Mkuu Udadisi,
Nimekusoma na pia nakubalina nawe kwa hoja/wazo hilo!
Nafikiri hivi sasa ni wakti muafaka umefika kwa Serikali yetu nayo kujifunza na kujaribu kuonyesha nia na dhamira za kuwaenzi na kuwathamini Wanataaluma wetu khasa Historians!?
Pia viongozi/wanasiasa wetu ifikie wakti wajaribu kukubali ukweli mchungu wa kihistoria na kuuweka bayana kwa Watanzania woote...khasa vizazi vijavyo!?
Kwa mfano kiduchu...inatia simanzi mno kuona yakua mpaka kesho wanafunzi wetu woote pale nchini,hata walioko kwenye vyuo vya juu,bado wanasoma/wanakarishwa history ambazo hata hao ma-Lecturers/Waalim wao na pia viongozi/wanasiasa woote...wanafahamu yakua ni history iliyochakachuliwa/iliyopotoshwa kwa makusudi!? Daah!
Kwa kifupi,tunaishi katika Taifa ambalo tumekubali sisi wenyewe na hata vizazi vyetu vijavyo wawe misukule/waliokaririshwa upotoshwaji wa kihistoria!? Daah!
Kwa mfano kiduchu,nasikia mpaka leo ati pale Mlimani-UDSM...ati wanakataa kufundishia/kutumia maandiko ya Maalim Mohamed Said kwa kisingizio/kigezo cha "udini" uliomo kwenye maandiko yake!? Daah!
Je kwa mfano pamefanzika jitihada zipi za kitaaluma ku-challenge au kujaribu kurakabisha hayo "makosa" ya "udini" tunayoaminishwa yakua yametamalaki ndani ya maandiko ya Maalim Mohamed Said!?...jibu ni hakuna kabisa! Daah!
Sasa badala ya Wanataaluma kujaribu kuwa mfano wa ku-encourage dialogue among themselves...lakini unakuta vyuo vyoote muhimu hapo nchini na hata serikali/wizara husika...wooote kwa pamoja wameamua kumbeza na kumweka kando Mwanahistoria/Mwanataaluma mwenzao,kwa visingizio vya kitoto na vya kipuuzi kabisa!? Daah!
Tuko pamoja Kaka!
Watu wengine wanasoma au wanasikiliza bila kujua kuna kitu kinaitwa critical thinking
Kuna hoja mbili kuhusu hili
1.Mohamed ameondoa ushiriki wa watu makusuadi katika historia anayosema ni ya Tanganyika, ingawa mambo yakibana husema ya wazee wake na ikiwa ngumu zaidi husema ya Waislam
Kosa ambalo Kivukoni walifanya kwa kutotambua michango mingine, kwake lina uhalali
2. Historia ina formula, kuieleza au kuiandika kwa mujibu wa matukio na wakati kama ilivyo
Jaribio la ku ''interject'' personal feelings or ideas, historia husota madole ya machoni dhahir shahir
Kwa waliosikiliza video, Mohamed anasema Kleist Sykes aliunda AA na kisha Jamii fil Islamiya 1933. Mohamed hakueleza chochote kuhusu Cecil Matola.
Kumtaja Cecil ni kumtaja Rais wa kwanza na hivyo hoja ya Kleist kuunda AA inakufa.
Katika maandishia anasema, Kleist aliunda kwasababu alikuwa na pesa na mashuhuri.
Mohamed haelezi Cecil Matola alikuwa msomi na 'immunity' dhidi ya Wakoloni kuliko Kleist
Tendo la kutomtaja Matola, historia haikukaa kimya imemnyooshea kidole
3. Mohamed anasema Abdul Aliunda TANU, Nyerere akiwa Rais wa TAA kabla ya 1954.
Kitendo cha kumuondoa Nyerere, historia inamzaba kibao Mohamed.
Huwezi kuwa Rais wa chama asiyejua transformation. Abdul hakuunda TANU, alishiriki
1929 cecil akiunda AA hadi uchaguzi katika miaka ya 1950 Abdul ni takribani miaka 23.
Kleist na Mwanawe Abdul walibaki na uana harakati kwa miaka 23.
Nyerere aliandika katiba ya TANU katika transformation ya chama kuwa ya kisiasa
Akafungua milango UN kwa kutumia usomi, na kupata Uhuru katika miaka 10
Mohamed hasemi hilo, lakini historia inamsuata bila mtu kuandika kitabu kingine
Miaka 23 Kleist na mwanae Abdul Sykes hawakuwa na wazo la kuandika katiba
Wazo amekuja nalo Nyerere. Ndio maana Mohamed hajibu hoja za nani aliandika katiba
Hataki kumsikia Nyerere mtu anayemchukia sana katika dunia hii
Mohamed anasema hotuba ya Nyerere UN iliandikwa na kamati ya watu watano.
Katika hao Mohamed hamtaji Nyerere aki back date kuandikwa kwake.
Historia inamshataki Mohamed, kama hotuba iliandikwa kabla ya Nyerere ni nani aliyetarajiwa kwenda UN?
Historia inasema kama kamati iliandika hotuba, kulikuwa na tatizo gani ikiwa lilikuwa suala la chama?
Kuna shida gani chama kuandika hotuba kubwa kama ya UN na kumkabidhi mhusika!
Mohamed anaingiza hoja kuonyesha Nyerere alisoma tu bila kujua maudhui ili kumdhalilisha.
Historia inamtetea Nyerere. Wakati hotuba inaandikwa yeye ni mmoja wa watu wachache sana waliokuwa na degree katika kiwango cha Master. Alishakuwa exposed katik siasa za dunia
Mohamed anaweza kumdhalilisha Nyerere atakavyo, wanaosoma kwa critical thinking watakuwa na rafiki yao mmoja anayeitwa Historia atakayewasaidia kuchambua chuki na ukweli