Mzee Pius Msekwa haifahamu historia ya TANU

Mzee Pius Msekwa haifahamu historia ya TANU

Mm ni mmoja wa watu niliokua nabishana nawe kwa jazba lkn taratibu nilielewa na ninaendelea kuelewa.
Asante sana mzee Mohammed Saidi... Naamini siku moja historia ya kweli ya nchi hii itaandikwa upya.
 
Mkuu Mohamed Said, kuna watu wanachuki na Uislamu na hawa watu hata uwaambie nini huwezi kuwaelimisha na huwezi kuondoa chuki zao dhidi ya Uislamu. Usipoteze mda wako kwa watu wa aina hii, hakuna aliyetokea kupendwa na wote hapa Duniani, hata MwenyeziMungu aliyeumba kila kitu anachukiwa na baadhi ya watu. Wewe tumwagie Elimu, atakaye elimika na aelimike na atakae chukia na achukie.
 
Hahah subiri watakavyokushukia hapa kama mwewe mkuu.
Mng'ato,
Hakuna mtu awezae kupinga uwezo wa Mwalimu Nyerere.

Nimemtafiti Mwalimu na nimemsoma katika Nyaraka za Sykes na kusikiliza kumbukumbu za watu waliomjua Nyerere na kwa hakika uwezo wake ulikuwa mkubwa sana.
 
Mkuu Mohamed Said, kuna watu wanachuki na Uislamu na hawa watu hata uwaambie nini huwezi kuwaelimisha na huwezi kuondoa chuki zao dhidi ya Uislamu. Usipoteze mda wako kwa watu wa aina hii, hakuna aliyetokea kupendwa na wote hapa Duniani, hata MwenyeziMungu aliyeumba kila kitu anachukiwa na baadhi ya watu. Wewe tumwagie Elimu, atakaye elimika na aelimike na atakae chukia na achukie.
Daftari ...
Sipotezi muda hapa nasomesha historia ya uhuru wa Tanganyika na watu wanasoma na wananiuliza maswali na nawajibu kadri ya uwezo wangu.

Hizi ni fursa nzuri kwetu sote.
 
Mzee Said haishi vituko.
May Day,
Katika maisha yangu sijapta kuwa kituko popote.
Angalia hapo chini utanifahamu:
  1. PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
  2. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
  3. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
  4. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
  5. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
  6. Uchaguzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
  7. Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No. 1, Ibn Hazm Media Centre, 2019 Dar es Salaam.
  8. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
  9. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
  10. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
  11. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
  12. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
  13. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
  14. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
  15. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
  16. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
  17. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
  18. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
  19. 14. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
  20. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
  21. Awards: Several Awards
  22. Visiting Scholar: (2011)
  23. University of Iowa, Iowa City, USA
  24. Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
  25. Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.
  26. OTHER COUNTRIES VISITED
  27. Zambia, Ethiopia, Great Britain, Swaziland, Msumbiji, Zimbabwe, Zambia, Sudan, Egypt, Saudi Arabia, United Arab Emirates, Oman, Yemen, Uganda, Switzerland, Iran, France, Netherlands, Turkey and Abu Dhabi.
May Day,
Kituko hi wewe huna unalolijua lakini hujui kama hujui.

Imekuchoma kuwa historia ya Tanganyika ya kudai uhuru imefungamana na ukoo wa Sykes?
Je ungependa tuifute historia hii?

Imekuchoma kuwa Kleist Sykes kaingizwa katika Dictionary of African Biography (DAB)?

Imekuumiza kwa kuwa ulisomeshwa histoiria siyo na sasa nakuandikieni historia ya kweli unajihisi ujinga?

Unaumia kuwa huu ni mwaka wa 21 toka nimeandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes na hakuna aliyeweza kuja na kitabu kunipinga?

Unadhani leo hii kuna mtafiti anaweza kuandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika akaacha kuwataja wazee wangu?

Nini hasa kinakuhangaisha ni huu ukweli au ni hasad ya moyo tu?

Baada ya miaka 50 serikali ya Tanzania imemtunuku Abdul Sykes na mdogo wale Ally medali ya Mwenge wa Uhuru.

Jiulize kwa nini hawakuendelea kujifanya hawawajui?
 
Abdul ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam na kumjengea msingi wake wa siasa na alipojiuzulu kazi ya ualimu Mwalimu aliishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuu hadi TANU ilipomtafutia nyumba Magomeni Maduka Sita.
Nimewahi kukuuliza kama unaweza kufahamu nyumba ya Magomeni Mwalimu aliijenga mwaka gani. Japo hujanijibu, naona kama jibu la swali langu lipo hapa. Kumbe ile nyumba hakujenga yeye!
 
Nimewahi kukuuliza kama unaweza kufahamu nyumba ya Magomeni Mwalimu aliijenga mwaka gani. Japo hujanijibu, naona kama jibu la swali langu lipo hapa. Kumbe ile nyumba hakujenga yeye!
Gagnija,
Naona hilo swali limenipita.

Alipotoka kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuu alihamia Magomeni Majumba Sita.

Kisha ndiyo akajenga nyumba hii ya Ifunda ambako sasa ni Maonyesho ya Taifa ila sijui mwaka aliyojenga nyumba hii..
 
Ikutoshe tu kuwa baada ya

Kamata hili na mengi yatakuwa wazi kwako ...
unatumia kejeli halafu unajifanya muungwana, mnafiki sana we mzee... Mtu mstaarabu hatumii lugha za "ikutoshe tu kuwa... kamata hili na mengi yatakuwa wazi..."

"Abdul Sykes akiongozana na Ali Mwinyi Tambwe alikwenda Nansio kupata kauli ya mwisho ya Hamza Mwapachu kuhusu kumtia Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA ..."

You are not making any sense! Kikao cha nyumbani kwa mtu Nansio, Ukerewe, hakikuchagua uongozi wa TANU, kwa nini unapenda kuongea uongo????

Just because umetokea Gerezani, K'Akoo, hiyo haikupi leseni ya kutunga uongo wa historia ya TANU....TANU haikuwa movement ya Kariakoo peke yake, Nyerere is not from Kariakoo, na wewe sio Mtanzania peke yake mwenye roots za Kariakoo!

Abdul Sykes na Hamza Mwapachu walimchagua Nyerere Nansio Ukerewe, kwa hiyo basi Abduli ni mnafiki mkubwa kwa sababu alimchagua Nyerere Ukerewe halafu miezi michache baadae akaja kumpinga kwenye uchaguzi Ilala! What a quirky historian you are!
 
unatumia kejeli halafu unajifanya muungwana, mnafiki sana we mzee... Mtu mstaarabu hatumii lugha za "ikutoshe tu kuwa... kamata hili na mengi yatakuwa wazi..."

"Abdul Sykes akiongozana na Ali Mwinyi Tambwe alikwenda Nansio kupata kauli ya mwisho ya Hamza Mwapachu kuhusu kumtia Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA ..."

You are not making any sense! Kikao cha nyumbani kwa mtu Nansio, Ukerewe, hakikuchagua uongozi wa TANU, kwa nini unapenda kuongea uongo????

Just because umetokea Gerezani, K'Akoo, hiyo haikupi leseni ya kutunga uongo wa historia ya TANU....TANU haikuwa movement ya Kariakoo peke yake, Nyerere is not from Kariakoo, na wewe sio Mtanzania peke yake mwenye roots za Kariakoo!

Abdul Sykes na Hamza Mwapachu walimchagua Nyerere Nansio Ukerewe, kwa hiyo basi Abduli ni mnafiki mkubwa kwa sababu alimchagua Nyerere Ukerewe halafu miezi michache baadae akaja kumpinga kwenye uchaguzi Ilala! What a quirky historian you are!
Taso,
Si lazima uamini haya nielezayo.

Mimi natambua vipi historia hii ilivyobadili historia ya TANU na ya uhuru kusababisha ghadhabu kwa watu wengi.

Muhimu kwangu ni kuwa nimeeleza historia kama ilivyokuwa.

Yapo mengi sana.
 
Mimi natambua vipi historia hii ilivyobadili historia ya TANU na ya uhuru kusababisha ghadhabu kwa watu wengi.

Muhimu kwangu ni kuwa nimeeleza historia kama ilivyokuwa.
"historia hii ilivyobadili historia ya TANU"

Historia ipi ilibadili historia ya TANU ??? Historia ya TANU ilibadili historia ya TANU?

Na ni nani aliyepata ghadhabu kwa sababu ya hiyo historia, mkoloni ???
 
"historia hii ilivyobadili historia ya TANU"

Historia ipi ilibadili historia ya TANU ??? Historia ya TANU ilibadili historia ya TANU?

Na ni nani aliyepata ghadhabu kwa sababu ya hiyo historia, mkoloni ???
Taso,
Ghadhabu inajidhihirisha kwenye kauli na maneno yako makali.

Ghadhabu ni dalili ya kushindwa hoja.
Mwenye hoja akasiriki.

Unauliza historia ipi imebadili historia ya TANU.

Kabla ya kuandika kitabu uliwajua viongozi wa harakati za uhuru kama Hamza Mwapachu na Sheikh Hassan bin Ameir kwa kukutajia najina mawili tu?

Kuna mahali popote ulipatapo kusoma historia zao?

Achilia mbali Abdul Sykes na Chief David Kidaha Makwaia mazungumzo yao kati ya 1950 - 1952 nyumbani kwa Abdul Sykes ya kuunda TANU.

Ulipatapo kusoma popote Chief Kidaha akihusishwa na kuundwa kwa TANU?

Dr. Michael Lugazia je?

Dr. Luciano Tsere, Dr. Joseph Mutahangarwa, Dr. Wilbard Mwanjisi na Dr. Vedasto Kyaruzi?

Vipi kuhusu Schneider Abdillah Plantan?

Mtoto wa Chief Mohosh kutoka Kwa Likunyi, Imhambane Mozambique unajua kama yeye na Hamza Mwapachu na Abdul Sykes ndiyo walioutoa uongozi wa wazee ili kuingiza vijana kudai uhuru?

Aliyetolewa urais wa TAA ni Thomas Saudtz Plantan kaka yake Schneider.

Tuwaache hawa Wazulu.

Mkenya Dome Budohi na Mnyasa Denis Phombea kadi zao za TANU No. 5 na 6.

Ulipata popote kuwasoma popote?

Ulipata kuujua udugu uliokuwapo baina ya Abdul Sykes na Julius Nyerere udugu uliojengeka katika kupigania uhuru wa Tanganyika kiasi Mwalimu baada ya kujiuzulu kazi aliishi nyumbani kwa Abdul?

Hustaajabu?

Ulipata kusoma popote pale kuwa Nyerere alipokelewa na Abdul Sykes na aliwahi kugombea nafasi ya urais wa TAA na Abdul Sykes?

Ulipata hata siku moja kusoma mahali popote kuwa Abdul alikutana na Jomo Kenyatta Nairobi katika mkutano wa siri?

Abdul alikuwa na umri wa miaka 26.

Au ulijua kama Abdul Sykes aliacha nyaraka zinazoeleza historia nzima ya mapambano ya kupambana na ukoloni wa Waingereza?

Ulipatapo popote pale kusikia haya?

Unadhani baada ya mimi kueleza haya yote historia imebakia ile ile?

Kweli, kweli tuifute historia hii yote?

Hii ndiyo faida ya kuzaliwa Gerezani na kuzaliwa katika kipindi kile na kuzaliwa na wazee hawa.

Historia ya babu yangu ndiyo historia yangu simuhitaji Mzee Pius Msekwa anifunze historia yangu na akikosea kuieleza mimi namsahihisha kuwa haikuwa hivyo ilikuwa hivi.
 
Taso,
Hilo halina wasiwasi.

Abdul Sykes si tu alishiriki katika kumtia Mwalimu katika uongozi.

Abdul ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam na kumjengea msingi wake wa siasa na alipojiuzulu kazi ya ualimu Mwalimu aliishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuu hadi TANU ilipomtafutia nyumba Magomeni Maduka Sita.

Yako mengi sana yatakushangaza.

Nyumba ya Abdul Sykes ndiyo ilikuwa ngome ya mikakati yote ya mipango ya TANU.
kwani nini watu kama hawa wamesahaulika hata kwenye hotuba za Nyerer huwa hawataji wenzio mbali na Kawaw tu
 
Back
Top Bottom