Mzee Makamba, Kama unataka January awe Rais chunga ulimi wako usimharibie

Mzee Makamba, Kama unataka January awe Rais chunga ulimi wako usimharibie

Nimetazama clips za hotuba ya Kikwete na Makamba kwa umakini nikaona hawa wazee safari hii walikuwa wana hasira hatari. JK huwa yuko soft kwenye hotuba zake ila jana alikuwa wa moto mno. Neno mpuuzi, wapuuzi kalitaja mara kadhaa. Yaani hakuwa na masikhara hata kidogo. Makamba alikuwa na hisia kali toka juzi akihojiwa na waandishi. Mzee Makamba ndo alishindwa kabisa kuji-control. Bado sijaelewa kabisa sababu za wazee kucharuka hivi. Halafu mbona Bashiru alikuwa ka-relax kabisa? Nitafuatilia vizuri.
 
Kwa hali ya siasa inavyo elekea kama Chadema wasingefanya upuuzi na unafiki wa kumleta Lowasa Ukawa kwa hali ilivyo hivi sasa Chadema ingekuwa mioyoni mwa watu.

Sijui upinzani wamejipangaje ila tozo, mgao wa umeme, kodi na upandaji wa mafuta umewagusa sana watu wa chini.Ukichenji elfu 10 inayeyuka faster, hiyo laki ndio kabisa, yaani hela ngumu halafu hazikai.

Tatizo kila nikiwatizama upinzani simuoni mtu,huku kwenye tawala ndio kabisa HAMNA. So naamini nchi yetu tutasonga kwa huruma ya Mungu.
Wapo kuna henche(huyu atainyorosha nchi)😂,mnyika, john mrema, pambalu,, hawa mbona wanaweza san tu
 
Wapo kuna henche(huyu atainyorosha nchi)😂,mnyika, john mrema, pambalu,, hawa mbona wanaweza san tu
Hamna kitu, siasa 2015 kwa mtu mfuatiliaji wa siasa tokea 2005 -2015 ,utajua siasa zetu wasaka Tonge wapo wengi,wanafiki wengi wanaweza kuiuza hata nchi.

Ndio maana siku hivi vyama vya upinzani havina plan wacreate vijana wao na hata watu waliokulia kwenye system yao hawa waamini na ndio maana wakamteua Lowasa.
 
Back
Top Bottom