Mzee Kinana mbona hujatuambia CCM inapata ruzuku kiasi gani?

Benderea

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2021
Posts
686
Reaction score
1,303
Nimemsikiliza Mzee wangu Komredi Kinana eti akisema wamewapa ruzuku CHADEMA na kuwapakazia akataja na kiasi. MIMI nimuulize mzee wetu, je, CCM inapata ruzuku kiasi gani?

Akisema au akitaja basi nawaambia wananchi watazirai siku hiyo! Maana ni pesa nyingi sana lakini hata haieleweki zinakwenda wapi!

Kuna anaejua CCM wanapata ruzuku kiasi gani atueleze?
 
GENTAMICENE anajua mambo mengi.Je hii habari ya ruzuku ya CCM kiasi gani na wanafanyia nini ? Hebu tuelezee kamanda
 
Swali la msingi sana hili, angekuwa kweli muungwana angesema wao ccm wanapata kiasi gani na kuweka audit ripoti hadharani inavyoonesha jinsi fedha zilivyotumika alafu sasa ndo angehoji mapato na matumizi ya wengine kama chadema, act, n.k.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Kiongozi au mtu yeyote atakayeshabikia kuhoji si ajabu atafunguliwa kesi ya uchochezi, CCM haiko tayari wananchi tujue.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…