Mziray AMEJISHUSHIA heshima yake

Maximo alikuwa sahihi kabisa kutowaita hao watovu wa nidhamu katika timu ya taifa. Lakini kwa sababu hayupo tena na hao jamaa wamepata nafasi ya kuitwa timu ya taifa ni muda muafaka kwao kurudisha imani kwa washabiki wa soka kuwa wamebadilika!
 

Yani kama huyo mwalami katuuza mechi ya ya brazil na kwenye kombe la chalenge.mapunda alimkimbia kaseja alipoenda yanga na huyo shabani dihile bora 2 nikaye kimya.Eti kocha unampanga golikpa ambaye hakudaka hata mechi moja kwenye ligi(bartez) Hizo ni akili kweli wakati wakina shabani kado walikuwepo
 

Phenomena nakuelewa unachosema. Lakini ukumbuke unapokuwa kuwa Kocha, unakuwa na wajibu mkubwa sana, kuanza kukimbilia kwenye media inakuwa kama ni mambo ya mipasho jibu nikujibu. Kama ni kweli tatizo lilikuwa hilo yaani maximo kumtogoza mke wa kaseja au kaseja kumtongoza mke wa Kaseja, lawama inabeidi ziwaendee TFF kwa kuteua kocha asiye na maadili. Lakini believe me hizo habari unazosikia kupitia radio mbao usiziamini sana. Sababu ya yeye kukaa kimya ni kulinda umoja na nidhamu ndani ya timu... maturity ya kocha pia inaonekana kwenye uwezo wake wa ku-handle media pressure, otherwise itakuwa ni vijembe kila siku radioni.

Wachezaji wa timu ya taifa karibu wote wana maadili mazuri, haya mambo ya wanawake ni nature ya wanaume wote. Beckham did it, Tiger woods did, Bill Clinton did and Even George Bush did it, na kazi ziliendelea vizuri tu. Hiyo si sababu. Sababu kubwa ni hiyo niliyosema ya kushangilia Mapunda kufungwa. Ni kosa kubwa la kiufundi alilofanya Kaseja.
 

Me sijamwona mwenye afadhali kati ya hao wote wawili.kaseja hana mawazo ya kufikiria kiundani zaidi ndo maana mechi na misri akampanga ambaye hakuwahi kudaka hata mechi moja kwenye ligi(barthez).Hivi m2 aliyelelewa kwao kwa karibu miaka ishirini unaweza kumbadilisha tabia ghafla, labda hao wakina chuji,kaseja na boban hawana nidhamu toka utotoni inahitaji muda kusoma tabia zao ili kuweza kuwabadilisha
 

Tuna mtu anaitwa Ballotteli, Bellamy kwa ukorofi ndo kwa sana tu lakini hawajaachwa kwenye timu zao. Lakini kibaya kwa Maskio Maksimo ni kwamba Kaseja alishaomba radhi kwa kosa ambalo halijulikani hadi leo lakini yeye akaendelea na uamuzi wake wa kutomrejesha kwenye timu ya taifa.
 
Tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu mpaka tutakapokua na Under 12, 16, 17, 20 za uhakika lkn hawa wachezaji wa vipaji binafsi hawa hakuna lolote la maana tutapata
 
Tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu mpaka tutakapokua na Under 12, 16, 17, 20 za uhakika lkn hawa wachezaji wa vipaji binafsi hawa hakuna lolote la maana tutapata

Na tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu mpaka hapo tutakapotaifisha viwanja vya wazi vyote na vya mashule ya umma vilivyouzwa kinyemela kwa watu hapa Dar na mikoani. Hii itasaidia watoto kupata sehemu za kucheza na kujifunza mpira mitaani wanapoishi.
 

Maskio Makisio anaonekana kuwa na uzalendo kwa Tanzania kuliko sisi wenyewe. Kosa ni kuwa Kaseja alishangilia kufungwa kwa timu ya taifa kwa kuwa yeye hakuwa golini, lakini Maskio Makisio alisikitika.
 
habari wana JF, mimi najiuliza hivi kwa nini vyama vya michezo mbalimbali hapa nchini kwetu Tanzania vikiongozwa na TFF.vimekuwa vikihangaika kuagiza makocha toka nchi mbalimbali wakiwemo wa karate, soka,netball, tennes, na kufukuza upepo n.k. napenda kuelewa hivi hii inatokana na kukosa makocha wazalemdo wenye weledi au?
 
may be it is collonialism mindset
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…