Mzee Butiku: Watanzania wengi hawajaridhika Mkataba wa Bandari, tusahihishe ama tuache kabisa

Mzee Butiku: Watanzania wengi hawajaridhika Mkataba wa Bandari, tusahihishe ama tuache kabisa

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Mzee Joseph Butiku atoa ushauri wake sakata la Uwekezaji Bandari " Watanzania hawajaridhika na jambo hili,tulisahihishe ama tuliache kabisa"

----

Natoa shukrani kwa Rais wetu Dkt. Suluhu Samia kwa mambo mawili, kwanza kwa kuruhusu Watanzania kuzungumza, Watanzania tulikuwa na aibu ya kuzungumza lakini tangu Rais Samia aingie ametutaka tuzungumze, na tuzungumze waziwazi, ukweli na yote tuliyonayo moyoni

Hili jambo la bandari limeshakwenda serikalini na bungeni, raia tukaulizwa maswali kidogo na tukajibu. Baada ya hapo jambo hili la bandari lilirudi bungeni na kupitishwa na Bunge. Kwa mujibu wa utaratibu wa kikatiba, limeshapitishwa na hivyo ni la kutekeleza. Hivyo sasa wanaposema tuzungumze, tuzungumze kitu gani?

Ninaamini hoja zilizotolewa kuhusu bandari, serikali imezifuatilia. Kwa maoni yangu katika jambo hili (la bandari) ni kwamba Watanzania bado wana uoga, wasiwasi na hawana hakika kama maamuzi yaliyofanywa na serikali ni kwa faida ya nchi yao. Na sauti hiyo unaisikia nyakati zote, lakini ukitazama mitandao na ukisikiliza watu wakisema katika majukwaa mbalimbali ni kama Watanzania wanasema hatujardhika

Ukiniuliza kuhusu option ya serikali kwamba inaweza kuachana na jambo hili (la bandari), jibu langu ni ndio. Kama kuna makosa sehemu fulani fulani, kusahihisha huwa kuna gharama, hivyo serikali ikubali na kama Taifa tukubali kuwa gharama ya kusahihisha ni kubwa

Uamuzi wa kuendelea na mazungumzo haya (ya bandari) mimi haunipendezi na unaonekana unatugawa, na sijawahi kuona jambo kama hili ambalo watu wanazungumza kwa hisia kali wengine waziwazi na wengine chini chini, hata tunaodhani wamekubali pengine hawakukubali. Na tusiruhusu uamuzi wowote ukatuondolea sifa yetu ya msingi ambayo ni umoja wa Taifa hili

Wenzetu walioomba kushirikiana na sisi (serikali ya Dubai kupitia kampuni ya DP WORLD) isikilize maoni ya Watanzania na tusaidiane namna ya kuboresha maamuzi ya kutazama jambo hili (la bandari) au kuachana nalo. Na si vibaya kwa taifa letu kutazama upya jambo la bandari

Ukitoa hoja kuwa huyu mwekezaji ana meli 100 au ana utajiri mkubwa hiyo sio hoja, hoja ni kwanini uruhuhusu jambo hili (la bandari) litokee, na pia hoja ni kwamba umewashirikishaje unaowaongoza waelewe na tatu je umejiridhisha wamelielewa, na kama wamelielewa wafanye nini

Hakuna mtu anayeweza kuuza Tanzania bali mtu anaweza kufanya vitendo vya kukidhalilisha akidhani anaiuza Tanzania na hata hilo suala la uwekezaji wa bandari sio kuuza Tanzania.

Wawekezaji hata hawa wanaweka na kisha na wao wanachukua, dunia ya leo ni nipe nikupe lakini yako maeneo mengine ukifanya nipe nikupe inaleta shida ni kama mtu anagusa chumbani kwako. Bandari ni mali yetu kubwa mno ndio maana sisi inatupa shida.

Jambo
 
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Mzee Joseph Butiku atoa ushauri wake sakata la Uwekezaji Bandari " Watanzania hawajaridhika na jambo hili,tulisahihishe ama tuliache kabisa"
Mzee Butiku, TUKISUSA HAWA WAHUNI WA CCM WATAKULA TU. Tujipange kwa lolote kukomboa bandari zetu. Kuna kijana mmoja amesema wanaopigana maria space, Club house waendelee na sisi wenye ushupavu wa kushika bunduki tushike......
Mzee Butiku, lazima tuwe na la kufanya, siyo kuacha tu. Washenzi hawa watakula!
 
Kalamu ina ufutio.

Hii ikiwa na maana kwamba mwandishi anaweza kosea na kuhitaji kusahihisha.

Kwa swala hili la mkataba wa bandari.

Tujisahihishe.
 
Washenzi hawa watakula!
Mshenzi nani?
Unakusudia Raisi?
au waziri Mkuu?
au waziri wa Miundo mbinu naUchukuzi?
Yaani Unaita Serikali inayosimamia Mambo makuu ya nchi Washenzi?
Hii n Dharau ya Hali ya Juu na Ujinga .
Sijapata kuona Raia wa aina yako.
 
Leo Mzee kaongea jambo linalotakiwa kufanywa.
Hakuna Mtanzania anayepinga uwekezaji bandarini.
Tena uwekezaji wa Muwekezaji yeyote yule hata awe Mtalebani.

Kitendo tu cha Waziri kusani kwa kuiwakilisha Serikali ya Tanzania na Dubai wakati hana mamlaka ya kisheria ya kuiwakilisha Serikali ya Dubai.
Huo Mkataba Unakuwa BATILI.
 
Nilitarajia Baada ya WANANCHI kulalamikia UTARATIBU wa Kumpata MWEKEZAJI DP WORLD kuwa ZABUNI Haikutangazwa na USIRI na UBOVU wa MKATABA basi
SERIKALI MAKINI yenye kuwaheshimu na Kuwasikiliza WANANCHI wake ingekubali KUCHUTAMA na Kuwaomba RADHI Wananchi wake na kulitangazia TAIFA kuwa
MCHAKATO wa KUMTAFUTA Mwekezaji ktk BANDARI yetu UNAANZA UPYA na kuwashirikisha WANANCHI ktk KILA HATUA na kutaka MAONI na MAPENDEKEZO yao kwani BANDARI ni YETU na MAENDELEO ni YETU
Kutokuwasikiliza au Kupuuza MAONI na MAPENDEKEZO yao ni Kuwakosea sana kwani WANANCHI HAWAPINGI UWEKEZAJI ila wanataka UWAZI na UKWELI ktk RASLIMALI za NCHI.
 
Nakubaliana a wewe. Serikali itafute mwekezaji na ifuate taratibu zote za kimkataba na tupate mwekezaji aliyepatikana kwa njia ya halali. Sisi tunawataka wawekezaji sana.
 
Kukosea, kukiri na kurekebisha ndio ubinadamu, hakuna binadamu asiyeteleza.

Au ukiwa Rais wa Tanzania na ubinadamu unakwisha?

Au kukiri kuteleza na kurekebisha ni udhaifu?

Mama kelele hizi SI za kawaida na hazitakwisha Leo Wala kesho, hili jambo ni kubwa sana sauti za wengi ni sauti ya Mungu.

Usisubiri kuja kukiri hili baada ya kustaafu kama watangulizi wako, rekebisha Sasa Wala haujachelewa.
Sisi ma chawa hatutakuambia ukweli hata ukikosea sisi ni kukusifia kwa lolote lile.

Mimi pekee nimethubutu kusema hili kwani ninaupenda uongozi wako kwa dhati ukiharibu nitaumia sana.
Hili jambo litakuharibia pakubwa.

Achana na hizi kesi za uhaini mama utawaumiaza wenzetu. Bure.

Ni ushauri Tu waweza kupokea au kuukataa
 
Kukosea, kukiri na kurekebisha ndio ubinadamu, hakuna binadamu asiyeteleza.

Au ukiwa Rais wa Tanzania na ubinadamu unakwisha?

Au kukiri kuteleza na kurekebisha ni udhaifu?

Mama kelele hizi SI za kawaida na hazitakwisha Leo Wala kesho, hili jambo ni kubwa sana sauti za wengi ni sauti ya Mungu.

Usisubiri kuja kukiri hili baada ya kustaafu kama watangulizi wako, rekebisha Sasa Wala haujachelewa.
Sisi ma chawa hatutakuambia ukweli hata ukikosea sisi ni kukusifia kwa lolote lile.

Mimi pekee nimethubutu kusema hili kwani ninaupenda uongozi wako kwa dhati ukiharibu nitaumia sana.
Hili jambo litakuharibia pakubwa.

Achana na hizi kesi za uhaini mama utawaumiaza wenzetu
Bure.

Ni ushauri Tu waweza kupokea au kuukataa
Nyie vibaraka wa kanisa sijui mna matatizo gani? Mbona hamuongelee mikataba mingine mibomvu kurekebishwa kama ule wa serikali inapo poteza 36bn kila mwaka kwa taasisi za kanisa.
 
Nyie vibaraka wa kanisa sijui mna matatizo gani? Mbona hamuongelee mikataba mingine mibomvu kurekebishwa kama ule wa serikali inapo poteza 36bn kila mwaka kwa taasisi za kanisa.
Matatizo Gani kivip
 
Kukosea, kukiri na kurekebisha ndio ubinadamu, hakuna binadamu asiyeteleza.

Au ukiwa Rais wa Tanzania na ubinadamu unakwisha?

Au kukiri kuteleza na kurekebisha ni udhaifu?

Mama kelele hizi SI za kawaida na hazitakwisha Leo Wala kesho, hili jambo ni kubwa sana sauti za wengi ni sauti ya Mungu.

Usisubiri kuja kukiri hili baada ya kustaafu kama watangulizi wako, rekebisha Sasa Wala haujachelewa.
Sisi ma chawa hatutakuambia ukweli hata ukikosea sisi ni kukusifia kwa lolote lile.

Mimi pekee nimethubutu kusema hili kwani ninaupenda uongozi wako kwa dhati ukiharibu nitaumia sana.
Hili jambo litakuharibia pakubwa.

Achana na hizi kesi za uhaini mama utawaumiaza wenzetu
Bure.

Ni ushauri Tu waweza kupokea au kuukataa
Ushauri Mzuri Sana Huu.
Wahusika Wauchukue.

Mkataba urekebishwe na uendelee la sivyo ni bora kuanza upya.
 
Nyie vibaraka wa kanisa sijui mna matatizo gani? Mbona hamuongelee mikataba mingine mibomvu kurekebishwa kama ule wa serikali inapo poteza 36bn kila mwaka kwa taasisi za kanisa.
Huu mkataba ni kati ya Kanisa na nani?
 
Back
Top Bottom