Mzee Mwinyi alikuwa na nafasi ya kuwa Baba wa Taifa wa pili baada ya Nyerere ila maboko yake yalimkosesha hadhi hiyo

Watoto wa generation hii hamuwezi kujua mchango wa Mzee Mwinyi katika nchi ya Tanzania, Sisi ndio tunajua, chuki zako dhidi ya rais wa sasa usizitumie kumchafua mzee wetu,
Kaa na wazazi wako wakupe historia ya nchi yako vizuri.
 
wajumbe wa 1985 walimpa urais Mwinyi ili tu kuififisha nyota ya mwanadiplomasia na kipenzi cha Mwalimu - Salim Ahmed Salim - ambaye nyota yake ilionekana kuwafunika makada na magwiji wote chamani.

apart from that, Mwinyi wasn't, has never been and will never ever be presidential material.
 
Nyerere alikuwa na akili ila akishindwa kutumia akili zake kipindi cha mwisho kuwa na maono juu ya uelekeo wa dunia kutoka ujamaa kwenda ubepari. Kiburi chake ndio kimesababisha hadi sasa tupo nyuma kimaendeleo.
Kenya walifuata ubepari sasa hivi ardhi yao inashikiliwa na wachache. Katika vitu vya kujivunia ni ardhi tuliyonayo ambayo ni sera za Nyerere.

Wangeboresha tu kama kutafuta wawekezaji wenye uzoefu wa kilimo kufanya kilimo cha biashara kwenye mashamba ya mkonge ambayo yangezalisha ajira kama ilivyokuwa enzi za ukoloni.
 
Kwa tuliokuwepo Mwinyi alipokuwa rais, ilikuwa kichekesho! Alikuwa na upeo na ufahamu mdogo sana..

Alikuwa anaweza kuamua kumsamehe mfungwa wa ufisadi aliefungwa na akatoa sababu eti " mama wa fisadi alimfuata amalia sana mbele yake akamwonea huruma"
 
Kwa kweli mzee Mwinyi is a joker!
Ndiyo ana busara ya uzee lakini kwenye strategic thinking mzee hayupo na ni kweli he is a personally interested party katika kumsupport Magufuli na kutotaka kuudhi au kumsahihisha kwa lolote.
Cath ni ueair wa mtoto wake kule Zanzibar.
Pili kwa kuwa ni Mzanzibari, hataki kujihusisha na the general picture ya kitaifa, hilo ni dosari.
Mwisho kwa upeo wa kuwa "Baba wa Taifa, no. 2" he is a liability.
 
Hapa umemaliza kabisa!
Mwinyi ilikuwa hamna kitu kabisa...
 
Nyerere alikuwa na akili ila akishindwa kutumia akili zake kipindi cha mwisho kuwa na maono juu ya uelekeo wa dunia kutoka ujamaa kwenda ubepari. Kiburi chake ndio kimesababisha hadi sasa tupo nyuma kimaendeleo.
Nakufananisha na mtoto wa maskini anayelalamika baba yake ndiye kamfanya maskini.

Kwa mtazamo wako upo sahihi kabisa.....ila pia kuna nchi zilikuwa za kijamaa zinafanya vizuri lakini pia tunazo nchi ambazo hazijawahi kuwa tulipokuwa ila bado ni maskini.

Nyerere ni binadamu alifanya alipo paweza tuliobaki tufanye tunayoweza. Kufeli au kutokutufelisha ni mtazamo unaoweza kutazamika kwa namn mbalimbali.
 
Alishawahi kusema kwamba gari limepoteza muelekeo na maji yamekorogeka!! Naona watu wakamshauri atulie aanze kusifia.
 
Watoto wa generation hii hamuwezi kujua mchango wa Mzee Mwinyi katika ya Tanzania, Sisi ndio tunajua, chuki zako dhidi ya rais wa sasa usizitumie kumchafua mzee wetu,
Kaa na wazazi wake wakupe historia ya nchi yako vizuri.

Ulinionjesha kidogo tu ukanichinjia baharini
 
Huyo Nyerere nchi ilimshinda akang'atuka nchi hii ilieijenga mifumo ya sasa ni Mwinyi, ndie baba wa taifa hili, lile la Nyerere lilikufa la ujamaa na Mwinyi ndio akaanzisha hii mifumo, lakini kama kawaida aliekufa ndie mzuri. Lakini mumesahau Mwinyi alitutoa wapi na nchi ilikuwa wapi
 
Wewe una sifa hizo? Magufuli anazo? Ingawa sikuwa na umri mkubwa wa kutambua nn Mwinyi amefanya ila ni yeye ambaye alileta mwanga katika nchi hii ambapo sasa Bidhaa muhimu zikawa zinapatikana, angalau sasa mishahra ikaanza kupanda taratibu. Vitu vingi vilikuja kwenye utawala wake
 
We unaona huruma ni sababu DHAIFU? Huo ni moyo wa mtu.. ROHO mbaya si ya kujivunia
 
Mwinyi huyu anayejikomba kwa Jiwe ?

Kuna dogo aliwahi kumtandika Kofi mzee Mwinyi yule dogo alikuwa sahihi sana
 
Unakumbuka jina la aliyempiga kibao?

Ingawa niliona kwenye tv hata sura sikumbuki nakumbuka jamaa alikua na baraghashia ila vazi sikumbuki kama ilikua kanzu ya hughurungi au shati jeupe na suruali nyeusi
Aliitwa Ibrahim Said ama Said Ibrahi, kama sijapoteza kumbukumbu
 
Ndio nakuuliza sasa "aliyempiga ni nani" maana mimi sijawahi kusikia hii habari isipokuwa ya Warioba
 
Jana kwenye hotuba yake nilipatwa na mshangao, alimsifia sana mkapa kwa kukuza sana uchumi, then akaja kumsifia Magufuli kwa kuipeleka nchi mbele kwamba aliitoa nchi kubaya. Hii inamaanisha yeye Mwinyi na Kikwete waliiharibu nchi au sio?
Uzee umemnogea.
 
MWINYI LIMEBAKI JINA TU NA UMBO. MTU ALIYEFIKIA NGAZI YA KUWA RAIS WA NCHI AKAAPA KUILINDA KATIBA, LEO ANASIMAMA MBELE YA DUNIA HADHARANI KUPENDEKEZA KATIBA IVUNJWE KIENYEJI ETI HILI DUDU LIENDELEE KUTUBURUZA! NTUMELICHOKA!
 
Ni Wapi Mzee mwinyi alitamani "katiba ivunjwe" ili Magu aendelee???
WEWE NI MTANZANIA? ULIFUATILIA HOTUBA YA HUYO MZEE JUZI KWENYE MKUTANO WA CCM DODOMA KUMCHAGUA RAIS WA ZANZIBAR NA KUMPITISHA M JIWE KUWA MGOMBEA URAIS KUPITIA CCM? KAMA HUJUI JAMBO USIJIDHALILISHE HADHARANI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…