Mzazi mwenzangu ananilaumu na kunitangaza kwa ndugu zangu kwamba nimekataa kumsomesha mtoto wangu!

Poleni na majukumu wana jamvi, Binafsi staki kuwachosha, Baali nina jambo ambalo naomba kushea nanyi ili hata kupata uzoefu au hata idea tu maana maarifa elimu na uwezo wa kufikiri niliona nao mimi haiwezi kuwa sawa na mtu mwingine.
Pole sana Mkuu
 
Kabisa hivi tunaongea mtoto yuko nyumbani amefukuzwa ada
Pole sana,najua wanawake wanakosa sana elimu ya kujitambua,,anaharibu future ya mtoto kwa mambo ya kipuuzi..........vipi huwezi mshauri mumpeleke zile shule za serikali zinazofundisha kiingereza?Ada 300000 na vikorokoro labda laki 600000 kwa mwaka,halafu stop matumizi,,,unakuwa unatoa Mambo muhimu Kama nguo na matibabu
 
Kwanza mzazi mwenzio akisha jua kwamba umeoa, hana cha kupoteza.
Sasa dawa ni kukaza tu, hakuna kumpa matumizi ya mtoto wala nini. Akiona hawezi kulea bora akupe mwanao mlee mwenyewe.
Yes,hili nalo neno,Bora achukue mtoto akae nae mwenyewe...
 

Kaka niljaribu na shule nikapata ila hataki kuelewa
 

Asante mkuu kwa ushauri
 
Asikusumbue akili,Kama umeoa chukua mtoto,asikugeuze kitega uchumi!maana hiyo laki tu unayotuma Kila mwezi wewe ni baba unajielewa sana alitakiwa akuheshimu

Kila mwezi natuma laki mkuu na bado mtoto matibabu nimemkatia bima NHIF
 
Ukiuza toa risifi
Ukinunua toa risiti.

Kama unashiriki kulipa ada basi hakikisha unapata risiti au unafanya bank transfer kwa akaunti ya shule.

Kama kuna matumizi ya mtoto hakikisha unayatoa kwa ushahidi wa afisa ustawi wa jamii. Au nenda Dawati la Jinsia awe anapokelea huko.

Mkuu ukizubaa atakutengenezea mazingira ya kukukamua zaidi
 
The way umeelezea hiki kisa ni wazi kuwa huyo mwanamke wako hajitambui. Haiingii akilini kuwa alifanya maamuzi ya kupeleka mtoto shule ya gharama akijua wazi jukumu la kulipa hataweza kulibeba yeye binafsi wala wewe na yeye pamoja.

Kwa umri wa mtoto unaweza kumchukua na kumlea wewe ila sheria itakutaka uwe na mke wa mkumlea huyo mtoto hata kama si mama yake mzazi.

Toa shaka mtoto akishafika umri huo kumlea ni rahisi na hautashindwa. Umri huo sio umri wa kumuacha mtoto na mama tu kwa maana ndio umri watoto huharibika tabia na kuanza kuwa na mienendo ya hovyo.

Ukiendelea kumuacha hapo atakuharibia mtoto huyo mwanamke anaonekana hayupo serious na Maisha, mahusiano na malezi ya watoto.
 
Mi hata sikuonei huruma utajua mwenyewe. Una familia lakini bado unazaa nje hovyo hovyo.
Ndo maana mnakufa mapema.
Fata ushauri wa wadau
 
Simamia hapo hapo, maamuzi ya mwanamke siku zote hayaangalii mbele itakuwaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…