu vichwa bali wamebase kweny changamoto za maisha ya kila siku.


6. Beautiful Boy
Story kuhusu baba na mtoto wake wa kiume anayesumbuliwa na addiction.
Waandaaji wa hii movie wanajua addiction ni nini, nimeangalia movie nyingi zinahusu addiction but this has the best depiction of addiction.

The struggles ambazo huyu baba na mwanae wanapitia zinasikitisha sana, kwenye hii movie niligundua jinsi gani addiction ilivokuwa ngumu kuacha, najua utakuwa una idea ya ugumu wake kama ulishawahi kukaa na mtu mwenye addiction, ila kama hujawahi usimcheke mtu mwenyew addiction ukasema anajiendekeza. Kinachosikitisha zaidi is the fact that huyu main character wa hii movie sio kwamba anapenda anachofanya, sio kwamba aanapenda kuharibu maisha yake.


5. Atonement
Hii ni love story, kwenye love stories zote nilizoangalia nimeamua kuichagua hii Atonement iwepo kwenye list yangu, kwann?? Well ni story ambayo inahusu "the love that was never meant to be".
Mtoto mdogo wakike alishuhudia dada yake mkubwa akifanya mapenzi na mfanya kazi wao, kwa wivu aliokuwa nao dhidi ya dada ake akamsingizia jamaa kwa kumbaka binamu yao, Jambo ambalo lili-affect maisha ya mshkaji aliyekuwa hana mbele wala nyuma.


4. The Hunt
Story kuhusu mwalimu wa kindergarten ambaye anapenda sana kazi yake na watoto, lakini hayo yote ni bure aliposingiziwa kumshika kinyume na maadili mmoja wa wanafunzi wake (mtoto mdogo wa kike). Aisee wanasemaga "bad news spreads faster than good news" inasikitisha sana kuona jinsi maisha ya jamaa yaliyobadilika ghafla, kutoka kuwa mwalimu anayependwa na jamii kwa kujitoa kwake kwa kuwajali watoto hapo shuleni, hadi kupoteza kazi na kuwa mtu wa kuchukiwa na jamii nzima na kutengwa na familia, hata akiingia kweny mall wanamfukuza kwa kumpiga na kumdhihaki.

Tangia niangalie hii movie niliacha kabisa haya mambo ya kuwachangamkia watoto wa kike, hata kama ni wa dada angu nahakikisha kama nipo nae bac na ndugu wengine wapo(kiufupi nilianza kuogopa watoto). Najua ni ngumu, lakini kwenye hii movie utamchukia huyu mtoto.


3. Manchester by the Sea
This is the best depiction of "Grief, Loss, Suffering and Pain"
Story hii inamuhusu character anayesumbuliwa na depression ya tukio la ajali lililotokea miaka ya nyuma kidogo, lililosababisha vifo vya wanae wote watatu, sitaongelea kuhusu hilo tukio nisije kutoa spoilers, but if you're interested go watch it. Inahusu jambo ambalo lingenitokea mimi personally, sidhani kama ningeweza kuishi nalo.


2. Schindler's List
Hii inastahili kuwa namba moja but nimeiweka namba mbili kwa sababu zangu binafsi.
True story inayomhusu Oscar Schindler, mfanyabiashara wa kijerumani aliyeanza kuwaonea huruma wayahudi waliokuwa ujerumani kupindi cha WWII, na kuanza kuwasaidia kutoroka ujerumani kwa njia ya kuwaajiri na kuwasafirisha, alianza kuwaonea huruma baada ya kushughudia mauaji ya wayahudi live kitu ambacho kili-ignite huruma ndani ya moyo wake.

Aisee mambo yaliyokuwa yakiendelea kweny zile concentration camps ni mambo ya kinyama sana, kuona jinsi watoto wa kiyahudi walivokuwa wanahangaika kujificha hadi wengine wakienda kujificha kweny mashimo ya choo sehemu za kuhifadhia vinyesi.

Nimeangalia movie nyingi zinazohusu holocaust but this one is the best.


1. The Elephant Man
True story of man aliyeishi uingereza between 1862-1890.

After watching this movie i was speechless.

Kweli dunia ni uwanja wa mateso.


Weka na zako ambazo hazipo kweny hii list.
The goat life. Nzuri saa masaa 3 kasoro ambao hawapendi zile ndefu hawataweza hii
 
Sijaona uiweke the million dollar baby..seven Pounds.. A Walker to remember,Me before you..a dead poet society...The Miracle walker...
Hizo zote top tier movies, haswa hio million dollar baby, what a tragic ending.
 
Hizo zote top tier movies, haswa hio million dollar baby, what a tragic ending.
Kuna kipindi nilitafuta movies za watu wanaosumbuliwa na magonjwa, nikapata kama 100,kwa siku nilikua nacheki mbili..nina list ndefu sana ya movie za kujiliza..

Sure mwisho unahuzunisha..umeicheki 5 feet apart??story ya watu wanapendana but hawaruhusiwi kusogeleana zaidi ya hatua tano..so maisha yao yanakua hivyo hivyo...
 
Sikupigii lol na utaniadithia ukiwa sawa,kuna movie storyline yake inanihuzunisha sana inaitwa Pieces of a women,story ya mdada anapenda kua na swiftie wake,mungu anamsaidia anapata Ujauzito,yeye na boyfriend wake wanatunza Ujauzito vizuri kwa upendo wote,wakishirikiana kwa kila kitu,bahati mbaya ujauzito ukatoka,dotto I cried like a little baby 😂😂..Magumu na depression aliyopitia yule dada baada ya miscarriage..huruma..
We niache bana, au nipigie nikuhadithie.
 
Sikupigii lol na utaniadithia ukiwa sawa,kuna movie storyline yake inanihuzunisha sana inaitwa Pieces of a women,story ya mdada anapenda kua na swiftie wake,mungu anamsaidia anapata Ujauzito,yeye na boyfriend wake wanatunza Ujauzito vizuri kwa upendo wote,wakishirikiana kwa kila kitu,bahati mbaya ujauzito ukatoka,dotto I cried like a little baby 😂😂..Magumu na depression aliyopitia yule dada baada ya miscarriage..huruma..
😂😂😂😂

Next time lia mbele yangu nikubonde!
 
Back
Top Bottom