Mzazi mwenzangu ananilaumu na kunitangaza kwa ndugu zangu kwamba nimekataa kumsomesha mtoto wangu!

Mzazi mwenzangu ananilaumu na kunitangaza kwa ndugu zangu kwamba nimekataa kumsomesha mtoto wangu!

Poleni na majukumu wana jamvi, Binafsi staki kuwachosha, Baali nina jambo ambalo naomba kushea nanyi ili hata kupata uzoefu au hata idea tu maana maarifa elimu na uwezo wa kufikiri niliona nao mimi haiwezi kuwa sawa na mtu mwingine.
Pole sana Mkuu
 
Kabisa hivi tunaongea mtoto yuko nyumbani amefukuzwa ada
Pole sana,najua wanawake wanakosa sana elimu ya kujitambua,,anaharibu future ya mtoto kwa mambo ya kipuuzi..........vipi huwezi mshauri mumpeleke zile shule za serikali zinazofundisha kiingereza?Ada 300000 na vikorokoro labda laki 600000 kwa mwaka,halafu stop matumizi,,,unakuwa unatoa Mambo muhimu Kama nguo na matibabu
 
Kwanza mzazi mwenzio akisha jua kwamba umeoa, hana cha kupoteza.
Sasa dawa ni kukaza tu, hakuna kumpa matumizi ya mtoto wala nini. Akiona hawezi kulea bora akupe mwanao mlee mwenyewe.
Yes,hili nalo neno,Bora achukue mtoto akae nae mwenyewe...
 
Pole sana,najua wanawake wanakosa sana elimu ya kujitambua,,anaharibu future ya mtoto kwa mambo ya kipuuzi..........vipi huwezi mshauri mumpeleke zile shule za serikali zinazofundisha kiingereza?Ada 300000 na vikorokoro labda laki 600000 kwa mwaka,halafu stop matumizi,,,unakuwa unatoa Mambo muhimu Kama nguo na matibabu

Kaka niljaribu na shule nikapata ila hataki kuelewa
 
Acha kumpa matumizi na hana cha kukufanya, zaidi atakushtaki dawati au ustawi. Kule ukiitwa wenenda na ukasimamie kwamba unamtaka mwanao kwasababu mama yake ameshindwa kumlea na amempeleka kwa bibi yake. Pia ongezea kwamba hauna imani na mama wa mtoto wako kwasababu haujui kama kweli pesa unazo mpatia anamhudumia mwanao.

Asante mkuu kwa ushauri
 
Asikusumbue akili,Kama umeoa chukua mtoto,asikugeuze kitega uchumi!maana hiyo laki tu unayotuma Kila mwezi wewe ni baba unajielewa sana alitakiwa akuheshimu

Kila mwezi natuma laki mkuu na bado mtoto matibabu nimemkatia bima NHIF
 
Poleni na majukumu wana jamvi, Binafsi staki kuwachosha, Baali nina jambo ambalo naomba kushea nanyi ili hata kupata uzoefu au hata idea tu maana maarifa elimu na uwezo wa kufikiri niliona nao mimi haiwezi kuwa sawa na mtu mwingine.

Iko hivi mimi ni mwnaume na naishi dsm nina mwanamke ambaye nilizaa nae mtoto mmoja wa kike ana miaka 7 sasa, Tangu mtoto kuzaliwa mimi kama baba nilihakikisha anapata kila kitu ambacho kiko ndani ya uwezo wangu kutimiza mahitaji muhimu kadri ya uwezo ikiwemo bima ya afya. Mtoto alikua vizuri nashukuru Mungu kwa hilo.

Alipofikisha umri wa kwenda shule tukaongea na mama yake vizuri na tukakubaliana mtoto asome kwenye shule za kawaida kwa sababu ya uwezo na kipato tunachoingiza kwa mwezi. Mtoto akaaandikishwa shule ya msingi na akaanza darasa la kwanza, Ulipofika mda wa kuingia darasa la pili mama mtu akamhamisha mtoto bila hata kuniuliza au kunitaarifu tu, Akamtoa shule ya kawaida na kumpeleka shule ya private ambayo ada yake kwa mwka kipindi hicho ilikuwa ni 1,900,000/= (Milioni moja na laki tisa) kwa sasa ni almost 2,300,000/= million mbili na laki tatu).

Sasa siku moja nilimpigia simu bibi yake mtoto (yaani mama yake na baby mama) kama kumsalimia tu ndio akaniambia niandae ada mtoto amehishiwa shule ya private. Nikashangaa na kumuuliza mbona sina taarifa hiyo na imekuwaje mmefanya hivyo bila kunishirikisha? Akasema yeye hajui alijua nimejulishwa labda nimuuliza mama mtoto!

Nilipompigia mama wa mtoto kumuuliza why umehamisha mtoto bila kuniambia?! Akanijibu mtoto wangu hawezi soma Saint Kayumba hivyo nimeamua kumhamisha mwenyewe na nitalipa ada mwenyewe hata usipo lipa wewe haitanishinda! Nikamsihi mno na kumwambia kuhusu future na kumweleza kama atasoma shule ya kawaida tutakuwa comfortable kumtengenezea mazingira mazuri tu ya kufaulu vizuri asome kwa furaha! But akakataa kata kata!

Ilikuwa ugomvi na nikaambiwa mimi baba gani sijali na sina mapenzi na mtoto kwanini nimsomeshe shule za saint kayumba, But ukweli ni kwamba mshara wangu haufiki hata milioni moja na tayari na mimi nina familia so nilijua siwezi aford ukilinganisha na pesa niniayoipata kwa mwezi. Actually yeye ananizidi mashara pengine nikajua hiyo ndio inampa nguvu kusema yote hayo.

Mwisho wa siku mimi nikabaki na msimamo wangu wa kutoa pesa ya mahitaji tu amabayo nilikuwa naitoa kila mwenzi tangu mwanzo, kimsingi huwa natoa 100,000/= kila mwezi kama pesa ya mahitaji ya mtoto!.

Tukaenda hivyo kwa mda mcheche, ikafika kipindi akaanza kunisumbua kuwa nilipe ada ya mtoto, Binafsi nilimwambia sina na badala yake nikaendelea kutotoa pesa ya mahitaji tu ya kila mwezi na hyo nimekuwa nikitoa kwa mda wote na sijawahi kukosa kutoa. Nikamwambia alipe ada kama alivyosema anaweza wala hanitegemei! Ama adundulize hiyo nayotuma kila mwezi ada ikifika alipe kwani mimi sina pesa inyingine napo hakunielewa.! Sasa Imefika hatua anamwambia mtoto wangu kwamba baba yako amekataa kukusomesha, mara apigie simu ndugu zangu na marafiki na akilalamika na kuwaambia nimekataa kusomesha mtoto!

Nimemwambia kama ameshindwa anipe mtoto wangu nimchukue na niishi nae mimi nimtafutie shule nyingine ambayo kidogo iko affordable pia hataki, yeye na mtoto wanaishi Mwanza mimi niko dsm na mtoto yuko darasa la tatu sasa!

Sasa ebu niambieni jamani nafanyaje katika hili na hasa kwa mama mtoto kama huyu na jeuri kiburi hasikilizi la mtu isipokuwa alopanga yeye!
Je niapambane tu nilipe ada ama nikaze tu!
Ukiuza toa risifi
Ukinunua toa risiti.

Kama unashiriki kulipa ada basi hakikisha unapata risiti au unafanya bank transfer kwa akaunti ya shule.

Kama kuna matumizi ya mtoto hakikisha unayatoa kwa ushahidi wa afisa ustawi wa jamii. Au nenda Dawati la Jinsia awe anapokelea huko.

Mkuu ukizubaa atakutengenezea mazingira ya kukukamua zaidi
 
The way umeelezea hiki kisa ni wazi kuwa huyo mwanamke wako hajitambui. Haiingii akilini kuwa alifanya maamuzi ya kupeleka mtoto shule ya gharama akijua wazi jukumu la kulipa hataweza kulibeba yeye binafsi wala wewe na yeye pamoja.

Kwa umri wa mtoto unaweza kumchukua na kumlea wewe ila sheria itakutaka uwe na mke wa mkumlea huyo mtoto hata kama si mama yake mzazi.

Toa shaka mtoto akishafika umri huo kumlea ni rahisi na hautashindwa. Umri huo sio umri wa kumuacha mtoto na mama tu kwa maana ndio umri watoto huharibika tabia na kuanza kuwa na mienendo ya hovyo.

Ukiendelea kumuacha hapo atakuharibia mtoto huyo mwanamke anaonekana hayupo serious na Maisha, mahusiano na malezi ya watoto.
 
Simamia hapo hapo, maamuzi ya mwanamke siku zote hayaangalii mbele itakuwaje.
Poleni na majukumu wana jamvi, Binafsi staki kuwachosha, Baali nina jambo ambalo naomba kushea nanyi ili hata kupata uzoefu au hata idea tu maana maarifa elimu na uwezo wa kufikiri niliona nao mimi haiwezi kuwa sawa na mtu mwingine.

Iko hivi mimi ni mwnaume na naishi dsm nina mwanamke ambaye nilizaa nae mtoto mmoja wa kike ana miaka 7 sasa, Tangu mtoto kuzaliwa mimi kama baba nilihakikisha anapata kila kitu ambacho kiko ndani ya uwezo wangu kutimiza mahitaji muhimu kadri ya uwezo ikiwemo bima ya afya. Mtoto alikua vizuri nashukuru Mungu kwa hilo.

Alipofikisha umri wa kwenda shule tukaongea na mama yake vizuri na tukakubaliana mtoto asome kwenye shule za kawaida kwa sababu ya uwezo na kipato tunachoingiza kwa mwezi. Mtoto akaaandikishwa shule ya msingi na akaanza darasa la kwanza, Ulipofika mda wa kuingia darasa la pili mama mtu akamhamisha mtoto bila hata kuniuliza au kunitaarifu tu, Akamtoa shule ya kawaida na kumpeleka shule ya private ambayo ada yake kwa mwka kipindi hicho ilikuwa ni 1,900,000/= (Milioni moja na laki tisa) kwa sasa ni almost 2,300,000/= million mbili na laki tatu).

Sasa siku moja nilimpigia simu bibi yake mtoto (yaani mama yake na baby mama) kama kumsalimia tu ndio akaniambia niandae ada mtoto amehishiwa shule ya private. Nikashangaa na kumuuliza mbona sina taarifa hiyo na imekuwaje mmefanya hivyo bila kunishirikisha? Akasema yeye hajui alijua nimejulishwa labda nimuuliza mama mtoto!

Nilipompigia mama wa mtoto kumuuliza why umehamisha mtoto bila kuniambia?! Akanijibu mtoto wangu hawezi soma Saint Kayumba hivyo nimeamua kumhamisha mwenyewe na nitalipa ada mwenyewe hata usipo lipa wewe haitanishinda! Nikamsihi mno na kumwambia kuhusu future na kumweleza kama atasoma shule ya kawaida tutakuwa comfortable kumtengenezea mazingira mazuri tu ya kufaulu vizuri asome kwa furaha! But akakataa kata kata!

Ilikuwa ugomvi na nikaambiwa mimi baba gani sijali na sina mapenzi na mtoto kwanini nimsomeshe shule za saint kayumba, But ukweli ni kwamba mshara wangu haufiki hata milioni moja na tayari na mimi nina familia so nilijua siwezi aford ukilinganisha na pesa niniayoipata kwa mwezi. Actually yeye ananizidi mashara pengine nikajua hiyo ndio inampa nguvu kusema yote hayo.

Mwisho wa siku mimi nikabaki na msimamo wangu wa kutoa pesa ya mahitaji tu amabayo nilikuwa naitoa kila mwenzi tangu mwanzo, kimsingi huwa natoa 100,000/= kila mwezi kama pesa ya mahitaji ya mtoto!.

Tukaenda hivyo kwa mda mcheche, ikafika kipindi akaanza kunisumbua kuwa nilipe ada ya mtoto, Binafsi nilimwambia sina na badala yake nikaendelea kutotoa pesa ya mahitaji tu ya kila mwezi na hyo nimekuwa nikitoa kwa mda wote na sijawahi kukosa kutoa. Nikamwambia alipe ada kama alivyosema anaweza wala hanitegemei! Ama adundulize hiyo nayotuma kila mwezi ada ikifika alipe kwani mimi sina pesa inyingine napo hakunielewa.! Sasa Imefika hatua anamwambia mtoto wangu kwamba baba yako amekataa kukusomesha, mara apigie simu ndugu zangu na marafiki na akilalamika na kuwaambia nimekataa kusomesha mtoto!

Nimemwambia kama ameshindwa anipe mtoto wangu nimchukue na niishi nae mimi nimtafutie shule nyingine ambayo kidogo iko affordable pia hataki, yeye na mtoto wanaishi Mwanza mimi niko dsm na mtoto yuko darasa la tatu sasa!

Sasa ebu niambieni jamani nafanyaje katika hili na hasa kwa mama mtoto kama huyu na jeuri kiburi hasikilizi la mtu isipokuwa alopanga yeye!

Je, niapambane tu nilipe ada ama nikaze tu!
 
Back
Top Bottom