Mziki wetu Unaangushwa Na "Beats" Na Sio "Mashairi wala Videos"

Kuna wimbo wa jamaa anaitwa PSY unaitwa Gangnam style, hebu nitajie kama umebebwa na vocal na melody ama beat pekee?
 
Hiki kitu naunga mkono.
Diamond kafanya wimbo na Neyo halafu umeisikia beat? Utacheka.

Darasa beat ya Muziki akaona imeteka watu kilichofuata? Akatoa hasara roho na utanitoa roho zikiwa na beat kama ile.
Ujinga ni kwamba hata ile muziki sikuona watu wameona nini mule lakini hizi mbili ni floppy.

Rayvanny katoa wimbo mpya, Zezeta, wimbo beat, melody mpaka vocal ya kawaida mno.
Pro WCB wanakwambia wimbo mkali. Huo wimbo ni mkali kwa masikio ya kitanzania lakini huo wimbo tukiutoa nje nani atasikiliza?
Shenzi.

G Nako na Belle 9 katika wimbo Go Low na Ma ole wamesoma alama za nyakati, ingawa G kakopi ngoma.
Ben pol kafanya poa kwenye huu wimbo 3, kuanzia beat, melody, vocal mpaka video.

Kuhusu beat tunaweza ongelea siku nzima.
 
Kuna wimbo wa jamaa anaitwa PSY unaitwa Gangnam style, hebu nitajie kama umebebwa na vocal na melody ama beat pekee?
Ngoja niusikilize then ntarudi Mkuu.
 
Kwa kuwa nyimbo za kileo ambazo biashara ndio msingi sio ujumbe beats kali ni lazima.
 
Kwa kuwa nyimbo za kileo ambazo biashara ndio msingi sio ujumbe beats kali ni lazima.
Hiyo ni dhahiri, hizi beat za Fire ya Diamond waNigeria wameshtuka wamezikacha ingawa ni wao diyo walizileta kwetu.

P Square wakaaga hizo beat kwa ngoma ya Away, Ycee akaruka na Omo Alhaji na hata remix ya huu wimbo beat haikurudi na midundo ya kinigeria. Wizkid na Come Closer beat imehama iko level za dunia na wimbo umeruka mpaka huko.

Davido akaanza na If, kaja na Fall, Maleek Berry na Kontrol, Runtown kwenye Lagos to Kampala alikua kama siyo yule aliyeimba Gallardo.

Wasanii wetu sijui hawana washauri...
 
In general, hapa kwetu wengi hawana vipaji wanalazimisha fani tu. Ni kiwataja JF haitoshi.
 
tatizo hapa kwetu ukiwaambia ukweli wasanii wetu unaonekana mnafki,lakini maproducer wa hapa bongo ovyo,yan bora wasanii waangalie mbadala wa producers wa bongo
 
Sheddy Clever Ndiye Producer Aliyemtoa Diamond Kimataifa Wimbo (my Number One Na Ntampata Wapi) Lakini Ajabu Akamuweka Producer Wa Kiwango Cha Chini Lazer

Nareel Pia Alimtengenezea Diamond Wimbo Wa (Nana) Ukamfanya Azidi Kung'aa Lakini Ajabu Diamond Hawatumii
 
Hakuna Anae Ujua Mziki Humu. Nmefatilia Comment Zenu Nnachokiona Mnashndana Kutangaza Studio Zenu. Mnafungua Studio Wkt Hamna Elimu Za Mziki, Mnatuletea Mitazamo Yenu Pumba. Km Wabongo Hawanajui Kutengeneza Bit Hao Akina Kiba, Diamond, Rayvan Wangetoa Wap Hzo Tunzo Za Nje? Mnajua Maana Ya Mziki? Je Akitokea M2 Akaimba Accapela Au Acoustic Hauwezi Ukawa Wimbo Bora? Tunavutiwa Na Midundo Wengi Kwakua Hatujui Kinachoimbwa Lkn Mzk Unamambo Mengi Zaid Ya Beats. Soko La Mziki Toka Nje Kwa Bongo Huwa Lina Vuma Km Upepo. Km Ni Mwenyej Wa Dar Unakumbuka 80's Zlivuma Nyimbo Za Marekani Na U.K Na 90's Wakavuma S.A Na Congo, 200n's Wakarudi Tenda U.S, Saiz Ni Zamu Ya Nigeri Ni Swala Tu La Fans Wamevutiwa Na Ladha Ya Kule So Co Lazma Tuige, Tumeiga Hipop Ya Marekan Imewafksha Wapi? Mkaanza Kuimba Kwaito Ya S.A, Leo Mnataka Mzk Wa Nigeria, Wenu Upo Wap? Kwann Tusitengeneze Mzk Kwa Style Yetu Nigeria Wakaiga Kwetu? Mzk Unaenda Na Culture Ya Mahali Husika, Co Kuiga2 Km Kasuku.
 
Mkuu umeeleweka lakini nna wasi wasi pengine wewe ndo hujui mziki au pengine hufahamu mashabiki wa mziki nje ya bongo wanahitaji nini,Unasema tutengeneze mziki kwa style yetu, Hilo hakuna aliyekataa lakini hyo style yetu inaenda na mdundo gani ili kushawishi dunia kusikiliza mziki wetu na sio wa nigeria?

Embu soma vizuri post yangu ya kwanza nimeelezea kwamba wanigeria wanafanya mziki wao kwa style yao na sometimes kwa lugha yao na mda mwingine wanaimba vitu hata havieleweki lakini midundo yao inatufanya hata mimi na wewe ambao hatuelewi mziki wao tunyanyuke tucheze ama tuweke kwenye simu zetu tusikilize...
 
Mkuu twende tartiiibu!!
Production ndio nini (nataka tuende sawa)
 
Hakuna Anae Ujua Mziki Humu. Nmefatilia Comment Zenu Nnachokiona Mnashndana Kutangaza Studio Zenu. Mnafungua Studio Wkt Hamna Elimu Za Mziki, Mnatuletea Mitazamo Yenu Pumba. ....
Wewe jamaa kwamba haujui tuzo zinakuja kutokana na kura au? Hata kama wimbo mbovu kabisa unaoujua wewe ukapigiwa kura na watu wengi ndiyo huo huo utaonekana bora.

Hoja yako ya kwamba hatujui muziki kwakua hizi nyimbo zinachukua tuzo ni mufilisi haina mashiko.

Beat ina mchango hutaki sema tuanze kwenda kwa mifano
 
kabisa, niko tayari kumpa mifano kibao tu
 
Km Hamtaki Acheni Ila Maproducer Waliosoma Hawawez Kusikiliza Mawazo Yenu, Ndo Maana Bongo Movie Imekwama Kwa Tabia Ya Kucopy, Angalia Movies Za Wamarekan, India, China, Korea, Haya Nimataifa Yenye Ushndan Na Kila Mmoja Anataka Cha Kwake Kiwe Bora. Na Mziki Upo Hivyo, Ss Unasema Tatzo Beats Nitajie Wimbo Uliousikia Hapa Bongo Uco Na Beat. Producers Wetu Wanafanya Kaz Nzr Na Wala Hawawezi Kusikiliza Ushauri Wenu, Km Kuna K2 Mmekiona Nadhani Wao Wanauwezo Wa Kuona Zaid Yenu. Ninyi Mnapagawa Na Mafanikio Ya Nigeria, Wale Wana Fanbase Kubwa Na Wanapeana Support Ndo Maana Unaona Akina Davido Wapo Juu. Km Unauza Vzr Kwa Population Ya Nigeria, Huwez Kushndwa Kutoa Quality Video. Lkn Wa Naigeria Ni Wakawaida Tu.
 
mto Mada yupo sahihi,angalia show za nje za diamond nyimbo ya number one remix ile beat ikianza tu watu hushangilia sana,iko catchy sana na suala sio kolabo na davido maana kafanya hadi na neyo lakini beat ya my number one ni nyoko sana
 
Maisha haya stress sana,badala ya kuleta midundo ya kuchamsha na kuchezesha tusahau matatzo watu wanaleta midundo ya kulia lia,wasanii wengi wa kuimba bongo hapa wanalia lia sana kwenye nyimbo zao.
Watoe midundo ya kuchangamsha kama wenzao wa west africa,watu wasahau shida zao,muzik burudani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…