Mzee Muta alivyomfunga miguu Saida Karoli

Mzee Muta alivyomfunga miguu Saida Karoli

dah hilo swala limeniumiza sana jana kwa kweli, yn inamana saida hana haki kwny kazi zilizotengenezwa na kipaji chake, sijui mkataba wao ulikaaje kaaje mi sijaelewa kabsa.
Ni Quruani Biblia tu ndio haiwezi kuvadilika. Hapa ndio haki za bibadamu wanatakiwa kuingilia badala ya kimchangia mtukana Rais!
 
Duh!!!mambo mazito haya,,kumbe shule inahitajaka sana bongo..kwamaana hiyo ndo imeshakula kwake na hakuna wakutengua??mfano akikata rufaa ya kuukataa mkataba inawezekana?..
Yes, Saida Karoli anaweza kufanya attempts zozote za kisheria kuuvunja au kuupitia upya(Review) huo mkataba. Milango hiyo ipo wazi. Japokuwa ni gharama na pia ni pata potea kama Mzee Muta alilifanya hilo kwa weredi mkubwa(Which I think so, kutoka na kariba yake!)
 
'Ukipewa Kipaji lakini ukakosa Akili, kitakachotokea ni kutumikishwa tu'

Hicho ndicho kimemkuta Saida Karoli. Hakuna wa kumlaumu, wakujilaumu ni Saida Karoli mwenyewe.

Muta ni mtu mwenye Upeo na Akili, alikuwa anajua anachokifanya wakati ule akitumia muda na rasilimali zake ili kumtoa kimuziki Saida Karoli. Bahati mbaya sana Saida Karoli hakutaka kujua matokea ya Athari za kisheria katika mkataba wake na FM Studio(Muta) wakati ule.
Kilichomkuta Saida Karoli kimewahi kuwakuta pia Nakaaya(katika mkataba na Sonny), The Comedy (Katika mkataba na EATV), Hadija Kopa(Katika mkataba na TOT). Na ndicho hicho hicho huenda kikaja kuwakuta Ya moto Band(Katika mkataba wao na Saidi Fella), Dogo Janja(Na Tip Top Connection), Harmonize, Raymond, nk(Katika mkataba wao na Wasafi Classic..)

Ushauri:
Kwa sasa Saida Karoli akubali tu kuwa alikosea na ujinga wake umemgharimu. Tukio hilo alione kama ni darasa kwake na kwa wasanii wengine katika mambo ya mikataba.
Je anatokaje apo, tunatakiwa kumsaidia na sio, kumponda maana maswala ya kisheria sio wote tunayajua kwa asilimia zote
 
ndio maana huwa nawakubali sana watoto wa A town,wao wanaona ni bora kuuzia album kwenye rasket hata ukipata wateja watano hainanoma,kuliko kuwa chini,alafu chini ya rofa mwenzio,Saida anapakwa mchuzi uliotiwa maji,supu na nyama ya kweli wamekula wajanja
 
Haya mambo ya mikataba yanawagharimu watu wengine sana kwenye jamii, hususani watu walioajiriwa, wasanii na wataalamu. Ni issue inayotokea dunia nzima.
Bahati mbaya sana, wahanga wanakuja kugundua mikataba inawanyonya huko baadaye kabisa tena baada ya mambo yao kwenda Kombo na kukosa pa kushirikia.

Pole sana Saida Karoli.
 
Je anatokaje apo, tunatakiwa kumsaidia na sio, kumponda maana maswala ya kisheria sio wote tunayajua kwa asilimia zote
Ushauri pekee wa kumsaidia Saida Karoli ni huu.
1/Akubali kwanza kuwa alikosea mwenyewe.
2/Aache kulalamika ovyo kwenye mitandao.
3/Aende Kwa Muta na Kumshawishi ule mkataba upitiwe Upya ili uwe na maslahi mapana kwa pande zote(Na kama ikishindikana basi achukue hatua ifuatayo..)
4/Atafute wataalamu wa sheria za mikataba ili afungue shauri kwenye Vyombo husika(kama mahakamani, BASATA, COSOTA, Wizarani nk)
 
Ukishakuwa chini ya record label hayo ya Saida yanatokea sana! Wewe kama msanii unakuwa huna mchango wowote kwenye utengenezaji kazi zaidi ya talent yako ya uimbaji na labda uandishi na kutengeneza melody! Kinyume chake, unakuta label ndiyo inakugharamia wewe kwa kila kitu... kuanzia na kazi zako hadi maisha yanayoambatana na kazi zako! Unakua "hujui" hata gharama ya kurekodi wimbo wala gharama ya kufanya video! Inakuwa hujui gharama ya mavazi ya kazi wala gharama za hotel unapoenda kufanya show!!!

Kutokana na hilo na ukikosa entertainment lawyer, kuna uwezekano mkubwa sana kazi unazofanya zisiwe mali yako bali zitakuwa copyrighted kwa kampuni uliyopo! Hili likitokea, haki zako zinaweza ku-include % ya mauzo ya album, shows, singles n.k! Hata kama mkataba wenu umeshaisha, utakuwa na haki ya kupata mrabaha/royalty inapotokea matumizi ya nyimbo zako kwa namna moja au nyingine... kwa mfano, kv Diamond ame-sample Salome, yeye kama yeye amemlipa mwenye hati miliki lakini Saida nae anastahili kupata % ya malipo yaliyofanyika! And for what I know, Saida amepata 25% wakati Mzee Mutta kakomba kilichobaki!!!

Anyway, nilichosema sio standard bali hiyo ni moja ya aina za contracts unapokuwa chini ya label!

Ubaya mkubwa zaidi wa mikataba ya aina hii ni pale wakati unaingia msanii unaweza kudhani umelamba dume manake kila utakachotaka, utapewa tu! Utahudumiwa kwa kila kitu huku ukidhani unapewa bure kumbe wenzako wanaweka kumbukumbu kwa kila kitu! Hapa ndipo huwa inaanza migogoro mingi kati ya wasanii na mabosi wao! Siku ya siku album imenunuliwa au umepiga show ya pesa ndefu, unakuta jamaa anakata hadi pesa ulizokuwa unakunywa soda! Mwisho wa siku unakuta unapiga mark time tu cuz' baada ya gharama zote kutolewa, mgao wako unakuta imebaki pesa mboga tu!!!
Sasa saida wa watu hayo mambo enzi hizo angeyajulia wapi, ukizingatia elimu yenyewe ndio vile tena!! Hadi huruma.
 
ndio maana huwa nawakubali sana watoto wa A town,wao wanaona ni bora kuuzia album kwenye rasket hata ukipata wateja watano hainanoma,kuliko kuwa chini,alafu chini ya rofa mwenzio,Saida anapakwa mchuzi uliotiwa maji,supu na nyama ya kweli wamekula wajanja
Akuna cha A-Town wala wapi? Mikataba aiangalii upuuzi wa A-Town wala wapi. Yoyote anapigwa uwe popote mbona kuna wasanii kibao wanapelekwa pelekwa katika matamasha ya Fiesta. Wanapewa mikataba ya kijinga na wanakubali ili mradi wasikose icho kidogo
Mfano mzuri awo Weusi wanapewa pesa ya kawaida na wanaimba katika Fiesta na Niki wa pili ni msomi ulaghai upo kila kona inategemea una njaa ya kiasi gani
Awo Mapacha wenyewe walisanda kwa awo clouds media.

Haya mambo ya mikataba yanategemea yamekukuta na njaa ipi?
 
Sasa saida wa watu hayo mambo enzi hizo angeyajulia wapi, ukizingatia elimu yenyewe ndio vile tena!! Hadi huruma.
Yaani haya mambo ni zaidi ya kuwa na elimu!! Unaweza kuwa na elimu na bado ukadhulumika vile vile ingawaje udhulumikaje wake utakuwa ni tofauti na ule wa wenzangu mimi! Na ndio maana wenzetu lazima wahusishe Wanasheria... na sio ili mradi Mwanasheria tu bali entertainment lawyer vinginevyo unaweza kupoteza haki zako bila kutarajia! Kuna makorokoro mengi sana yanayohusiana na masuala ya hatimiliki ambayo mwanasheria wa kawaida anaweza asiyajue au akayajua juu juu na matokeo yake akashindwa kukupatia kile ambacho ulistahili kupata!
 
Akuna cha A-Town wala wapi? Mikataba aiangalii upuuzi wa A-Town wala wapi. Yoyote anapigwa uwe popote mbona kuna wasanii kibao wanapelekwa pelekwa katika matamasha ya Fiesta. Wanapewa mikataba ya kijinga na wanakubali ili mradi wasikose icho kidogo
Mfano mzuri awo Weusi wanapewa pesa ya kawaida na wanaimba katika Fiesta na Niki wa pili ni msomi ulaghai upo kila kona inategemea una njaa ya kiasi gani
Awo Mapacha wenyewe walisanda kwa awo clouds media.

Haya mambo ya mikataba yanategemea yamekukuta na njaa ipi?
Sijakataa,ila fuatilia wasanii wa zamani wa Atown walianza vipi kujitegemea ki muziki hasa masula ya production na distribution,kitu kilichowapa heshima mpaka leo,achana na akina Nick watoto wa juzi,wapo akina Xplastaz na wengine,hii ili create awareness sana kwa wanamziki wa chuga,kwa mshabiki wa juziwa mziki hawez kunielewa,njaa zipo na ujeuri wa mwenye njaa upo pia
 
Ushauri pekee wa kumsaidia Saida Karoli ni huu.
1/Akubali kwanza kuwa alikosea mwenyewe.
2/Aache kulalamika ovyo kwenye mitandao.
3/Aende Kwa Muta na Kumshawishi ule mkataba upitiwe Upya ili uwe na maslahi mapana kwa pande zote(Na kama ikishindikana basi achukue hatua ifuatayo..)
4/Atafute wataalamu wa sheria za mikataba ili afungue shauri kwenye Vyombo husika(kama mahakamani, BASATA, COSOTA, Wizarani nk)
Good
Maana watu wengi wanakuwa waanga kwa kukosa kujua sheria na wakati mwingine maisha magumu yanafanya mtu aingie katika haya mambo.
Mfano mzuri unaitwa England unapewa mkataba na kushawishiwa kutia saini ya mkataba mwisho wa siku. Unakuwa ushaingiza watu wengi katika majanga na ndio yanawakuta wengi hata awa wasanii wakubwa wa ulaya na wenyewe inawakuta hiyo
 
Akuna cha A-Town wala wapi? Mikataba aiangalii upuuzi wa A-Town wala wapi. Yoyote anapigwa uwe popote mbona kuna wasanii kibao wanapelekwa pelekwa katika matamasha ya Fiesta. Wanapewa mikataba ya kijinga na wanakubali ili mradi wasikose icho kidogo
Mfano mzuri awo Weusi wanapewa pesa ya kawaida na wanaimba katika Fiesta na Niki wa pili ni msomi ulaghai upo kila kona inategemea una njaa ya kiasi gani
Awo Mapacha wenyewe walisanda kwa awo clouds media.

Haya mambo ya mikataba yanategemea yamekukuta na njaa ipi?
Nini weusi, hata mbele wasanii wanapigwa sana! Hadi akina Jiggar hadi wanakuwa akina Jiggar, washapigwa sana huko walikotoka!!! Hadi akina 50 Cents leo hii wanakuwa executive producers wa show kubwa kama Power, wamekula vitasa sana humu njiani!!! Hata kama sina ushahidi lakini naweza kusema with confidence kwamba hakuna msanii duniaani ambae hajapigwa sana kwenye safari yake ya muziki!! Na wakati mwingine wala sio kwa sababu ya njaa... wengi wanavyotafuta kutoka wanakuwa tayari kwa lolote lile!
 
Wasanii wabadilike sasa.. washtuke ..wajarib kuwatumia wanasheria wapo kibao mtaani hawana kazi... mutta hajafanya fair.. jasho la mtu haliliwi lazima imtokee puani..
 
Ishu ya copyright hiyo!
Kwa kidogo nnachofahamu kuhusu haki miliki ni kwamba kuna wasanii wengine hua wanauza hakimiliki zao. Hawa maproducer mda mwingine wanawatapeli sana wasanii ndo mana wasanii wengi wanaishia pasipojulikana.
Unakuta mwanamziki anapewa range rover tu na vishillingi basi anaona katoka wakati mtu aliemkabidhi kazi anaingiza zaidi ya hapo. Hii nchi utaratibu wa kulinda haki za wasanii ni mbovu na wanaoingilia fani kwa pupa wanaishia kuumizwa tu.
 
Asanteni kwa mchanganuo wenu wa hoja hii. Ukitaka kujua kwa undani malalamiko ya wasanii naomba pata muda wa kusikiliza mashairi ya Solo Thang katika wimbo wa "MTAZAMO" wa Afande Sele/Prof. Jay, na wimbo wake mwenyewe Solo Thang wa "KILIO CHANGU". Afande Sele kwenye wimbo wake wa "Karata Dume" kagusia suala la kahimiliki, ingawa anaogopa kuwataja wahusika. Suma G pia kuna wimbo wake mmoja kalalamikia kupewa laki kwenye mauzo ya milioni!
*****************************************************

Kuna wakati nilikuwa nasikiliza redio moja maarufu ya kwa vijana hapa mjini, producer wa AY na Mwana FA bwana Hermy B aliliongelea kwa undani sana suala la copyright (hakimiliki). Kwa aina ya umbumbumbu walio nao wasanii wetu, si rahisi sana kukwepa maswaibu kama ya dada Saida. Hermy B alisema kwamba, kwa kila kazi inayotoka studio kwake, yeye lazima achukue asilimia fulani (hakuweka wazi ni % ngapi anachukua) kila kazi ya msanii aliyemrekodi inapotumika popote pale, iwe kwenye show, matangazo ya redio, tv ama magazetini.

Hapo bado meneja wa msanii nae hajachukua mgao wake. Hii ina maana kwamba, kama msanii ana kipaji na hana pesa za kumrekodi, studio nyingi wako tayari kumrekodia na kumtafutia meneja wa kumsambazia kazi zake, provided atasaini mkataba wa kuachia haki za kazi zake zimilikiwe na hao wanaomtoa, Nadhani hata ugomvi wa Hermy B dhidi ya AY na FA ulitokana na vipengele hivi kandamizi. Huenda hata ile kesi ya Tigo dhidi ya Mwana FA/AY kuna mtu aluchukua mgao wa zile ringtones bila wahusika FA na AY kupewa chochote.

Kuna haja kwa washauri wa kisheria kupitia upya mikataba kandamizi ya wasanii wetu ili angalau waishi kutokana na jasho lao, na si jasho lao kufaidisha mameneja wao ama ma-producer wao. Ugomvi wa Muumini Mwinjuma/Ally Choki na African Stars Band una harufu za masuala hayahaya ya hakimiliki. Ally Choki/Muumini anakuwa mwajiriwa wa African Stars Band na kulipwa pesa kulingana na show, ingawa Asha Baraka mmiliki wa bendi hajaimba wala kupiga kinanda.

Mwisho wa siku album zinamilikiwa na ASET. Ndicho kilichotokea kwa Marehemu Banza Stone, nae kapitia bendi hii na kuishia TOT, nadhani mpaka kifo kinamkuta alikuwa fukara wa kutosha tu, hata pesa za kununulia dawa mpaka watu wapitishe bakuli. Mauzo ya album za TOT na Twanga Pepeta hayakumsaidia kwa sababu yalichukuliwa na wamiliki, ingawa nyimbo katunga yeye. Kwa maana hii, Choki na wenzie wasipojiongeza basi wataishia kulipwa mishahara huku album walizoimba tangu 2000 zikiwa zinauzwa sokoni na mauzo yanaenda ASET, ihali walioimba wanaishi kuwa maskini.

Nini kifanyike?
  1. Wasanii wana umoja HEWA ambao unawasaidia kwenye kuzikana tu, wajiongeze na kutafuta mwanasheria wa kuwasaidia ku negotiate mikataba yao.
  2. Wasanii hawapendani kabisa, hata ukisikia nyimbo zao wanatukanana sana. Waamke na kupambana na wanyonyaji wao pale inapobidi, sio lazima wafanikiwe wao, hata watoto wao wanaweza kufaidika huko mbeleni.
Samahani kwa kuandika gazeti refu, ila nimejifunza mengi sana
 
Asanteni
Nini kifanyike?
  1. Wasanii wana umoja HEWA ambao unawasaidia kwenye kuzikana tu, wajiongeze na kutafuta mwanasheria wa kuwasaidia ku negotiate mikataba yao.
  2. Wasanii hawapendani kabisa, hata ukisikia nyimbo zao wanatukanana sana. Waamke na kupambana na wanyonyaji wao pale inapobidi, sio lazima wafanikiwe wao


  1. Mkuu gazeti ni refu sana lakini nime kusoma uko sahihi asilimia 100000000000
 
Back
Top Bottom