Mzee Bilal Rehani Waikela

Mzee Bilal Rehani Waikela

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
AF1QipOzH-zPRRXO-74T5Au_4Z-ZZ6b7NuDNv0elEVge

2016%2B-%2B1

Kushoto: Mzee Bilal Rehani Waikela na Sheikh Ponda Issa Ponda nyumbani
kwa Mzee Waikela Tabora


Leo nilitembelewa na Mzee Bilal Rehani Waikela, mwasisi wa TANU Tabora 1955 na Katibu wa EAMWS Western Province kwa miaka mingi hadi ilipopigwa marufuku na serikali mwaka wa 1968 kupisha BAKWATA.

Mzee Waikela ndiye aliyenisaidia katika kuandika sehemu ya tatu ya kitabu cha Abdul Sykes kwa kunipa nyaraka halisi za barua, ''cutting,'' za magazeti na miniti za mikutano wakati wa kile kiichokuja kujulikana kama, ''Mgogoro wa EAMWS.''

Nyaraka hizi bila ya kuogopa vitisho alizificha kwa miaka 20 hadi alipozifikisha MSAUD katika miaka ya 1980 na kupitia MSAUD zikanifikia mimi.

Nyaraka hizi alimkabidhi Mohamed Lulengelule kijana kutoka Tabora aliyekuwa Mwenyekiti wa MSAUD.

Wenzake wengi waliokuwa katika uongozi wa EAMWS katika kipindi cha Mgogoro wa EAMWS kwa hofu ya kuwekwa kizuizini walizitia moto nyaraka zao.

Ukumbi wa H.H. Aga Khan, Girls School, 1963
Nyerere alitulia tuli pembeni mwa Rais wa Baraza la Tanganyika la EAMWS Tewa Said Tewa akimsikiliza Waikela.

Aliposimama kujibu hotuba ya Waikela Nyerere kwa upole alisisitiza msimamo wa serikali wa kutoa haki na usawa kwa raia wake wote.

Kwa kiasi fulani Nyerere alikuwa amefanikiwa kupunguza joto kati ya Waislam na serikali.

Hotuba ya Waikela na ya Nyerere zikapewa umuhimu mkubwa katika Tanganyika Radio Corporation (TBC).

Waislam wengi wakajitokeza stesheni ya gari moshi Tabora kuja kumpokea shujaa Waikela.

Alipewa heshima ile kwa kuwa na ujasiri wa kuweza kusimama kidete dhidi ya wale waliodhani kuwa wanaweza kuwakalia Waislam vichwani.

Mara ya kwanza nilipomsikia Mzee Waikela anahadithia haya yaliyotokea mwaka wa 1963 Ukumbi wa Aga Khan Girls School nilisisimkwa mwili mzima na malaika wakanisimama.

Ile hadhira ilikuwa kubwa na baadhi ya waalikwa siku zile katika mikutano ya EAMWS walikuwa mabalozi kutoka nchi za Kiislam...kisa kizima kipo katika kitabu cha Abdul Sykes.

(Nilifanya mahojiano haya mwaka wa 1987 nyumbani kwa Mzee Waikela, Gongoni, Tabora, nikiwa nimesindikizwa na marehemu Ilunga Hassan Kapungu na shemeji yake Salum Ali Mkangwa ambae alikuja baadae kufasiri kitabu hiki kwa Kiswahili mwaka wa 2002).

Hizi nyaraka zipo katika Maktaba ya MSAUD sasa inakimbilia miaka 40.

Huwezi kuchoka kumsikiiza Mzee Waikela kwa hakika ni hazina na ‘’Encyclopedia,’’ ya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Katika utafiti wangu ni Mzee Waikela na Hamza Aziz ndiyo watu wawili ambao Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alipata kuwaombea dua maalum Allah awanusuru na shari zilizokuwa zimejikita katika siasa baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961.

Allah amzidishie umri mrefu na aimarishe afya yake.
 
Watu wameamua kupuuza? Why? Watu njooni huku kwa nini mnamuacha mzee peke yake?
 
Tanganyika ya 1961-1985 ilikuwa Na watu Jasiri Sana pamoja Na vitisho Na Mauaji na Mateso waliyopata

Kizazi Cha Sasa kina chui wa karatasi tu kujiita wanaharakati
 
Tanganyika ya 1961-1985 ilikuwa Na watu Jasiri Sana pamoja Na vitisho Na Mauaji na Mateso waliyopata

Kizazi Cha Sasa kina chui wa karatasi tu kujiita wanaharakati
Wapo ila madhila yanayowakuta wa sasa yanawatia woga ndio maana wengi hawachelewi kuunga mkono juhudi... wametanguliza maslahi binafsi mbele... wazee maslahi ya taifa ndio yalitangulia...
 
Dini juu ya Taifa,unaweza kuchagua kimoja kuwa juu ya kingine.Wengi huona dini ni jambo linalowaunganisha zaidi kuliko Taifa.

Mzee Rehani,pale Tabora alipewa mtaa,unaitwa Mtaa/Barabara ya Rehani,ipo kata ya Ng'ambo.Upande wa kusini inakutana na barabara ya Sikonge na upande wa Kaskazini inakutana na barabara ya Kitete iliyopo Kata ya Kanyenye.Barabara ya Kitete ndio ilipo nyumba ya Marehemu Mchemba.

Kata ya Ng'ambo mitaa ya Kazeh Hill ndipo ilipo nyumba ya Muasisi wa TANU akiitwa Kulwa(Jina lingine limenitoka).Huyu alikuwa nembo ya TANU mkoa wa Tabora.
 
Mzee Waikela akielezea kwa ufasaha kabisa kuhusu Harakati za Uhuru, Harakati za Waislamu kipindi cha uhuru n.k

 
Back
Top Bottom