Mkenda01
New Member
- Dec 12, 2013
- 1
- 10
Habari wana JF
Wakati swala la kusajili kadi za simu kwa kitambulisho cha nida na alama za vidole unaingia nchini tulipewa umuhimu mbalimbali wa jambo ilo ikiwemo swala la usalama na kudhibiti utapeli kwa njia ya mtandao.
Nimeleta hoja hii kwani ni miaka sasa tangu swala la kujisajili kwa kutumia nida na alama za vidole uanze lakini bado tatizo la utapeli kwa njia ya mtandao umekuwa unaendelea kukua kwa kasi sana. Najiuliza mfumo huu wa usajili umekwama wapi kuwakamata matapeli awa ambao wanawaumiza baadhi ya watanzania na ata kusababisha umauti kwa wengine
Je hizo kadi za simu zinazotuma jumbe mbalimbali za utapeli zinasajiliwa kwa namna gani tofauti na hii iliyoelekezwa na serikali? Na kama zinasajiliwa kwa alama za vidole na nida kwanini watu awa wamekuwa hawakamatwi wakati utambulisho wao unafahamika.
Wapo wanaosema vinatumika vitambulisho vya wananchi wengine bila wao kujua, lakini kama ni kweli iko hivyo kwanini hii mitandao ya simu haiwajibishwi kwa kuwa wao wanawafahamu vijana wao waliowapa vibali vya kusajili mtaani. Kwani line inayosajiliwa mtaani haina taarifa za wakala aliemsajili?
Ninaomba kufahamu kwanini utaratibu huu wa usajili haujafanikiwa kwa kiwango kikubwa kutatua changamoto hii ya utapeli, lakini pia kushauri nini kifanyike.
Wakati swala la kusajili kadi za simu kwa kitambulisho cha nida na alama za vidole unaingia nchini tulipewa umuhimu mbalimbali wa jambo ilo ikiwemo swala la usalama na kudhibiti utapeli kwa njia ya mtandao.
Nimeleta hoja hii kwani ni miaka sasa tangu swala la kujisajili kwa kutumia nida na alama za vidole uanze lakini bado tatizo la utapeli kwa njia ya mtandao umekuwa unaendelea kukua kwa kasi sana. Najiuliza mfumo huu wa usajili umekwama wapi kuwakamata matapeli awa ambao wanawaumiza baadhi ya watanzania na ata kusababisha umauti kwa wengine
Je hizo kadi za simu zinazotuma jumbe mbalimbali za utapeli zinasajiliwa kwa namna gani tofauti na hii iliyoelekezwa na serikali? Na kama zinasajiliwa kwa alama za vidole na nida kwanini watu awa wamekuwa hawakamatwi wakati utambulisho wao unafahamika.
Wapo wanaosema vinatumika vitambulisho vya wananchi wengine bila wao kujua, lakini kama ni kweli iko hivyo kwanini hii mitandao ya simu haiwajibishwi kwa kuwa wao wanawafahamu vijana wao waliowapa vibali vya kusajili mtaani. Kwani line inayosajiliwa mtaani haina taarifa za wakala aliemsajili?
Ninaomba kufahamu kwanini utaratibu huu wa usajili haujafanikiwa kwa kiwango kikubwa kutatua changamoto hii ya utapeli, lakini pia kushauri nini kifanyike.