Mzee Akilimali: Yanga haiwezi kukodishwa kama masufuria

Eti kamati ya mwafaka...kamati hii imetoka wapi kwenye katiba ya yanga.
Huyu mzee atakuwa kapigwa chini kwenye "benchi la ufundi"
ha haha
 
Labda nijibu swali kwa swali
Nitajie kiongozi wa Yanga kabla ya Manji ambaye amefanya kitu wewe unacho hisi unakikumbuka mpaka leo.

Ukifanikiwa kumtaja ntarudi, ukishindwa kumtaja maana yake hakuna kiongoz wa yanga alowagi fanya chochote


Umesahau kua sasa hivi deni la yanga ni bilion kumi na moja(11) wakati Madega anakabidhi ofisi timu haikua na deni sasa hivi inadaiwa bilioni kumi na moja. Na alisema akikabidhiwa timu itamchukua miaka minne kulipa deni.
 
Kabla ya maamuzi sahihi jipe muda sio kukurupuka msije mkamujuta na kutafuta mchawi tathmini kura wazo kwa umakini upande upi uko sawa
 
Yanga a.k.a vyura sio masifuria ya sherehe mkuu, bangachori aanzishe timu yake
Huyo mwenye njaa zake kwa nini yeye asianzishe timu yake. Wenye timu kama wameamua who cares?
Wamatopeni wanauza nyumba ili wakaishi guest house. Wenyewe kama wameamua nani ngulumbili wa kuzuia?
 
Timu inakodishwa kama wahayamalaya wa uwanja wa fisi
 
Kama Manji ana nia nzuri na Yanga bhax aisaidie timu bila kujikodishia, Haina haja ya kujikodishia timu baada kwa miaka kumi, Akiwa mwenyekiti kwa miaka kumi ni sawa lkn sio kujikodishia timu. Huyo muhindi alikuwa na plan zake cku nyingi, Cha kwanza kilikuwa ni kuwin mioyo ya wana Yanga hlfu kufanya na kukipata anachotaka kutoka Yanga(Maslahi yke binafsi)
 
Hao wazee waje kwenye mkutano tarehe 23 kama wana hoja .na huyu MZEE akilimali alishafukuzwa uanachama na sasa anatafuta nini sasa?

Ni nani aliyemfukuza uanachama mzee Akilimali????.....Pengine hamuijui historia ya YANGA...Klabu hii siyo ya kufukuzafukuza ovyo wanachama...wanachama ndio ambao hujiweka kando na siyo kufukuzwa....Halafu kwanini YANGA ikodishwe???? Huyo Manji ameshindwa nini kuitumia nembo au logo hiyo akiwa yeye ni Mwenyekiti????Ni kwanini anataka kampuni yake aliyoianzisha ndiyo itumie logo hiyo??? Kukodisha timu kuna faida gani??? Je, faida hizo haziwezi kupatikana bila kukodisha???
 
Hayo ni kweli na gharama ya ubingwa huo ni hayo mabilioni anayowadai!Unadhani kununua match mchezo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…