NAMNUKUU
"Hiko chama cha ACT Wazalendo kinachojilabu mwaka huu kitachukua Serikali mashudu, kusema kitu chengine bwana. Hapa waafrika hawatawaliwi tena, bora tufe sote kiwanja kiwe hakipo lakini hatutawaliwi, hamuwezi kutufanyia upuuzi huu.
Eti kusema mwaka huu tutashinda ACT wazalendo, nipike mie, nipakue mie, nilishe halafu wewe ije ushibe mimi nikae na njaa, maneno haya yametoka wapi. Hivi kweli hiyo! Tisha toto tu hiyo. Ikifika kweli chama cha Mapinduzi kitanyanyua makucha, kila mmoja hataiona kali yake.
Chama cha CCM hakijaumbwa kushindwa kwa njia zote. Piga, chinja, nyanyua, akinyanyuka anasonga mbele anachukua nchi. Tulifanya mapinduzi kwa hilo"