Mzazi wako anapokuwa kwenye mahusiano rasmi yaheshimu kama kweli unampenda

Mzazi wako anapokuwa kwenye mahusiano rasmi yaheshimu kama kweli unampenda

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Wengi tungependa kuishi na kulelewa na wazazi wetu waliotuzaa lakini maisha yana changamoto nyingi. Kuna wanaozaliwa na wazazi wanapoteza maisha, wengine ni matokeo ya kubakwa, wengine ni mimba za ujanani wakati wazazi wote hawana dira za maisha.

Wengi wetu pale unapomuelewa mtu na kuanza kumfikiria kwa maisha ya baadae ndipo unamueleza kuhusu watoto ulio nao. Maana hizi gym na make up siku hizi mama wa watoto wanne anaonekana bado kigori kabisa.

Shida inakuja kwa watoto kuanza kumkubali baba au mama mpya. Inawezekana ulishawapa utaratibu wa kuendesha maisha yao ya kila siku mfano mdogo tu ni nyama, ukirudi uji kuta imekwisha unatafuta mboga ya kesho, mama mpya anakuja na serikali mpya kuwa kilo ya nyama lazima ikate siku mbili.

Hakuna mzazi anayependa watoto wake wapate shida lakini na watoto waelewe mtu mzima kuishi bila mwenza ni changamoto. Wapeni ushirikiano. Juzi rafiki yangu ameitwa mke bandia mke halali alikua mama yetu. Sasa kama mama yenu ni mke halali yuko wapi sasa hivi?
 
Mama binadamu ameumbwa kutokubali mabadiliko kiurahisi labda awe mtoto mdoogo sana, ila mabadiliko ynapokuja ukubwani halafu yakawa na matokeo hasi kutoka mtindo wa maisha uliozoeleka hapo moto lazima uwake aisee.
 
Mama binadami ameumbwa kutokubali mabadiliko kiurahisi labda awe mtoto mdoogo sana, ila mabadiliko ynapokuja ukbwani halafu yakawa na matokeo hasi kutoka mtindo wa maisha uliozoeleka hapo moto lazima uwake aisee.
Mabadiliko yakitokea ukubwani, elewa kuwa siku zako za kuishi pale zina hesabika, unatakiwa kuwa shuleni, chuoni au kwenye ajira na wewe uwanze maisha yako.
 
Mabadiliko yakitokea ukubwani, elewa kuwa siku zako za kuishi pale zina hesabika, unatakiwa kuwa shuleni, chuoni au kwenye ajira na wewe uwanze maisha yako.
Ukubwa sisemei 18+yrs hapana hata primary mkubwa, mwenza wa mzazi akija aendeleze mila na desturi alizozikuta sio kubadilisha mtindo wa mausha alioukuta, akaleta usioshabihiana na familia husika
 
Sahihi kabisa,

Mtu akiona kitu hakiendi anapaswa aondoke sio kuvuruga mahusiano ya Watu....

Wengine wapo kwenye Miji yao lakini kama Mzazi hasa wa Kiume akipata mwenza wake Mji wake haukaliki tena anaandaa vita kabisa ya kumtoa Mama wa Kambo utadhani Mzee wake akiumwa kiuno ataweza kumkanda.
 
Ukubwa sisemei 18+yrs hapana hata primary mkubwa, mwenza wa mzazi akija aendeleze mila na desturi alizozikuta sio kubadilisha mtindo wa mausha alioukuta, akaleta usioshabihiana na familia husika
Hapa unaweza kuweka utawala wa kidekrasia mkae mezani baba mama na watoto. Utaratibu wa zamani uwe wazi na maoedejezo mapya yawekwe. Watu wapige kura.

Pamoja na yote watoto waeleweshwe kuwa mama ni mkubwa kwao na anastahili heshima.
 
Sahihi kabisa,
Mtu akiona kitu hakiendi anapaswa aondoke sio kuvuruga mahusiano ya Watu....

Wengine wapo kwenye Miji yao lakini kama Mzazi hasa wa Kiume akipata mwenza wake Mji wake haukaliki tena anaandaa vita kabisa ya kumtoa Mama wa Kambo utadhani Mzee wake akiumwa kiuno ataweza kumkanda.
Kisa kikubwa utasikia nyumba uliijenga na mama yetu, lakini mzee nae alikua na mchango wake.
 
I think changamoto kubwa kwa sisi wabongo ni kutowaandaa wanafamilia kisaikolojia kuhusu entry ya new member kama mzazi wa kambo. Mostly ni tamko linatolewa ghafla ambalo kila mtu anatakiwa afuate bila kuhoji. Thats why wamama wengi wanaoolewa kwenye nyumba ambayo ina taratibu zake wanakutana na vizuizi vingi hasa from watoto.
Nadhani ingekua heri if hao watoto wangeanza kuandaliwa mapema na wao pia kutoa views zao kuhusu hili suala. Pia huyo mama mpya ni muhimu kuspend time na wanafamilia ili aone how to adjust
 
Ukitaka kuwe na furaha,wewe baba tafuta beki 3 wa kuwahudumia watoto

Furaha ya mwili tafuta mwanamke wa kutumia tu muwe mnalala chumba cha nje kama huna jenga.

Una watoto watatu unaoa tena ili iweje.

Hujawaongelea mama zetu hasa wajane hata kama ana miaka 45,jamani nawaombeni nao tusiwabuguzi tunapogundua wamepata wenzi wapya,waacheni wafurahie maisha pia waburudishe miili yao
 
I think changamoto kubwa kwa sisi wabongo ni kutowaandaa wanafamilia kisaikolojia kuhusu entry ya new member kama mzazi wa kambo. Mostly ni tamko linatolewa ghafla ambalo kila mtu anatakiwa afuate bila kuhoji. Thats why wamama wengi wanaoolewa kwenye nyumba ambayo ina taratibu zake wanakutana na vizuizi vingi hasa from watoto.
Nadhani ingekua heri if hao watoto wangeanza kuandaliwa mapema na wao pia kutoa views zao kuhusu hili suala. Pia huyo mama mpya ni muhimu kuspend time na wanafamilia ili aone how to adjust
Umeongea kitu cha muhimu sana, tatizo kubwa ni mirathi, unakuta nyumba aliyoacha mama watoto wanaumia kuona mwanamke mwingine anakaa mle hasa chumbani kwa mama yao.

Kama una uwezo jenga nyumba nyingine au pangisha nyumba muanze maisha mapya.
 
Kinachokera unakuta mzazi anapata mwenza asiye na mbele wala nyuma kiuchumi anakuja kwenye familia anaanza kujifanya yeye ndio mmiliki wa uchumi wa mzazi pia kuwa na matumizi mabaya ya pesa.
Fikiria leo ni nani atakataa mama yake apendane na mtu anayejiweza kiuchumi?
Tatizo linakuja mama anapendane na choka mbaya halafu anamleta nyumbani kwa watoto wake kula maisha.
 
Umeongea kitu cha muhimu sana, tatizo kubwa ni mirathi, unakuta nyumba aliyoacha mama watoto wanaumia kuona mwanamke mwingine anakaa mle hasa chumbani kwa mama yao.

Kama una uwezo jenga nyumba nyingine au pangisha nyumba muanze maisha mapya.
Kwa sisi waafrika ni heri ukajenda kwingine watoto wawe wanakuja kukusalimia tu maana hatujafikia ustaarabu wa kuishi na mama mpya ndani kwa amani
 
Umeongea kitu cha muhimu sana, tatizo kubwa ni mirathi, unakuta nyumba aliyoacha mama watoto wanaumia kuona mwanamke mwingine anakaa mle hasa chumbani kwa mama yao.

Kama una uwezo jenga nyumba nyingine au pangisha nyumba muanze maisha mapya.
Yes. Baba kama unataka kuishi kwa amani na mkeo mpya (mama wa kambo wa watoto wako); usimlete mkeo mpya kwenye nyumba uliyojenga na mkeo wa zamani. Bora hata ukapange huko na huyo mkeo, bila hivyo tegemea vita vikali kutoka kwa watoto wako. Hiyo nyumba ni ya mama yao sio ya mkeo mpya. Wanaweza wakagugumia kimyakimya ila siku ukidondoka paaa; huyo mkeo mpya na wanawe watatafuta pa kwenda
 
Mabinti ndio husumbua zaidi kuliko watoto wa kiume Hilo nimeliona Sana.
Sana. Mara nyingi wamama wa kambo wanapata changamoto sana wanapoolewa na mwenza mwenye watoto wa kike kuliko kwa watoto wa kiume. Wanawake tuna asili ya kugombania upendo/attention; tunakuwa kama wake wenza
 
Ni kawaida ya watoto wa kike kuwaonea wivu baba zao; kama ambavyo watoto wa kiume mnawaonea wivu mama zenu

Sisi wanaume tunakuwa na wakati mgumu pale Baba WA kambo anapotekeleza majukumu yake ya kuleta heshima na nidhamu ya Mama, Kama kumfokea au kumpiga.

Kiukweli ho mfumo unaweza leta mapigano Kati ya mtoto wa kiume na Baba yake wa kambo
 
Back
Top Bottom