Mzee Duni: Kwani CHADEMA ilipotaka maridhiano na hayati Magufuli ilikuwa CCM B? Kwanini ACT Wazalendo kuwemo katika SUK iwe nongwa?

Mzee Duni: Kwani CHADEMA ilipotaka maridhiano na hayati Magufuli ilikuwa CCM B? Kwanini ACT Wazalendo kuwemo katika SUK iwe nongwa?

Mwenyekiti wa ACT Wazalendo mzee Juma Duni Haji amesema mzee Mandela alisema hakuna fursa nzuri ya kisiasa kama ile ya kukaa na mpinzani wako na kumueleza ukweli huku unamuangalia machoni.

Hivyo hao wanaopayuka kuwa ACT Wazalendo ni CCM B hawatusumbui kwani Chadema walipoomba maridhiano na hayati Magufuli walikuwa CCM B? ameuliza mzee Duni.

Chanzo: ITV Dakika 45
nimeami majina yana mana kubwa sana huyu mzee ni duni tu kama ilivyo jina lake
 
ACT kuwepo huko SUK imekuwa nongwa kwasababu wanaonekana wote wanaburuzwa na mawazo ya mkuu wao ndio maana wajanja wameanza kuwakimbia chamani kwao.
Ukweli ni kwamba ACT ile aliyekuwepo Al Marhum Maalim Seif wa Pemba kuwepo huko SUK hakukuwa na Nongwa yoyote na ilikuwa sahihi,lakini hii ACT ya Bab Duni wa Unguja kuwepo huko SUK ni NONGWA tena kubwa saana.Muda utasema

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Watu wanashindwa kujua kuwa mageuzi ni Process ndefu. Kuna wapinzani hawakumbuki kwamba huko Zanzibar walishamaliza mbinu zote za kistarabu kutaka kuleta mageuzi. Kama ni kufa watu wamekufa zaidi kuliko sehemu yoyote ya Tanzania hii. Kama ni migomo na kususia ndio usiseme. Kama ni kufungwa ndio wamefungwa zaidi, kama ni kubambikiziwa huko ndiko kuna chuo cha kubambikizia watu, kama ni unafiki wa watawala huko ndiko kuna chuo kikuu kabisa lakini hao wanaoponda ACT na iliyokuwa CUF kuingia SUK walitaka nini?
Walitaka hata hio fursa ndogo ya kuendeleza mapambano ya ndani nayo ipotee na wapinzani wapotee kwa ujumla wake? hivi hao wanaopinga kuna walau anayefika robo ya siasa za akina maalim Seif?

Unapoishutumu ACT kisa eti Imekubali kushiriki GNu na CCM ni kushindwa kuwaheshimu Wazanzibari na madhila yao waliyopitia katika kudai mabadiliko.

Halikuwa jambo dogo hata kidogo kwa CCM kukubali kubadilisha katiba ya Zanzibar na kuwafanya wahafidhina watambjue kwamba huwezi kuongoza Zanzibar bila kuwa na Ushirikiano na wengine. Walau angeulizwa mh Aman Karume na iko siku atasema ukweli. Heshima kwa wapinzani wa zanzibar (akina Maalim Seif na wenzake mh Duni) kwa kutotoka kswenye mstari. Watu wanajuwa wanachokifanya.

Mimi nadhani kulitakiwa kuongezwe spidi tu na mikakati ya kudai mabadiliko kwa kuongezwa mbinu wakati unashikilia hicho kidogo. Wanaobeza hawajui historia ya kweli ya Zanzibar na hawajui siasa. ACT imeheshimu Muktadha wa zanzibar katika safari ya mabadiliko ya Tanzania. Kongole kwenu ACT.

Watu walishasahau maridhiano na miafaka 3 iliyofeli, kuleta mabadiliko si jambo dogo. Hapo ACT ilipofika Zanzibar ni kituo kidogo kuelekea mabadiliko kamili. Its a matter of Time. Msichojua hao wahafidhina hawataki hata kusikia Wapinzani kuwemo Serikalini na kujua mipango ya Serikali. wanaumia vibaya lkn katiba haiwaruhusu. Kwa nini usiwasifu ACT walau kwa hilo?

Nyinyi hebu nyamazeni bwana.........

..Tatizo la CUF [ sasa hivi ni ACT ] ni kushindwa kutetea ushindi waliokuwa wakiupata ktk kila uchaguzi.

..Kila walipokuwa wakishinda Maalim Seif alikuwa akiitwa PEKE YAKE ktk vikao na CCM na baada ya hapo aliwaachia ushindi.

..Kutokana na viongozi wa CUF[ sasa ACT] kukosa msimamo wa kusimamia HAKI mpaka mwisho, ndio maana CCM wameweza kuongeza dozi ya ukatili ktk kila uchaguzi mkuu unaofanyika Znz.
 
Mwenyekiti wa ACT Wazalendo mzee Juma Duni Haji amesema mzee Mandela alisema hakuna fursa nzuri ya kisiasa kama ile ya kukaa na mpinzani wako na kumueleza ukweli huku unamuangalia machoni.

Hivyo hao wanaopayuka kuwa ACT Wazalendo ni CCM B hawatusumbui kwani Chadema walipoomba maridhiano na hayati Magufuli walikuwa CCM B? ameuliza mzee Duni.

Chanzo: ITV Dakika 45
Kumbe duni ndio mwenyekiti wa act?
 
Magufuli hakuwa CCM alikuwa ni Rais wa wa Tanzania bila kujali vyama vyao tofauti na CCM ambacho ni chama cha wenye chama kwa hiyo ni halal kuomba maridhiano na Rais wa nchi.
 
Back
Top Bottom