Mzee Tashrif kafariki leo na kazikwa leo. Waislam wanajua heshima, umuhimu na maana ya mazishi

Mzee Tashrif kafariki leo na kazikwa leo. Waislam wanajua heshima, umuhimu na maana ya mazishi

Ndio maana nimeweka hapo kuwa ni maoni yangu binafsi na sio msimamo wa uislam, mimi sio mfuata kila linalosemwa kwa sababu natambua uislam asili yake sio huku kwetu na pia ni karne nyingi zimepita lazima mabadiliko yawepo.

Maelekezo ni kuwa mtu akifa inatakiwa azikwe haraka wakati huo, now lazima nifanye reasoning kwa nini ilisemwa hivi, nagundua ala kumbe wakati huo hakukua na teknolojia kubwa katika uhifadhi wa maiti, mawasiliano, uchukuzi n.k. Lakini uzuri zaidi imesisitizwa tu kuwa mazishi yafanyike haraka, hakuna palipotajwa kuwa yafanyike haraka kwa kiasi gani kwa hiyo kwako wewe masaa mawili unaweza kutafsiri kwamba ni haraka, yule akatafsiri haraka ni masaa sita na mimi nikasema haraka ni siku tatu, hakuna tatizo hapo.

Mimi sio kama wewe unafuata lolote bila kufanya reasoning, chochote kikitamkwa ni lazima kina sababu nyuma yake.

Wewe unavojinasibisha kua ni Muislam na izo reasoning zako chunga sana usije kua umesharitadi nahisi huujui uislam vizuri kua makini, kwenye issue za dini usilete usomi wako,usilete reason zako wala nini kitu kilichokua kimepokelewa na kupitishwa kama hadith sio kitu chakurekebisha vinginevo utakua unapinga na ukipinga maanake unakataa mafunzo ya mtume wetu Muhammad s.a.w na unaweza jikuta hauna dini au mwingoni mwa wanafik ama wasio amini kisa kutafta kuonekana unathinking capacity kubwa umu JF,

Ukisema kuweka reasoning wapo waislam kwa kwafikra zao watasema sisi bas tunachoma maiti maana kipind cha mtume walikua na sehemu za kuzika saiv kuna population hatuna sehem za kuzika

Kuna wengine watasema sisi tunazika kwa kama MAGHOLOFA(sio kwenye ardhi) maana kwenye ardhi watu wanatumia miili sana kufanya SHIRKI au waislamu wengine walio kwenye nchi za BARIDI watasema si hatuziki maana maiti zetu hazioz uko jangwani ndo kuna joto kwaiyo mtu akifa wanampamba tu kwenye mabarafu mwisho utakuta kila bala ama nchi waislam wana namna yao ya kuzika na iyo itakua kufru kubwa maana nikuyaacha mafundisho ya mtume wetu Muhammad s.a.w

Mtume sio mjinga aliposema tuwahishe kuzika huo ndo utaratibu na uislam unasheria na kanuni zake worldwide yan ukimwona mtu tuu unajua uyu ni mwislamu bila hata ya kuuliza kama kweli anafata maagizo sheria na kanuni za dinni.


jifunze kua humble kusoma zaidi dini kwa maana watu walio soma zaidi hua wanasifa za upole na akiongea huongea points jikite kwenye ibada timiza maagizo ya mola wako af mengine utajua siku ya mwisho ukiwa mbele ya mola wako otherwize labda we sio Muislamu ama Muislamu jina.
 
Hapo laizzm gharama nazo ziwe kubwa.. matokeo yake kukalifishana kwenye michango ya malaki ya pesa...roho ishaenda kukutana na amali zake nyie manabaki kuranda randa na kukaa na mwili ulokuwa hauna tena faida
IMEANDIKWA!
[emoji116][emoji116]
Yoshua bin Sira.38:16-23
16Mwanangu, mlilie mtu aliyekufa;
lia kwa uchungu, kuonesha huzuni yako.
Uuzike mwili wake kwa heshima ipasavyo,
wala usipuuze mazishi yake.
17Lia kwa uchungu na kwa moyo,
hudhuria matanga kama anavyostahili marehemu,
omboleza siku mbili tatu usije ukasemwa;
kisha ufarijike kutokana na huzuni yako.
18Maana huzuni huweza kusababisha kifo,
na huzuni ya moyo hunyonya nguvu za mtu.
19Mtu akiondolewa duniani huzuni imekwisha,
lakini maisha ya maskini, huulemesha moyo.
20Usiruhusu moyo wako kutawaliwa na huzuni;
ifukuze huzuni, ukifikiria mwisho wako.
21Usisahau kwamba hakuna kurudi nyuma,
humsaidii marehemu chochote na unajidhuru mwenyewe.
22Kumbuka, utakufa kama alivyokufa,
jana yeye, kesho wewe.
23Marehemu anapowekwa kupumzika kaburini,
nako kumkumbuka kuachwe;
nawe usiendelee kumlilia roho yake ikisha ondoka.
 
Hakuna kitu kibaya kama kukariri, kwa hiyo mimi kuita hija ni utalii unaniita kafiri, hebu tutazame maana ya neno hijja


Hijja ama Hajj ina faida kubwa sana kwa nchi ya saudi arabia.

Baada ya mafuta.. chanzo cha pili cha mapato utalii wa kidini ambao ni Hijja.
Fungua hii link
Mungu akufungue ufahamu nduguu
Nguzo ya tano ya uislamu Hyo Broo
Sio kunufaisha Waaarabu bwana
 
Unaweza kuorodhesha majina ya au taja angalau watatu waliowahi kuzikwa kabla ya kufa? Nipo hapa nasubiri
Kwani unapopelekwa makabulini kwa takbira unaweza ukasema nipo häi msinipeleke!
Hapo udongo ukikukandamiza uko peke yako nani wa kuorodhesha wakati watu wamesha tawanyika wenye maradhi wanampa pole nyingi mjane[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Umeshindwa vizuri ila kumbuka zipo nchi zinatekeleza
Hizo ni nchi za kizombi zinazoishi karne ya 7. Ndio manaa hata ninyi wenyewe hamna ndoto za kuishi Iran wala Afghanistan, mna ndoto za kuishi Marekani na Ulaya ambako hizo sheria hazipo.

Nyie hapa Tanzania mnatekeleza amri nyingi za Alah kama swala, kufunga etc...

Mbona amri ya kuua wanaouacha uislam hamuitekelezi? Ni kwa sababu IMEPITWA NA WAKATI kwa kizazi cha karne hii.
 
Unatubu dhambi kwa kiumbe mwenzio yesu,huo ndio ushirikina na ukafiri kimbia haraka
Ungeweka ushahidi basi!; Na sio Unaropokwa na kuturushia [emoji15][emoji12]
 
Uislam hauendeshwi kwa mawazo na busara zako, uislam unaendeshwa kwa kufata Quran na Sunnah

Katika uislam mambo matatu yanatakiwa yafanywe haraka.
1.Mtu anapohitaji kuoa aozeshwe haraka
2.Mtu anapotaka kuslim asilimishwe haraka
3.Mtu anapo fariki azikwe haraka.

Huo ndo uislam kila kitu kimefundishwa katika uislam had staili ya Kutembea, kula&Kunywa, kuvaa, kulala, kuamka, kiiila kitu kimefundishwa na huo ndo unatakiwa uwe mwenendo wa waislam na siyo burasa zako na maoni yako.
Weka ushahidi wa ayat quran inawaagiza mkifa mkamūane ngama![emoji101][emoji101]
 
Ni ukengeufu hata biblia haijaainisha hvyo, imeainisha vilevile waislamu wanavyofanya
Bibilia gani imeainisha namna ya kuzika? Unajua Yakobo alisafirishwa siku ngapi mpaka akazikwa? Je umesoma walimuombolezea siku ngapi?? Kila mtu abaki na utaratibu wake katika kuzika hatuwezi fanana, Cha msingi hakikisha jina lako limeandikwa kwenye kitabu cha uzima, hakuna tuzo katika mazishi
 
Mzee Tashrif kafariki leo na kazikwa Leo , hvyo ndo inavyotakiwa , sisi wakristo ni wakengeufu sana , Hata Biblia haihalalishi kuhifadhi maiti mda mrefu , mfano Yesu alifariki akazikwa sku hyo hyo,

View attachment 2585799


Mlolongo wa mazishi kwetu sisi wakristo ni kama ifuatavyo.:

Mtu anafariki , anahifadhiwa mochwari sku nzima, kesho yake anahifadhiwa tena , sku inayofata watu wanajikusanya , sku inayofata anafanyiwa ibada fupi kanisa la nyumbani na anaagwa , sku inayofata anasafrishwa kwenda kwao , sku inayofata anafikishwa kwao, zinapita sku mbili akisubiriwa mwanae kwani yupo ulaya, baada ya hzo sku mbili sku inayofata inafanyika ibada fupi ( syo fupi kama unavyofkri) anaagwa , na kama makaburi yapo karbu basi huzikwa... Na kama yapo mbali husafrishwa na sku inayofuata huzikwaa... Too long

Watu washalia vya kutosha , watu wamesimamisha shughuli zao zaidi ya wiki wanazurura tuu, gharama zimeongezeka mara dufu mana watu wamekusanyika nyumbani kwake na kule anakozikwa pote lazima wahudumiwe, madaftari ya michango ya uongo na kweli kila kona na watu washapita na rambi rambi , mwisho wa sku familia kuachiwa mzigo wamadeni

Tashrifu hakuwa mtu mdogo ila mazishi yake yamezingatiwa kwa uharaka zaid....


Wakristo tuendelee kuchukua notisi
Ni hivi, wewe sio MKRISTO
 
Kwani unapopelekwa makabulini kwa takbira unaweza ukasema nipo häi msinipeleke!
Hapo udongo ukikukandamiza uko peke yako nani wa kuorodhesha wakati watu wamesha tawanyika wenye maradhi wanampa pole nyingi [emoji38][emoji38][emoji38]
Maneno meeengi bila ushahidi ni kelele tu
 
Mimi ni muislam lakini katika suala la kuwahisha mazishi niko kinyume na wengi.

Kuzika haraka mtu anapofariki sio muongozo wa quran bali ni maelekezo ya mtume wetu kutokana na wakati wao hakukuwa na teknolojia ya kuhifadhi maiti ili ikae muda mrefu.

Pia kutokana na joto la huko jangwani ikawa ni rahisi maiti kuharibika upesi, lakini pia kutokana na kukosa mawasiliano ya simu wakati huo ikawa sio rahisi kuwapelekea taarifa watu waliopo mbali ili wawahi mazishi, kwa hiyo mtume kwa hekima akasema kati ya mambo yanayotakiwa kufanywa haraka basi mazishi ni mojawapo.

Sasa kwa kuwa nyakati zimebadilika, teknolojia imekua kwa maana maiti inaweza kuhifadhiwa muda mrefu na pia wafiwa pengine wapo mbali na taarifa wamepata kupitia simu au whatsapp, je kuna ubaya gani kuchelewesha mazishi kwa sababu mazishi pia ni ibada mtu akihudhuria anapata thawabu.

Haya ni maoni yangu binafsi kwa sababu kuna Uislam na Uarabu, kun mambo inabidi kuyafuata kama Uislam unavyosema lakini pia kuna masuala ya utamaduni wa kiarabu ambao huku kwetu hauko applicable sio mbaya kama tutaacha huo utamaduni bila kuathiri dhima ya Uislam.
Akhiiy kaa chini usome
Dini ya Uislamu haiongozwi kwa akili bali kwa kufuata Quran na Sunnah

Nb. Kama huna elimu katika yetu nyamaza kimya acha wajuzi wazungumze
 
Naona wafia dini hapo juu wananiattack sana, naomba nitoe kauli yangu.

1.Hakuna sehemu niliyosema kuwa uislam uendeshwe kwa matakwa yangu

2. Hakuna nilipodeclare kwamba mimi ni msomi.

3. Hakuna mahali nilipozuia wafu kuzikwa haraka.

Ila nilitoa maoni yangu kulingana na Uislam na utamaduni wa Kiarabu kwamba hili jambo la kuwahisha kuzika nadhani ni kutokana na ukosefu wa teknolojia wakati huo kama mawasiliano, uhifadhi wa maiti na pia uchukuzi, ndio maana ikashauriwa kuwa maiti azikwe haraka, nimeandika neno imeshauriwa kwa sababu hakuna sehemu iliyoweka amri katika jambo hili.

Kuhusu uharaka wa kuzika hiyo ni perceptions za watu, kwa mfano mimi naweza kusema kuzika haraka ni ndani ya masaa mawili baada ya mtu kufa, mwingine akasema kuzika haraka ni baada ya masaa 24 ndugu wakishafika, mwingine anawesa kusema watoto wa marehemu wapo Marekani wanataka kushiriki ibada ya mazishi hivyo tutasubiri kwa siku tatu ili wafike, hiyo pia ni haraka kwa sababu hakuna maiti inayowekwa tu ndani halafu watu wakae nayo bila sababu.


Hayo yalikuwa ni maoni yangu, ssa tuje kwenu wafua dini mnijibu maswali haya mawili.

1. Tafsiri ya neno haraka nyinyi ni muda gani?
2. Mtume (S.a.w) alipofariki hakuzikwa siku hiyo hiyo, nini kilifanya wacheleweshe kuzika na je hapo hakukuwa na ulazima wa kufuata hiyo haraka mnayoipigia kelele.


NB:
Raha ya dini uamini kwa tafakuri sio kukaririshwa bila kufanya reasoning.
Kuna Uislam na kuna utamaduni wa kiarabu.

Naona umekazana na uislam na uarabu kwanza nikuhakikishie kuwezi kuutenganisha uislamu na huarabu utafanya vyoote lakini utararudi kwenye asili ya dini na sehemu ilipopokelewa.

Rejea kwenye LUGHA ya Qurani tukufu.

Pili jua kua sio kwakua uislam umeanzia uko middle east ndo kilawaho wanachokifanya ndo uislam hapana[emoji777] au kila tunachokifanya kwenye uislamu ni uarabu hapana[emoji777]

Kuna vitu vimewekwa kua ni sahihi na vitu vingine kua sio sahihi, mungu alipomchagua mtume wake atokee huko alikua na maana yake(HEKMA) na sijui ulitaka amchague mtume kutoka africa walipokua wanavaa nusu utupu!!!

Note ”Mungu ndo mjuzi wa yale tunayoyajua na tusoyajua, hakika hata angechagua mtume wake kutoka yoyote basi ingekua sahihi”

Mfano kuhusu vazi la kanzu, Kanzu ya asili yenyewe inasifa zake, kuanzia rangi mpaka muundo (haina mambo mengi, ipo kama sanda),

Mfano, HEKMA iliopo kwenye ilo vazi ni kua kama wote tungevaa kanzu ya asili hakuna ambae angeonekana tajiri au masikini ndani ya msikiti, haina maneno yotote ivo hata ndani ya ibada unakua na concetration, wala wakati wa swali haitokupa shida wala kuwaza mambo mengine.

Em assum upo ndani ya ibada af mtu anakuja mbele yako kavaa jezi ya Yanga au sijui Arsenal na wewe ni shabik wa mpira automatic mawazo yataenda kwenye match badala ya kufanya ibada.

Kanzu Ilipendekezwa kupitia sifa zake na ndo maana likawa ndo vazi rasmi kuvaliwa kwa mtu aliyemuislamu na wala sio dhambi kuvaa tofauti as long as sifa za asili za mavazi (kike&me) yalioruhusiwa hujapunguza hata moja kwaiyo usitake kusema kanzu ni tamaduni za waarabu kwaiyo sisi waafrica haifai kisa baridi sijui joto sijui unataka tuvae suti?,

kanzu itabaki kua VAZI bora kwenye uislamu, Sisi tunafata Qurani na sunna, kama mtume alivaa kanzu au alifuturu tende bas jua kanzu itakua na bora kuliko mavazi mengine kwaiyo ni muhimu sana japo sio lazima kuvaa, pia kama mtume alipenda kufuturu tende bas kama unauwezo nivizuri na muhimu kufuturu tende kuliko kitu kingine ila sio lazima na ivoivo kwa vitu vingine kama kufuga ndevu, kulala, kuoga, and etc kwa sababu ni SUNNA.

Swali no 1
Swala la muda ni limehusiwa(kusisitizwa) kua tuwazike marehem mapema iwezekanavyo.
Tunaposema mapema ni kua kama hakuna sababu ya MSINGI yakutozika mfano kwa sasa;
*Police kesi (uchunguzi wa mwili)
*Usafi (Mfano mwili ulo na risasi unabidi utolewe risasi zote kwanza ndo uoshwe then uzikwe)
*Mgogoro wa kifamilia (kuna miili watu wanakua wanavutana wengine wanavutana kua marehem azikwe dini hii wengine wanakataa)
*Utaratibu wa hospital (Labda mwili unadaiwa) and etc

Sio izo sababu zenu za et kuna mtoto wake yuko marekani kwaiyo mpaka afike!
Sijui mwili lazima ulale kwake kwanza sijui kusafirisha au kwakua kuna fridge za kutunzia maiti kwaiyo ni sawa tuu kutunza maiti hata mwezi!!! and etc. Unataka kuturetea mambo yakiwafiri tuu mwisho utasema kupiga picha za mwili kama kumbukumbu ni sawa maana zamani walikua hawana camera, saivi tuweke qaswida msibani maana zamani hawakua na speakers kwaiyo saiv ni sawa!!!

Swali no 2.
Mtume hakuzikwa sikuiyoiyo kwanza tambua mtume NI HAKUZIKWA ingekua unanambia kuna hadithi ilo thibit kua mtume alipata msiba wakat akiwa hai na alichelewesha kuzika apo ningekuelewa maana hatujudge matendo baada ya mtume tunajudge kile alochofanya yeye sababu baada ya kufa huenda hata maswahaba wake wangeutupa mwili lakini iyo isingekua juu yake maana keshakufa na kama kufundisha keshafundisha kwaiyo kufwata ama kutofwata alichoelekeza ni juu yetu sisi sio yeye tena.

Pili mapokeo ya hadithi za kifo chake zipo nyingi ila nyingi zinaonesha kipindi umauti unamkuta alikua na upande wa ke na ilibid wapetikane upande wa me na walipotimia 6 wakiongozwa na Ali ibn Abi Talib maramoja walifanya taratibu zote za kuzikwa kama mafundisho ya dini yetu yanavyo hitaji, huwez kuzika ukiwa mtu mmoja

Kwaiyo unaona kua sababu ilo wapelekea kuchelewa kuzika sio ya kizembe wala mahitaj ya mtu binafsi au kundi la watu, ila kama uwezekano wakuzika ungekuepo mda huo bas angezikwa.


Mwisho nawasiwasi nahisi wewe sio muislamu huwezi kua muislamu af ulete izo reasoning zako kwenye dini na hayupo mwislamu wa ivo usiijite et we ni mwisilamu wa haina flani muislamu ni muislamu tuu wote tunaafata na kuamini kitabu kituqufu na mafundisho ya mtume fullstop.
 
Mzee Ngorika alipofariki, Mabasi yake Ngorika yaliyokua na route za Dar-Arusha Tanga-Arusha yakapotea.

Warithi wa Tashriff wajifunze
 
Back
Top Bottom