Mzee Akilimali: Yanga haiwezi kukodishwa kama masufuria

Mzee Akilimali: Yanga haiwezi kukodishwa kama masufuria

Sasa wamiliki si ndo uongozi wenyewe mana anachagua bodi yake yeye mwenyewe na si wanachama..Uboro wa Azam FC haina migogoro kama ya timu ambazo zina umri wa babu,inajiendesha yenyewe kwa faida bila kukopakopa na ni timu inayoonyesha upinzani katika ligi kuu
Upinzani upi huo? Labda Tigopesa & Mpesa ndo upinzani mlio nao.. Azam Fc haijawahi kutangaza mapato yake, unaweza vipi kusema inajiendesha kwa faida ?

Azam Fc 1 - 1 Mtb ..
 
Upinzani upi huo? Labda Tigopesa & Mpesa ndo upinzani mlio nao.. Azam Fc haijawahi kutangaza mapato yake, unaweza vipi kusema inajiendesha kwa faida ?

Azam Fc 1 - 1 Mtb ..
Sasa itangaze mapato yake kwani inagawana na wanachama wake?
 
Siku kadhaa kabla ya kufanyika mkutano wa Yanga, Kamati ya Mwafaka ya Wazee wa Yanga imezungumza na waandishi wa habari kuhusu mfumo ambao mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji anataka autumie katika kuingia mkataba wa miaka 10 kuimiliki nembo ya klabu.

Katibu wa Kamati ya Mwafaka ya Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimalia amesema ambacho Manji anakifanya kinaweza kusababisha timu hiy ikaingia katika vurugu ambazo hazikuwepo kwa muda mrefu kwa sababu njia ambayo anatumia inawagawa wanachama na mashabiki kwa wengine kuutaka mfumo na wengine kuukataa.

“Hatutaki kurudi kule tulipokuwepo katika mgogoro wa miaka saba, mwaka 2003 ndiyo tukapata usuluhisho na kukubaliana kuwa litumike jina ambalo lilikubaliwa na waasisi wetu, tukakubaliana kuwa kuwe na Yanga SC na Yanga Cooperation,

“Yanga kampuni ilifishwa na kukawa na utaratibu kuwa kuwe na hisa, Yanga SC kuwe na hisa 51 na wanachama wawe na asilimia 49, na tulizunguka mikoa mingi ili kufuta mgogoro uliokuwepo na kuomba ridhaa ya wanachama wa klabu kukubali hisa,” alisema Akilimali na kuongeza.

“Tulipata mwenyekiti mpaka anatoka timu ilikuwa na Mil. 200, tukampata bwana Nchunga yeye akajiuzulu baada ya miaka miwili, tukamchagua Bwana Manji akaongoza kwa miaka miwili, kwasababu tu ya upenzi ikabidi tuikanyage katika akaongeza muda, ili tujipange na yeye ajipange ili tutafute kuongozi wa baada yake, na tukafikia hatua ya kumchagua kwa mara nyingine,

“Haijafika hata miezi nane imeibuka swala la deni la Bilioni 11 na laki sita, jambo ambalo limetushtusha sana wanayanga, limekuja tamko la mwenyekiti kuleta hoja kuwa akodishwe Yanga na lebo yake kwa muda wa miaka 10, kwasisi wote tunasema Yanga ni kubwa sana, Yanga haiwezi kukodishwa kama masufuria ya kwenda shughulini. Kupitia mimi na wazee wa kamati tumesema hatukubaliani na hilo”

Nae aliyekuwa Mwenyekiti wa Matawi ya Yanga, Mohammed Msumi amesema kutokana na Manji kuwa na mahitaji makubwa na klabu ni vyema akakaa pembeni na kuanzisha timu yake mwenyewe na kuacha Yanga iendeshwe na mfumo ambao umezoeleka.

“Kwanini anataka hili jambo haraka haraka na wakati alisema Yanga inajiendesha kwa hasara, mfanyaniashara gani anakaa sehemu ya aina hiyo, kama hawezi kufata utaratbu anaweza kuanzisha timu nyingine sio kuitaka yanga na kutumia mamlaka kwa mabavu ili tu aipate Yanga,” alisema Msumi.

Chanzo: Dewji Blog
Hao wazee waje kwenye mkutano tarehe 23 kama wana hoja .na huyu MZEE akilimali alishafukuzwa uanachama na sasa anatafuta nini sasa?
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] LABDA NIANZE KUKUULIZA

1:KWANI YANGA HAIJAWAHI TWAA UBINGWA WA LIGI KUU BARA MARA 3 NDANI YA MIAKA MINNE?
KAMA IMEWAHI KIPI KIPYA KUTOKA KWA MANJI

2: KWANI YANGA HAIJAWAI FIKA ROBO FAINALI MICHUANO YA AFRICA[emoji15]

KAMA ILISHAWAHI KIPI TUTAKACHOMKUMBUKA MANJI

3: HAUJAFUNGWA NA SIMBA KWA MIAKA MIWILI [emoji23] unamaanisha unajisifia kuifunga Simba mara 2 mfululizo NILIJUA UTAVUNJA REKODI YA MNYAMA YA KUKUFUNGA MIAKA 8 MFULULIZO [emoji23] [emoji23]

KWA HILO NDIO UTAMKUMBUKA MANJI KWA HILO

4: CLUB IMETULIA KIVIP [emoji2] [emoji2] [emoji2] HAKUNA CLUB INAYOKOSA MIGOGORO ILA CLUB NYINGI ZINAMALIZIA MATATZO YAKE CHUMBANI
kama ulimsikiliza CHUJI majuz atakupa sababu kwa nini wakipigwa 5 na SIMBA alifichua kila kitu japo mimi na wewe hatukuvijua


NARUDIA TENA NITAJIE MAMBO ALIYOYAFANYA MANJI AMBAYO ATAENZIWA HATA AKIACHANA NA SOKA[emoji1] [emoji1]

mbona hutaj kile kiwanja chabekar nyingi au mshastuka itakuwa anawapiga cheusi chekundu


NA ENDAPO UKISHINDWA KUTAJA HAPO NDIPO UNATAKIWA UKUBALIANE NA MZEE AKILIMALI KUWA YANGA NI ZAID YA MANJI NA.SIKU ZOTE MFANYABIASHARA NI MTU MJANJA SANA ANAKUWA KIMASLAHI ZAID
Vyura unafikiri watakuelewa, hao Manji wanamsujudu
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Hii njaa ya hivi vizee vinavyoamini kuwa Yanga ni mradi wao was kuwaweka mjini ni shida sana.
Nyuma yao kuna watu wanachochea yote haya na vizee vyenye njaa vinatumiwa tu.
Kwa nini hao watu wasiwe na ujasiri wa kuja na hoja mbadala mkutanoni?
Waje mkutanoni wamwage hoja zao kuwashawishi wana Yanga
Huyo mzee Akilimali Kwa nini asiseme yote hayo mkutanoni?
Yanga a.k.a vyura sio masifuria ya sherehe mkuu, bangachori aanzishe timu yake
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Manji amefanikisha timu kuwa mabingwa wa ligi kuu mara 3 ndani ya miaka mi 4, tumeshinda kombe la FA.
Tumefika robo fainali ya kombe la CAF afrika
Hatujafungwa na Simba kwa miaka miwili sasa.
At least na kipindi cha uongozi wake klabu imetulia hamna fujo fujo.
Manji anaweza kuwa ana matatizo yake ila huwezi sema hajafanya kitu, kafanya ila hajafanya kwa asilimia 100, na haja fanya kile ambacho wewe ulitaka afanye.
Humu wanaomkataa manji ni mashabiki wa simba mkuu wasikusumbue hao
 
Vyanzo vya mapoto ya Yanga SC..
1. Ada za wanachama.
2. Wadhamini (Kilimanjaro, Vodacom & Quality Group).
3. Mauzo ya vifaa yenye nembo ya club.
4. Viingilio vya mechi (mauzo ya tiketi).
5. Haki ya kurusha moja kwa moja matangazo ya mechi zao..
6. Majengo..

Kote huko Yanga wanatengeneza hela nzuri tu, pamoja na kwamba kuna gharama za kuendesha timu, haiingii akilini kusema Yanga kama timu inadaiwa na mtu mmoja zaidi ya BILIONI 11..

huku ni kupatwa kwa Yanga, kama hali itabaki kama ilivyo ndani ya miaka 20 hili deni litakuwa linakimbizana na lile la taifa..
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Na je.anashindwaje kufanya hayo mabadiriko anayoyataka akiwa Kama mwenyekiti. Kwanini apewe timu kwa mkataba alioandika yeye.
Yanga ni kubwa kumzidi manj kwahiyo wanayanga tusikubali wala kushawishika na siasa za mabomba yatatoa maziwa.
 
Sasa itangaze mapato yake kwani inagawana na wanachama wake?
Kwani Man City wakitangaza wanakuwa wanagawana na wanachama? Ukweli ni kwamba Azam FC inajiendesha kwa hasara na hilo halina mjadala. Azam FC wapo kwa ajili ya kutangaza bidhaa & huduma za Bakheresa Group. na wala hakuna kingine cha ziada.

Azam Fc wamewekeza pesa mingi kwenye timu lakini hakuna chochote wanachokifanya iwe ndani ya nchi au nje .. kiufupi wameshindwa kabla ya lengo kutimia.
 
Humu wanaomkataa manji ni mashabiki wa simba mkuu wasikusumbue hao
Kwani lazima kila kitu tuweke upinzani? igeni hata yale mazuri ya Simba Sc .. sasa mnakodisha timu ili muonekane mko tofauti na Simba Sc au mnamkomoa nani hasa?
 
Soka la sasa ni pesa, mwenye pesa ndiye anatakiwa atoe sauti. Hao wazee wanataka kuendesha yanga sasa kama 1947. Haiendi hivyo, wenye pesa waendeshe yanga sisi wengine wote tuwe mashabiki tu. Utakuwaje na sauti wakati huna pesa?

Kama kuna wakati Yanga itaingia kwenye mgogoro mkubwa ni sasa kama Yanga Yetu haitakubaliwa kukodisha. Ngoja Manji ajitoe uone vilio.
 
Hao wazee wanapiga kelele yanga ni club kubwa, wanadhani bila fedha itabaki kuwa kubwa tu.
 
Mkuu utakuwa una tatizo la kumbu kumbu siyo bure
Nenda kapitie rekod za mechi zoote utajua.
Kwanza kumbe mda wote huu nabishana na shabiki la simba, shwain wee ebu kaongelee klabu yenu huko
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] wewe ulijua mimi ni kandambili
1476910908085.jpg
 
Kwani Manji kaifanyia nini vyura fc zaid ya kununua mechi na marefa kama yeye kiboko mbona KLABU BINGWA anachemsha

cc:Madeama
LAZMA MKUBALI YANGA ISHAKUWA GARI LA MAITI KILA MTU ANAWEZA KODISHA
View attachment 420879
We pimbi muulize aunt popo anamjua manji ni nani
 

Attachments

  • 1476911553415.jpg
    1476911553415.jpg
    31.3 KB · Views: 29
Ili soka la Tanzania likue inawapasa washabiki na wapenzi wa mpira kutafakari namna ya kupata muafaka wa unazi wa Simba na Yanga kwenye vyombo vya maamuzi ya soka nchini. Yanayoendelea Yanga sasa ni kama yameachiwa makusudi. Vyombo vya maamuzi havina meno ya kusimamia kanuni kuimarisha heshima ya soka letu.

ningelikuwa kiongozi wa TFF, kuna watu wangekuwa banned hata kufika viwanjani kutokana na mchango wao wa kudumaza soka letu.

Bila kukubali kubadili mtzamo na mwelekeo tutaliacha soka la Tanzania kwenye tope zito

Nimekupm mara nyingi kuhusu issue ya kuniadd kwenye group la wakubwa nadhani upo occupied kidogo na majukumu hukuona mkuu

I ask for your consideration mkuu
 
--NDG YUSUF MANJI KWA HESHIMA NA TAADHIMA NAKUOMBA VIACHIE HIVYO VIBABU HIYO TIMU.
--WALISHA ZOEA KULA HAPO KILABUNI KTK KILA MECHI KWA SASA MFUMO UMEBADILIKA YAANI WANAUMIA KWELI.
--KIROHO SAFI WAACHIE VIBABU VIENDESHE TIMU.
 
Ninapata shida juu ya uelewa Wa wazee...kwann kama wana ushauri kinyume na yeye wasimwite tu...timu ya yanga ni kweli kubwa...ila bila pesa ni ndogo tu...hata MANJI akitoka akija mfadhili mwingine hawezi kukubali mfumo Wa upigaji uliopo....naona zama za kusajili wachezaji kwa mafungu unakuja, kila mwenye nguvu yake ataleta mchezaji...
Naona MANJI aghaili tu ili tuone huu ukubwa Wa Yanga
 
Back
Top Bottom