Mzee Majuto atangaza rasmi kuacha kuigiza, sasa kumrudia Mungu wake

Mzee Majuto atangaza rasmi kuacha kuigiza, sasa kumrudia Mungu wake

Siyo rahisi kwake kufanya anayoyapanga ie kuachana na fani yake na kujikita kwenye ibada. Kwa jinsi alivyojulikana kwenye hiyo fani, watu watamjia na kumwomba akacheze kwenye mchezo fulani na ahadi ya donge nene.Atashindwa kukataa!
 
Ametufumbua macho, kumbe kuigiza ni kosa mbele za Mungu?!
 
Duh!kasema ya uzi huu inatia shaka kwa nguli kama huyu mpaka sasa comments hazijafika 30 au watu mlikuwa hamtaki apumzike?
 
MAJUTO22.jpg


Mzee majuto ambaye amejipatia umaarufu sana kwa uigizaji hususani katika Comedy ametoa kauli rasmi kuwa kwa sasa ameamua kuachana na kazi hiyo ya uigizaji na sasa kumtumikia Mungu na kuomba asamehewe makosa kwa yale aliyotenda nyuma.

Mzee Majuto amesema kuwa kwa sasa anaamini anaweza kuishi bila kutumia kipaji chake hicho cha ugizaji na muda huu atatumia kumuomba Mungu amasamehe makosa aliyotenda na kudai kuwa anaamini itawezekana kwani Mungu ndiye anayetoa ridhiki kwa kila mtu.

“Mashabiki zangu nawaomba wawe na amani tu kwa maamuzi yangu haya kwani hakuna kitu ambacho kinaishi milele kwani ni Mungu pekee ndiye anayeweza kuishi milele, imefika wakati nimeamua kumpuzika na kumtumikia Mungu, naamini maisha yatakwenda kwani kuna watu ambao hawana vipaji ila wanaishi vyema, wanatibiwa na maisha yao yanakwenda salama hivyo hata mimi nitaishi vyema’ alisema Mzee Majuto.

Source: eatv.tv
Hivi kwani kuigiza ni dhambi mpaka mtu unaacha halafu unamrudia Mungu?/
 
Attention seeker Hivi unaamini vipi kauli ya msanii?
 
Majuto na sanaa ni kama yanga na ubingwa havitengani
Nyie Manara kawatia ujinga kweli, Yanga mmeiwezesha nyinyi (simba) kwa kuipatia pointi 6 kama haitoshi mmekutana na Azam mkaitengenezea njia Yanga.
 
Karibu kwa Mungu mzee Majuto, lakini awe yule Mungu aliye hai, asiyepiganiwa na wanadamu
 
Nyie Manara kawatia ujinga kweli, Yanga mmeiwezesha nyinyi (simba) kwa kuipatia pointi 6 kama haitoshi mmekutana na Azam mkaitengenezea njia Yanga.
Anzisha thread nyingine, watakuwekea picha ya 5-0 halafu siku yako iharibike ghafla
 
Mkuu macho yako yana matatizo gani mbona hiyo statement iko wazi kama nguzo za umeme
 
Siyo rahisi kwake kufanya anayoyapanga ie kuachana na fani yake na kujikita kwenye ibada. Kwa jinsi alivyojulikana kwenye hiyo fani, watu watamjia na kumwomba akacheze kwenye mchezo fulani na ahadi ya donge nene.Atashindwa kukataa!
Huu ndio Ukweli.[emoji106]
 
Back
Top Bottom