Mzee Pius Msekwa haifahamu historia ya TANU

Mzee Pius Msekwa haifahamu historia ya TANU

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MZEE PIUS MSEKWA HAIFAHAMU HISTORIA YA TANU

Katika gazeti la Tazama la leo tarehe 14 Oktoba 2019 kuna makala iliyoandikwa na Pius Msekwa yenye kichwa cha habari, ‘’Mwalimu Nyerere kama nilivyomfahamu (2),’’ ambamo ameandika maneno haya yafuatayo kuhusu Mwalimu Nyerere kuwa:

‘’...alifanikiwa kuwaridhisha kwa nguvu za hoja zake, wanachama wa iliyokuwa asasi ya kupigania maslahi ya wafanyakazi wa Kiafrika katika Serikali ya Kikoloni, iliyokuwa inaitwa ‘’Tanganyika African Association’’ (TAA).

Alifanikiwa kuwashawishi wanachama wa asasi hiyo kukubali wenyewe kuvunja chama chao hicho, na badala yake kuunda chama kipya cha siasa cha, ‘’Tanganyika African National Union (TANU), mnamo mwezi Julai, 1954, ili kiwe chombo cha kisiasa cha kupigania uhuru wa Tanganyika.’’

Mzee Pius Msekwa amekosea hii si historia ya kweli ya TANU na kwa bahati mbaya Mzee Msekwa hakutaja majina ya hao walioshawishiwa na Nyerere, ‘’ kuvunja chama chao.’’

TAA hakikuwa chama cha kupigania maslahi ya wafanyakazi wa Kiafrika katika serikali ya kikoloni.

TAA kilikuwa chama cha Waafrika kikipigania maslahi zaidi ya hayo ya wafanyakazi na kilifika wakati kikawa kinakidhi mahitaji ya Waafrika wa Tanganyika kama chama cha siasa kisichokuwa na katiba ya siasa na kwa ajili hii kikawa kinagongana na serikali ya kikoloni TAA ikishutumiwa kuwa ilikuwa inajihusisha na siasa dhahiri.

Gavana Twining alipata kutoa Government Circular kadhaa kuionya TAA kati ya mwaka wa 1951 hadi 1953 kuhusu kujihusisha na siasa.

Mzee Msekwa anaweza kuanza kuisoma historia ya African Association kutoka kwa kalamu ya mmoja wa waasisi wa chama hicho Kleist Sykes aliyoiandika kabla ya kufariki mwaka wa 1949 na mswada huu ukawa mikononi kwa mwanae Abdulwahid Sykes hadi mwaka wa 1968 pale bint yake, Daisy alipoutoa hadharani akiwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki, Dar es Salaam kama mada katika semina ya Idara ya Historia ya chuo hicho.

Wakati huo Daisy alikuwa mwanafunzi chini ya mwalimu bingwa wa historia ya Tanganyika, John Iliffe.

Matokeo ya mada hii ni sura katika kitabu alichohariri John Iliffe, (Daisy Sykes Buruku, ‘’The Townsman: Kleist Sykes’’ Moderm Tanzanians, Nairobi 1973, pp 95 – 114).

Laiti angesoma kitabu hiki Mzee Msekwa angeijua historia ya si tu TAA na TANU pia.

Hakuna popote katika sura hii ambamo imeelezwa kuwa TAA kilikuwa chama kinachopigania maslahi ya wafanyakazi wa serikali ya kikoloni.

Katika kitabu hiki anaweza pia kusoma maisha ya Hassan Suleiman na Ali Juma Ponda.

Hawa walikuwa viongozi wa TAA (''The Politicians Ali Ponda and Hassan Suleiman,'' pp. 227 – 253) na hakuna popote viongozi hawa walishughulika na maslahi ya wafanyakazi wa serikali wakiwa viongozi wa TAA.

Ningependa kuhitimisha nukta hii kwa kumfahamisha Mzee Msekwa kuwa huyu Abdul Sykes niliyemtaja hapa ni mtoto wa Kleist Sykes na ndiye baba yake Daisy alikuwa kiongozi wa TAA 1950 na ni mmoja wa wale wazalendo 17 walioasisi TANU mwaka wa 1954 na imesadifu kuwa nimeandika kitabu cha maisha yake, ‘’The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 – 1954) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,’’ Minerva Press, London 1998.

Mzee Msekwa akipenda anaweza kuisoma historia ya TANU kutoka kwa wenyewe waliounda African Association 1929 na wakaja kuunda TANU 1954 kutoka TAA Abdul akiwa na mdogo wake Ally, Julius Nyerere, Dossa Aziz, John Rupia na wazalendo wengine kutoka katika majimbo ya Tanganyika kama Japhet Kirilo, Joseph Kimalando, Saadan Abdu Kandoro kwa kuwataja wachache.

Kuwa Nyerere ndiye aliyewashawishi wazalendo hawa kuunda TANU hii si kweli.

Ikiwa utasoma kitabu cha maisha ya Abdul Sykes utaona mle mabadiliko yaliyotokea ndani ya TAA kuanzia mwaka wa 1950 baada ya Mwalimu Thomas Plantan kama Rais wa TAA na Katibu wake Clement Mtamila kuondolewa madarakani kwa mapinduzi na uongozi wa TAA ukachukuliwa na Dr. Vedasto Kyaruzi kama Rais na Abdul Sykes Katibu.

Abdul Sykes alikuwa na fikra ya kuunda chama cha siasa toka yuko Burma wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia (1939 – 1945) na alipoingia katika uongozi wa TAA na kuwa mjumbe katika TAA Political Subcommitee ambao wajumbe wengine walikuwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Churembo, Steven Mhando na John Rupia na nia ya kuunda hii kamati ikiwa kuunda chama cha siasa.

Itamshangaza mtu yoyote kusikia kuwa Nyerere aliyepokelewa ndani ya TAA na Abdul Sykes 1952 tena wakati huo Abdul akiwa Kaimu Rais na Katibu TAA, iwe Nyerere ndiye aliyemshawishi Abdul na wenzake katika uongozi wa TAA ati wavunje TAA waunde TANU.

Mzee Msekwa anazungumza historia ambayo yeye haijui.

Ukweli ni kuwa kulikuwa na mazungumzo kabla na nyuma sana kati ya Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kuhusu kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Abdul alishaanza mazungumzo na Chief Kidaha Makwaia achaguliwe Rais wa TAA na mwaka unaofuatia TANU iundwe na Chief Kidaha aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Kuna mengi hapa hadi Nyerere akaja kuchaguliwa kuwa Rais wa TAA mwaka wa 1953 na Abdul Sykes akawa makamu wake katika uchaguzi uliofanyika Ukumbi wa Arnautoglo.

Kikao cha kumpa Nyerere uongozi wa TAA kilifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu, Nansio Ukerewe katika miezi ya mwanzoni 1953 kati ya mwenyeji Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na Ally Mwinyi Tambwe aliyekuwa Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) chama ambacho aliasisi baba yake Abdul mwaka wa 1933 na chama hiki ndicho kilichotoa wanachama na viongozi wa mwanzo wa TANU mwaka wa 1954.

Kwa kumalizia ningependa kumweleza Mzee Msekwa ni chama gani kilikuwa kinashughulika na maslahi ya wafanyakazi Waafrika katika serikali ya kikoloni.

Chama hiki hakikuwa TAA.

Chama kilichoshughulika na maslahi ya wafanyakazi Waafrika kilikuwa kinaitwa, ''Tanganyika African Government Servant Association (TAGSA).''

Chama hicho kiliasisiwa mwaka wa 1927 kwa lengo la kuendeleza maelewano mazuri baina ya serikali ya Malkia na watumishi wake Waafrika ili kuboresha huduma na kuendeleza maslahi na ustawi wa waajiriwa Waafrika.

Katika kipindi hiki cha mwanzoni mwa mwaka wa 1950 viongozi wa TAGSA walikuwa Thomas Marealle kama Rais na Ally Sykes Katibu.

Rashid Kawawa, Dr. Wibard Mwanjisi, Steven Mhando, Dr. Michael Lugazi walikuwa wanakamati na hawa wote walihusika sana katika kuunda TANU na wakiishi na fikra ya kuunda chama cha siasa kudai uhuru wa Tanganyika wala hawajasikia jina la Julius Nyerere.

Huu ndiyo ukweli wa historia ya TANU.
CHIEF KIDAHA.jpg
HAMZA MWAPACHU NA ABDUL SYKES.png
GAZETI LA TAZAMA MSEKWA.jpg
 
Ndo hivyo ishatokea,kijana ametoka zake kijijini huko Butiama akapindua meza watoto wa mjini(Saigoni) wakabaki wanalia lia tu huku ndoto yao ya kulifanya taifa liwe kiislam zikishindikana.
Mng'ato,
Mjadala huu si mjadala wa lugha kama hiyo yako, "kupindua meza," huu ni mjadala wa heshima si wa kihuni wa kurushiana kejeli.

Naandika historia hii nikiwa mjukuu wa wazee wetu waliounda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wala mjadala huu hauna uhusiano wowote na Saigon.

Sasa ikiwa una elimu ya historia ya TANU tujadiliane la huna itakuwa busara ukawa kimya.
Nimelinyamzia hili la Uislam kwa makusudi kwa kutambua kuwa huna unachokijua.
 
Mng'ato,
Mjadala huu si mjadala wa lugha kama hiyo yako, "kupindua meza," huu ni mjadala wa heshima si wa kihuni wa kurushiana kejeli.

Naandika historia hii nikiwa mjukuu wa wazee wetu waliounda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wala mjadala huu hauna uhusiano wowote na Saigon.

Sasa ikiwa una elimu ya historia ya TANU tujadiliane la huna itakuwa busara ukawa kimya.
Nimelinyamzia hili la Uislam kwa makusudi kwa kutambua kuwa huna unachokijua.
Lengo la TANU na waasisi wake halikuwa kushindana baina yao kwa wao wala wao dhidi ya Watanganyika wenzao bali kudai uhuru na hatimaye kuishi kwa amani na utulivu kama Watanganyika.Haipendezi watu wazima tena wasomi kuja hapa jukwaani na lugha za kihuni na kuingiza mambo yasiyo na staha.Binafamu hukosea bali kwa muungwana hujutia makosa yake na kujisahihisha.Maalim Said nimekusoma na kusoma kila siku,endelea kutuelimisha mkuu maana wewe ni kisima chetu cha maarifa
 
Lengo la TANU na waasisi wake halikuwa kushindana baina yao kwa wao wala wao dhidi ya Watanganyika wenzao bali kudai uhuru na hatimaye kuishi kwa amani na utulivu kama Watanganyika.Haipendezi watu wazima tena wasomi kuja hapa jukwaani na lugha za kihuni na kuingiza mambo yasiyo na staha.Binafamu hukosea bali kwa muungwana hujutia makosa yake na kujisahihisha.Maalim Said nimekusoma na kusoma kila siku,endelea kutuelimisha mkuu maana wewe ni kisima chetu cha maarifa
Balibaba...
Ahsante sana kaka...
 
Nyerere akaja kuchaguliwa kuwa Rais wa TAA mwaka wa 1953 na Abdul Sykes akawa makamu wake katika uchaguzi uliofanyika Ukumbi wa Arnautoglo.

Kikao cha kumpa Nyerere uongozi wa TAA kilifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu, Nansio Ukerewe

Chaguo moja: Nyerere alipewa uongozi wa TAA na kikao cha nyumbani kwa mtu Nansio, Ukerewe au kwenye uchaguzi wa kura, ukumbi wa Arnautoglo, Dar-es-Salaam ???
 
Taso,
Hilo halina wasiwasi.

Abdul Sykes si tu alishiriki katika kumtia Mwalimu katika uongozi.

Abdul ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam na kumjengea msingi wake wa siasa na alipojiuzulu kazi ya ualimu Mwalimu aliishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuu hadi TANU ilipomtafutia nyumba Magomeni Maduka Sita.

Yako mengi sana yatakushangaza.

Nyumba ya Abdul Sykes ndiyo ilikuwa ngome ya mikakati yote ya mipango ya TANU.
 
Hilo halina wasiwasi.

Abdul Sykes si tu alishiriki katika kumtia Mwalimu katika uongozi.

Abdul ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam na kumjengea msingi wake wa siasa na alipojiuzulu kazi ya ualimu Mwalimu aliishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuu hadi TANU ilipomtafutia nyumba Magomeni Maduka Sita.

Yako mengi sana yatakushangaza.

Nyumba ya Abdul Sykes ndiyo ilikuwa ngome ya mikakati yote ya mipango ya TANU.


That IS NOT what I asked you!

Sijakuuliza nani alimtafutia nyumba Nyerere Magomeni Maduka Sita, sijakuuliza nani alimpokea mjini kutoka kijijini kwao, sijakuuliza aliishi kwa nani. Narudia nilichosema...

Chaguo moja: Nyerere alipewa uongozi wa TAA na kikao cha nyumbani kwa mtu Nansio, Ukerewe au alishinda kwenye uchaguzi wa kura, ukumbi wa Arnautoglo, Dar-es-Salaam ???

Usikwepeshe mada, nyoosha maelezo!
 
That IS NOT what I asked you!

Sijakuuliza nani alimtafutia nyumba Nyerere Magomeni Maduka Sita, sijakuuliza nani alimpokea mjini kutoka kijijini kwao, sijakuuliza aliishi kwa nani. Narudia nilichosema...

Chaguo moja: Nyerere alipewa uongozi wa TAA na kikao cha nyumbani kwa mtu Nansio, Ukerewe au alishinda kwenye uchaguzi wa kura, ukumbi wa Arnautoglo, Dar-es-Salaam ???

Usikwepeshe mada, nyoosha maelezo!
Taso,
Hakuna sababu ya kukasirika kwani hayo niliyokueleza wewe ulikuwa unayajua?
Ajabu sana sijui kwa nini mnachomwa na historia hii.

Mimi nikukwepe wewe kwa lipi ulijualo ilhali uko hapa nakusomesha historia ya Mwalimu, TANU na uhuru wa Tanganyika, historia ambayo imehifadhiwa katika picha na nyaraka sasa inafika miaka 100?

Tuanze na Mwalimu kujadiliwa nyumbani kwa Hamza Kibwana Mwapachu (1913 - 1962):

''Mohamed kuna sehemu katika maelezo yako ambayo kwa kweli ni murua sana ambako katika kuwataja Bwana Abdul na Bwana Mwinyi na suala la Nyerere kupata nafasi ya Urais wa TAA mwaka 1953 ulikuwa utaarifu safari yao kwenda Ukerewe na kufikizia kwa Hamza.

Msingi wa safari ile haukuwa pleasure.

Ulikuwa kujadili uongozi wa TAA.

Usisahau kwamba uongozi wa TAA wakati Abdul akiwa Rais ulizidiwa nguvu na Waislamu.

Hata Mzee Rupia alivutiwa sana na Waislamu.

Mzee Rupia alimpenda Hamza tangu 1945 na kumsaidia ujenzi wa nyumba yake ya kwanza mtaa wa Tabora, Mwanza.

Rupia alikuwa tayari ni contractor wa ujenzi.

Safari ya Ukerewe ilikua kupata mawazo ya Hamza kuhusu mustakabali wa vita ya uhuru na nani aongoze.

Waislamu Dar walimtaka Abdul.

Hamza aliwashauri kumkubali Nyerere na aliwapa sababu nyingi mojawapo ni Ukristo mbali na maarifa yake.

Hamza hakuwa mgombea kwa sababu za kifamilia.

Nakumbuka safari hiyo nikiwa darasa la nne hapo Bukongo Primary school.

Nilisikia mazungumzo yao.

Na kuja kwao ilibidi kaka Bakari na mimi tuhamishwe chumba cha kulala.

Jamani, historia ya TANU bado mbichi.''


Unamjua huyu nani anaeeleza haya?

Sasa nakuchukua Ukumbi wa Arnautoglo tarehe 17 April, 1953:Ukumbi wa Arnautoglo safari ndefu ya Mwalimu Nyerere ilipoanzia

George Arnautoglo alikuwa Mgiriki tajiri na ndiye aliyejenga jumba hilo akalitoa kwa matumizi ya Waafrika wa Tanganyika.

George Arnautoglo alikuwa hawapendi Waingereza kwa kuwa walikuwa wameikalia nchi yake Greece ambako Padri Makarios alikuwa akiongoza mapambano ya kudai uhuru.

Arnautoglo alipata kutoa fedha kwa siri kuwapa TANU zisaidie harakati za kudai uhuru na fedha hizi alimpa Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa mmoja wa viongozi wa juu wa TANU.

Kwenye Ukumbi huu wa Arnautoglo tarehe 17 April 1953 ulifanyika uchaguzi wa mwaka wa TAA kumchagua Rais na viongozi wengine.

Julius Kambarage Nyerere, mwalimu wa shule asiyefahamika sana kutoka Pugu alikuwa anagombea nafasi hiyo dhidi ya kijana maarufu wa Dar es Salaam na Kaimu Rais wa TAA na Katibu wake, mtoto wa mwanasiasa na mfanya biashara maarufu wakati wake, Kleist Sykes, Abdul akiwa Market Master Kariakoo Market.

Nyerere alishinda uchaguzi huu kwa kura chache sana.

Vipi Nyerere aliweza kumshinda Abdul Sykes siku ile ni kisa cha kusisimua katika historia ya Tanganyika na historia ya Mwalimu Nyerere.

Hapa kwenye jengo hili na siku ile ndipo Julius Nyerere alipoanza safari yake ndefu ya siasa na uongozi.

Hapa Nyerere alikuwa siku ile kavuka kiunzi kikubwa katika maisha yake ya siasa.

Meneja wa Ukumbi huu wa Arnautoglo ambae na yeye alishiriki katika kupiga kura ya kunyoosha mikono alikuwa kijana wa Kinyasa kutoka Nyasaland (Malawi) Dennis Pombeah.

Phombeah akiendesha pikipiki yake aina ya BSA alizunguka mji mzima kumfanyia Nyerere kampeni.

Abdul na wenzake katika TAA hawakufanya kampeni yoyote kwani walitaka Nyerere ashinde.

Imenichukua zaidi ya miaka 10 kutafuta picha ya Dennis Phombeah na mwisho nimeipata picha yake.
ARNAUTOGLO HALL.png
DENIS PHOMBEAH 1.jpeg
 
Nyerere alishinda uchaguzi huu kwa kura chache sana.


Abdul na wenzake katika TAA hawakufanya kampeni yoyote kwani walitaka Nyerere ashinde.

Kama Abduli alitaka Nyerere ashinde na hakufanya kampeni kwa nini aligombea?

Acha uongo!

Na kama Nyerere alichaguliwa Mwenyekiti Nansio, Ukerewe, kwa nini walifanya uchaguzi mkali Arnautoglo, Dar-es-Salaam?

Argument zako huwa hazina logic!
 
Ndo hivyo ishatokea,kijana ametoka zake kijijini huko Butiama akapindua meza watoto wa mjini(Saigoni) wakabaki wanalia lia tu huku ndoto yao ya kulifanya taifa liwe kiislam zikishindikana.
Mzee alikua smart by nature afu shule ipo kichwani.. majamaa wao walikua wanaelimu ya madrassa tu. At the end walikuja kujua umuhimu wa elimu ahera na dunia baada ya mzee kuwatoa relini..Si unajua ukiwa na elimu kati ya wasio na elimu unaswaga tu kama kundi la mifugo
 
Kama Abdul alitaka Nyerere ashinde na hakufanya kampeni kwa nini aligombea?

Acha uongo!

Na kama Nyerere alichaguliwa Mwenyekiti Nansio, Ukerewe, kwa nini walifanya uchaguzi mkali Arnautoglo, Dar-es-Salaam?

Argument zako huwa hazina logic!
Taso,
Unazo hoja ambazo mimi nazielewa vizuri na tunaweza tukafanya mjadala kuelimishana mimi nikafaidika na maswali yako nami nitakueleza yale ninayoyajua.

Ninachokusihi ni kuwa tulia hapana haja ya kutoleana maneno yasiyo na heshima huu ni mjadala tu tunajadili yale yaliyopita miaka mingi nyuma hatuko katika ugomvi tukatoleana matusi.

Tuendelee na mjadala.

Mathalan kama Abdul asingegombea maana yake ni kuwa kajitoa katika uongozi wa TAA na Nyerere angebaki peke yake katika chama.

Tambua kuwa Abdul na Dr. Kyaruzi walikichukua chama mwaka wa 1950 kwa mapinduzi na katika kipindi chao walifanya mambo mengi yaliyokipa chama nguvu na heshima kubwa katika jamii ya Waafrika kuanzia mapendekezo ya katiba kwa Gavana Twining 1950 hadi kumsaidia Japhet Kirilo kutoka Meru Citizens Union kwenda UNO kuwakilisha madai ya mgogoro wa Ardhi ya Wameru mwaka wa 1952.

Nyerere hakuwa anafahamika Dar es Salaam kumwacha peke yake katika uongozi wa TAA bila ya Abdul na viongozi wengine waliokuwa katika uongozi toka 1950 TAA ingepata matatizo Nyerere asingeweza kuendesha chama kutoka Pugu.

Ikutoshe tu kuwa baada ya Nyerere kuwa Rais wa TAA 1953 chama kilidhoofika sana kwa wajumbe wa halmashauri kutohudhuria mikutano.

Abdul Sykes akiongozana na Ali Mwinyi Tambwe alikwenda Nansio kupata kauli ya mwisho ya Hamza Mwapachu kuhusu kumtia Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA na uchaguzi ukafanyika Arnautoglo Hall.

Viongozi wa TAA waliochaguliwa katika uchaguzi ule ni hawa:

J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer and Ally K. Sykes as Assistant Treasurer. Committee members were Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo and Patrick Aoko (Tanganyika Standard, 19 th June 1953).

Naelewa hisia zako na wewe si wa kwanza.

Mimi si muongo kama unavyodai hawa watu ni wazee wangu nawajua vyema na nimesoma nyaraka zao zote za nyakati zile na ndiyo zilizoniwezesha kuandika kitabu.

Historia hii inachoma nyoyo za watu wengi kwa kuwa akili zao zinakataa kuamini haya ambayo wanasoma leo.

Tatizo ni kuwa historia iliyokuwa inaenezwa na kusomeshwa Abdul alikuwa hatajiki kama vile hakupata kuwapo katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Huyu mtu kadi yake ya TANU ni no. 3 na no. 2 ni kadi ya mdogo wake Ally na kadi no. 1 ni ya Julius Nyerere na hizi kadi za mwanzo alichapa Ally Sykes kutoka mfukoni kwake.

Kaa ukielewa kitu kimoja Abdul Sykes na Julius Nyerere walikuwa rafiki ndugu.

Kamata hili na mengi yatakuwa wazi kwako na hasira zako zitapungua kama si kutoweka kabisa.

Angalia picha hiyo niko na Dome Budohi Nairobi mwaka wa 1972.
Nimejifunza mengi kutoka kwake.

Budohi mtazame hapo juu ni Mkenya huyu lakini alikuwa katika uongozi wa TAA na kadi yake ya TANU ni no. 6.
DOME BUDOHI NA MOHAMED.jpg
 
Mzee alikua smart by nature afu shule ipo kichwani.. majamaa wao walikua wanaelimu ya madrassa tu. At the end walikuja kujua umuhimu wa elimu ahera na dunia baada ya mzee kuwatoa relini..Si unajua ukiwa na elimu kati ya wasio na elimu unaswaga tu kama kundi la mifugo
Denvers,
Hapana haikuwa hivyo ondoa kejeli jitulize na soma historia ya TANU utaelewa mengi na pengine hicho kiburi na kejeli katika maneno yako kitapungua na ujinga utakutoka.
 
Mzee alikua smart by nature afu shule ipo kichwani.. majamaa wao walikua wanaelimu ya madrassa tu. At the end walikuja kujua umuhimu wa elimu ahera na dunia baada ya mzee kuwatoa relini..Si unajua ukiwa na elimu kati ya wasio na elimu unaswaga tu kama kundi la mifugo
Hahah subiri watakavyokushukia hapa kama mwewe mkuu.
 
Back
Top Bottom