Mzee Shamte umenyamazishwa lakini haki ni asili, itadaiwa tu

Mzee Shamte umenyamazishwa lakini haki ni asili, itadaiwa tu

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Haki daima huwa ni ya asili ni vigumu kuzuia isidaiwe. Sheria ya maisha ya binadamu huonesha ukweli huo. Marekani walidhani kuwa kumuua Martin Luther King na Malcolm X watakuwa wamefanikiwa kunyamazisha ujumbe wao.

Likawa ni kosa lililofanywa na CIA, wakaibuka wapigania haki wengine wa miaka ya 1970 na 80 na moto ukawa ni ule ule waliojaribu kuuzima kwa kuwanyima haki ya kuishi wamarekani weusi wawili. Sauti ya haki ni ya Mungu ni vigumu sana kuipoteza, sana sana yanakuwa ni yale mambo ya kumpiga teke chura unachokifanya ni kumuongezea tu mwendo.

Mapambano ya kudai haki huwa na kawaida moja ya ajabu sana. Kwamba yule anayezimwa milele asiweze kusikika hupata mrithi mwenye maarifa na uelewa kumzidi yeye anakuja kuzisumbua mamlaka zile zile zilizodhani zimemaliza kila kitu.

Sauti ya Mzee Shamte huko Unguja na Pemba inaweza kuwa imezimwa na mamlaka zilizoingia madarakani kihalali, ilitaka kujitanua sauti ile ili iweze kuwafumbua macho wenye nchi yao lakini mifumo ikamuwahi mzee wa watu na kwa sasa ni kimyaaaa.

Awamu ya nane huko Zanzibar iliingia uongozini kwa pesa nyingi za waarabu. Mlungula ulitembea haswa kipindi kile cha uchaguzi wa 2020, na waliokuwa wakiutoa ni waarabu. Sasa pesa ina kawaida ya kutaka irudi kwa namna moja au nyingine.

Ukikubali kununulika, lazima kuna siku inakuja inabidi utii kile unachoambiwa na aliyekununua. Ukitabasamu wakati unapokea chochote chenye harufu nzuri lazima kuna siku utatakiwa utoke nje wakati wa jua kali na mamilioni ya macho yakikutazama halafu ukatakiwa kuifanyia kazi ile pesa iliyopewa ndani ya vyumba vyenye viyoyozi vya mahoteli makubwa.

Kuwapa wakodishaji wa ardhi (kama wanavyoitwa) haki ya kukodisha kwa miaka 99 ni suala la hatari sana kwa uhuru mzima wa nchi husika. Na haya maneno ni ujumbe wa Mzee Shamte aliyenyamazishwa na baadae akaja kuombe msamaha.

Tunarudi kule kule katika suala la haki kuwa ni la asili (nature). Nafsi ya Shamte ipo kimya japo sio kwa kupenda mwenyewe, itaibuka nafsi nyingine yenye elimu, busara, upeo na hekima ya kidunia kuliko ile ya Mzee Shamte na itaongea na kuweka kila kitu hadharani. Ndio asili inavyotuambia siku zote.

Alikuwepo hayati Mapalala na mamlaka za nchi zilipomzima akaibuka hayati Mtikila na alipozimwa milele asiweze kuongea tena wamezaliwa kina Fatuma Karume na wanaharakati wengi wanaotumia majukwaa ya kupashana habari katika kuitetea haki wanayoona kama vile mfumo wetu unajaribu kuiminya.

Mzee Shamte kuwa kimya, maana yake wataibuka wengine machachari na wenye uchungu mkubwa zaidi.
 
Huyo alikuwa na impact gani hapa Tanganyika na kule Zanzibar?
 
Haki daima huwa ni ya asili ni vigumu kuzuia isidaiwe. Sheria ya maisha ya binadamu huonesha ukweli huo. Marekani walidhani kuwa kumuua Martin Luther King na Malcolm X watakuwa wamefanikiwa kunyamazisha ujumbe wao.

Likawa ni kosa lililofanywa na CIA, wakaibuka wapigania haki wengine wa miaka ya 1970 na 80 na moto ukawa ni ule ule waliojaribu kuuzima kwa kuwanyima haki ya kuishi wamarekani weusi wawili. Sauti ya haki ni ya Mungu ni vigumu sana kuipoteza, sana sana yanakuwa ni yale mambo ya kumpiga teke chura unachokifanya ni kumuongezea tu mwendo.

Mapambano ya kudai haki huwa na kawaida moja ya ajabu sana. Kwamba yule anayezimwa milele asiweze kusikika hupata mrithi mwenye maarifa na uelewa kumzidi yeye anakuja kuzisumbua mamlaka zile zile zilizodhani zimemaliza kila kitu.

Sauti ya Mzee Shamte huko Unguja na Pemba inaweza kuwa imezimwa na mamlaka zilizoingia madarakani kihalali, ilitaka kujitanua sauti ile ili iweze kuwafumbua macho wenye nchi yao lakini mifumo ikamuwahi mzee wa watu na kwa sasa ni kimyaaaa.

Awamu ya nane huko Zanzibar iliingia uongozini kwa pesa nyingi za waarabu. Mlungula ulitembea haswa kipindi kile cha uchaguzi wa 2020, na waliokuwa wakiutoa ni waarabu. Sasa pesa ina kawaida ya kutaka irudi kwa namna moja au nyingine.

Ukikubali kununulika, lazima kuna siku inakuja inabidi utii kile unachoambiwa na aliyekununua. Ukitabasamu wakati unapokea chochote chenye harufu nzuri lazima kuna siku utatakiwa utoke nje wakati wa jua kali na mamilioni ya macho yakikutazama halafu ukatakiwa kuifanyia kazi ile pesa iliyopewa ndani ya vyumba vyenye viyoyozi vya mahoteli makubwa.

Kuwapa wakodishaji wa ardhi (kama wanavyoitwa) haki ya kukodisha kwa miaka 99 ni suala la hatari sana kwa uhuru mzima wa nchi husika. Na haya maneno ni ujumbe wa Mzee Shamte aliyenyamazishwa na baadae akaja kuombe msamaha.

Tunarudi kule kule katika suala la haki kuwa ni la asili (nature). Nafsi ya Shamte ipo kimya japo sio kwa kupenda mwenyewe, itaibuka nafsi nyingine yenye elimu, busara, upeo na hekima ya kidunia kuliko ile ya Mzee Shamte na itaongea na kuweka kila kitu hadharani. Ndio asili inavyotuambia siku zote.

Alikuwepo hayati Mapalala na mamlaka za nchi zilipomzima akaibuka hayati Mtikila na alipozimwa milele asiweze kuongea tena wamezaliwa kina Fatuma Karume na wanaharakati wengi wanaotumia majukwaa ya kupashana habari katika kuitetea haki wanayoona kama vile mfumo wetu unajaribu kuiminya.

Mzee Shamte kuwa kimya, maana yake wataibuka wengine machachari na wenye uchungu mkubwa zaidi.
Naona mzuka wa manjano umepanda
 
Alikuwepo hayati Mapalala na mamlaka za nchi zilipomzima akaibuka hayati Mtikila na alipozimwa milele asiweze kuongea tena wamezaliwa kina Fatuma Karume na wanaharakati wengi wanaotumia majukwaa ya kupashana habari katika kuitetea haki wanayoona kama vile mfumo wetu unajaribu kuiminya.
Tuliambiwa ajali ya gari, kumbe naye alizimwa?!
 
Haki daima huwa ni ya asili ni vigumu kuzuia isidaiwe. Sheria ya maisha ya binadamu huonesha ukweli huo. Marekani walidhani kuwa kumuua Martin Luther King na Malcolm X watakuwa wamefanikiwa kunyamazisha ujumbe wao.

Likawa ni kosa lililofanywa na CIA, wakaibuka wapigania haki wengine wa miaka ya 1970 na 80 na moto ukawa ni ule ule waliojaribu kuuzima kwa kuwanyima haki ya kuishi wamarekani weusi wawili. Sauti ya haki ni ya Mungu ni vigumu sana kuipoteza, sana sana yanakuwa ni yale mambo ya kumpiga teke chura unachokifanya ni kumuongezea tu mwendo.

Mapambano ya kudai haki huwa na kawaida moja ya ajabu sana. Kwamba yule anayezimwa milele asiweze kusikika hupata mrithi mwenye maarifa na uelewa kumzidi yeye anakuja kuzisumbua mamlaka zile zile zilizodhani zimemaliza kila kitu.

Sauti ya Mzee Shamte huko Unguja na Pemba inaweza kuwa imezimwa na mamlaka zilizoingia madarakani kihalali, ilitaka kujitanua sauti ile ili iweze kuwafumbua macho wenye nchi yao lakini mifumo ikamuwahi mzee wa watu na kwa sasa ni kimyaaaa.

Awamu ya nane huko Zanzibar iliingia uongozini kwa pesa nyingi za waarabu. Mlungula ulitembea haswa kipindi kile cha uchaguzi wa 2020, na waliokuwa wakiutoa ni waarabu. Sasa pesa ina kawaida ya kutaka irudi kwa namna moja au nyingine.

Ukikubali kununulika, lazima kuna siku inakuja inabidi utii kile unachoambiwa na aliyekununua. Ukitabasamu wakati unapokea chochote chenye harufu nzuri lazima kuna siku utatakiwa utoke nje wakati wa jua kali na mamilioni ya macho yakikutazama halafu ukatakiwa kuifanyia kazi ile pesa iliyopewa ndani ya vyumba vyenye viyoyozi vya mahoteli makubwa.

Kuwapa wakodishaji wa ardhi (kama wanavyoitwa) haki ya kukodisha kwa miaka 99 ni suala la hatari sana kwa uhuru mzima wa nchi husika. Na haya maneno ni ujumbe wa Mzee Shamte aliyenyamazishwa na baadae akaja kuombe msamaha.

Tunarudi kule kule katika suala la haki kuwa ni la asili (nature). Nafsi ya Shamte ipo kimya japo sio kwa kupenda mwenyewe, itaibuka nafsi nyingine yenye elimu, busara, upeo na hekima ya kidunia kuliko ile ya Mzee Shamte na itaongea na kuweka kila kitu hadharani. Ndio asili inavyotuambia siku zote.

Alikuwepo hayati Mapalala na mamlaka za nchi zilipomzima akaibuka hayati Mtikila na alipozimwa milele asiweze kuongea tena wamezaliwa kina Fatuma Karume na wanaharakati wengi wanaotumia majukwaa ya kupashana habari katika kuitetea haki wanayoona kama vile mfumo wetu unajaribu kuiminya.

Mzee Shamte kuwa kimya, maana yake wataibuka wengine machachari na wenye uchungu mkubwa zaidi.
Vipi mazombie wamemtoa roho huyo Mzalendo?
 
Haki daima huwa ni ya asili ni vigumu kuzuia isidaiwe. Sheria ya maisha ya binadamu huonesha ukweli huo. Marekani walidhani kuwa kumuua Martin Luther King na Malcolm X watakuwa wamefanikiwa kunyamazisha ujumbe wao.

Likawa ni kosa lililofanywa na CIA, wakaibuka wapigania haki wengine wa miaka ya 1970 na 80 na moto ukawa ni ule ule waliojaribu kuuzima kwa kuwanyima haki ya kuishi wamarekani weusi wawili. Sauti ya haki ni ya Mungu ni vigumu sana kuipoteza, sana sana yanakuwa ni yale mambo ya kumpiga teke chura unachokifanya ni kumuongezea tu mwendo.

Mapambano ya kudai haki huwa na kawaida moja ya ajabu sana. Kwamba yule anayezimwa milele asiweze kusikika hupata mrithi mwenye maarifa na uelewa kumzidi yeye anakuja kuzisumbua mamlaka zile zile zilizodhani zimemaliza kila kitu.

Sauti ya Mzee Shamte huko Unguja na Pemba inaweza kuwa imezimwa na mamlaka zilizoingia madarakani kihalali, ilitaka kujitanua sauti ile ili iweze kuwafumbua macho wenye nchi yao lakini mifumo ikamuwahi mzee wa watu na kwa sasa ni kimyaaaa.

Awamu ya nane huko Zanzibar iliingia uongozini kwa pesa nyingi za waarabu. Mlungula ulitembea haswa kipindi kile cha uchaguzi wa 2020, na waliokuwa wakiutoa ni waarabu. Sasa pesa ina kawaida ya kutaka irudi kwa namna moja au nyingine.

Ukikubali kununulika, lazima kuna siku inakuja inabidi utii kile unachoambiwa na aliyekununua. Ukitabasamu wakati unapokea chochote chenye harufu nzuri lazima kuna siku utatakiwa utoke nje wakati wa jua kali na mamilioni ya macho yakikutazama halafu ukatakiwa kuifanyia kazi ile pesa iliyopewa ndani ya vyumba vyenye viyoyozi vya mahoteli makubwa.

Kuwapa wakodishaji wa ardhi (kama wanavyoitwa) haki ya kukodisha kwa miaka 99 ni suala la hatari sana kwa uhuru mzima wa nchi husika. Na haya maneno ni ujumbe wa Mzee Shamte aliyenyamazishwa na baadae akaja kuombe msamaha.

Tunarudi kule kule katika suala la haki kuwa ni la asili (nature). Nafsi ya Shamte ipo kimya japo sio kwa kupenda mwenyewe, itaibuka nafsi nyingine yenye elimu, busara, upeo na hekima ya kidunia kuliko ile ya Mzee Shamte na itaongea na kuweka kila kitu hadharani. Ndio asili inavyotuambia siku zote.

Alikuwepo hayati Mapalala na mamlaka za nchi zilipomzima akaibuka hayati Mtikila na alipozimwa milele asiweze kuongea tena wamezaliwa kina Fatuma Karume na wanaharakati wengi wanaotumia majukwaa ya kupashana habari katika kuitetea haki wanayoona kama vile mfumo wetu unajaribu kuiminya.

Mzee Shamte kuwa kimya, maana yake wataibuka wengine machachari na wenye uchungu mkubwa zaidi.
Umeandika vizuri ,lakini Kuna wazee Tanganyika na Zanzibar wanajua Mambo mengi Sana kuliko hata yale ambayo tiyari yameandikwa kwenye vitabu au nyaraka mbalimbali, Hawa walitakiwa wanatafutwa na kuyaweka bayana KWa njia maandishi Ili vizazi vijavyo vije pata kumbukumbu hii, watawala watakuzonga kueleza Mambo mengine KWa maneno ya wazi ila KWa kalam hawataweza
 
Zenji huko, Mwinyi mtoto kapangisha visiwa kwa miaka 99.
Sasa huoni huu uzi ungekuwa mtamu sana kama ungekuwa na Sentensi hii Moja tu..., Naomba kama hautaona shida sana fungua uzi wenye hii sentensi moja tu.., ili watu waanze kushuka pros and cons za haya mambo aliyo-tutahadharisha Ndugai....
 
Umeandika vizuri ,lakini Kuna wazee Tanganyika na Zanzibar wanajua Mambo mengi Sana kuliko hata yale ambayo tiyari yameandikwa kwenye vitabu au nyaraka mbalimbali, Hawa walitakiwa wanatafutwa na kuyaweka bayana KWa njia maandishi Ili vizazi vijavyo vije pata kumbukumbu hii, watawala watakuzonga kueleza Mambo mengine KWa maneno ya wazi ila KWa kalam hawataweza
Historia inaandikwa na walioshinda. Wanachaguwa waandike nini. Kiandikwe kwa mtazamo upi na kipi kisiandikwe kabisa.
Wasomi wametelekeza jukumu lao kubwa la kusimamia ukweli. Nao wamekuwa wanasiasa.
 
Historia inaandikwa na walioshinda. Wanachaguwa waandike nini. Kiandikwe kwa mtazamo upi na kipi kisiandikwe kabisa.
Wasomi wametelekeza jukumu lao kubwa la kusimamia ukweli. Nao wamekuwa wanasiasa.
Ni kweli ila KWa sasa dunia inaenda Kasi ,wakiamua kuyaweka hata yale watawala hawataki sikia inawezekana, mfano mtu achukue clip ya history nzima nyumbani kwake ,na kitabu kiandikiwe huko ugaibuni watawala wasiotaka mengine kujulikana watafanya nini, au mtu mwenye ukweli wa haya Mambo asafili na kutolea kitabu chake nchi za mbali wasiopenda watafanya nini?
 
Ni kweli ila KWa sasa dunia inaenda Kasi ,wakiamua kuyaweka hata yale watawala hawataki sikia inawezekana, mfano mtu achukue clip ya history nzima nyumbani kwake ,na kitabu kiandikiwe huko ugaibuni watawala wasiotaka mengine kujulikana watafanya nini, au mtu mwenye ukweli wa haya Mambo asafili na kutolea kitabu chake nchi za mbali wasiopenda watafanya nini?
Ni kweli yawezekana.
 
Back
Top Bottom