"Mzoea vya kunyonga vya kuchinja Haviwezi". Hongera Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji

Unatoa vitu katika magroup watsp ya ccm unaleta hapa??
 

Sasa kwa nini mliweka wagombea Ubunge wakati mlijua hayo?
 
Hata wakati wa uchaguzi waligombea hawa kina mama mbona hamkuwapigia debe leo ndio hashuo la kina mama

Sasa mbona ndani ya Chama hawakupewa nafasi ya Kugombea kidemokrasia?
Mmetumia ubabe kuvuruga Haki ya kinamama halafu mnalaumu uchaguzi uliofanya hayo hayo mliyofanya.
Watanzania wanataka Chama bora mbadala kwa CCM ,sio bora chama Mbadala.
 
Who is next?
Nani atafiatia baada ya kina Mdee?
A) Mwenyekiti
B)
Katibu mkuu
C) Makamu Mwenyekiti bara/visiwani

D) naibu katibu mkuu

E) Madiwani wateule?
 
Ulitakaje labda?


Jambo la kwanza Chadema ilipaswa kwenda mahakamani kupinga Majina yaliyopelekwa na NEC na kujenga hoja ya kwamba kuna Udanganyifu uliofanyika.
Lengo ni kumpata mtu mmoja au wawili waliopeleka majina yale NEC.
Uchunguzi ungefanyika ili abainike aliyepeleka na kusaini yale majina.

Haiwezekani kuwa Wanawake 19 pamoja na aliyekua Gerezani wote walibeba barua na form zile kama Jeneza na kuzipeleka NEC.
Kama ni Mdee aliyepeleka awajibishwe peke yake na wengine wabaki kama Wabunge mana wameshaapishwa kuwawakilisha wananchi .

Chama kingeweza kikawatoa kwenye Nyadhafa zao zote na kuwakana kwa kutoshirikiana nao kwa namna yoyote lakini sio kuwavua uanachama.

Hakuna nchi yenye Demokrasia isiyokuwa na mgombea Binafsi.
Kuwaacha bila kuwafukuza kungemaanisha kwa vitendo kuwa Chadema ni Chama Cha Demokrasia na kinapigania Demokrasia ya kweli na Katiba mpya inayoruhusu mgombes binafsi.
Wangehojiwa kwa umakini bila kukurupuka kama Mnyika alivyofanya kuanza kuwakashifu na kuwafokea kwenye motandao kabla ya kuwasikiliza.
Baada ya kuhojiwa wangebaini nani hasa aliyefanya figisu zile na huyo angechukulwa hatua kali.
Wakina mama ndio watakaoijenga Chadema yenye Wanachama wenye kulipenda chama .
Mtoto akizaliwa akalelewa na mama anayeimba nyimbo za kukijenga chama na Demokrasia atakua na kuwa na imani na chaka hicho. Kuwatisha wanawake na kuwafukuza bila kujali mazuri waliyoyafanya ndani ya chama hicho ni kujenga Udikteta wa viongozi wanaojiona ni miungu watu.
Tunasema kila siku Mkuu wa nchi apunguziwe madaraka ili asiwe mungu mtu lakini cha ajabu tunajenga vyama vyenye kiungu watu huku wakiwa wanawatawala wanachama wao kwa kujenga hofu na kutaka waheshimiwe na kutukuzwa kwa gharama za kuwaumiza wengine.

Jengeni Chama Chenye dira tofauti kabisa na CCM.

Tujiiulize wote, hivi wale akina mama walipewa nafasi ya kukaa kama jumuiya na kutoa maoni yao kisha kuamua kidemokrasia kwa kupiga kura ya kukubali au kukataa kupeleka majina ya Viti maalumu Bungeni!?
Jibu ni hapana!
Wanawake wale walikua wanalazimishwa kukubaliana na matakwa ya wanaume ambao hawana hizo nafasi na haziwahusu.
Ni nafasi kwa ajili ya wanawake ili kujenga jamii yenye akina mama jasiri watakaowalea watoto wetu na kuondoa mfumo dume unaowafanya wanawake wawe kama bidhaa ya kuwatumiwa na wanaume wenye madaraka.

Tuwape ruhusa hao akina mama wakate rufaa ndani ya chama kisha waondolewe nyadhifa zao lakini wasifukuzwe.
Historia itashindwa kutofutosha kati ya utendaji wa serikali ya CCM katika maamuzi na utendaji wa viongozi wa Chadema katika maamuzi.

Kama utendaji wa na maamuzi yasiyojali kanuni za kutoa haki yanayofanywa na mwenyekiti Mbowe ni muhimu na wapambe wake wanayafurahiya na kuyasifia basi hata Mwenyekiti wa CCM na Rais wa nchi anafanya vizuri bila kujali Uhuru wa kujieleza,kusikilizwa,kutendewa kwa utu na kuheshimu haki za watu katika ujenzi wa nchi.

Haramu iwe ni haramu bila kujali ikefanywa na nani?

Cha ajabu Mbowe na Mnyika wakifanya Ubabe wanatukuzwa na kushangiliwa na kuitwa mwamba lakini Magufuli akitoa maamuzi magumu anatukanwa na kutangazwa dunia nzima kuwa ni dikteta na mbabe.
Tujiulize tunafanya nini na tunataka nini?
 
Katika bunge hili hakuna KUB (Kambi rasmi bungeni)maana wapinzani hawafikii 12% ya bunge zima kwa mujibu wa katiba ya JMT
 

Mkuu nilipoona tu umesema waende mahakamani nikajua huna jipya. Fanya hivi, hebu anzisha chama chako tuje tujifunze demokrasia kwenye chama chako. Hapa cdm wamechukua maamuzi sahihi. Naona unalazimisha kuchanganya mambo mengi ili kupotezesha uhalisia wa mada husika.
 
Tatizo shule zetu haziandai watu kusimamia haki kiujasiri,wanaojiita wasomi tz kama mayala mmejawa na ubinafsi na unafiki!! Mnatafuta kazi /vyeo kwakueneza habari zakufraisha wenye dola bila kujali kizazi kijacho mnakifunza nini...
Membe aliitwa na Ccm na akaenda kiheshima hukuongea huu ujinga,kwani kwako mdee na wenzie ninani mpaka washindwe kuitwa na viongozi wake wachama?? Unatafuta kuteuliwa huwezi kujiajiri? Au matangazo umenyimwa sasa mayala(njaa) inakukabili unataka ubebwe kwakuwa wakanda maalumu?
Acha ushamba paskali kujipendekeza ni utumwa,pambana na maisha usisubiri kubebwa na system
 
Cjawahi kuona unahangaika kutafuta uteuzi ccm mbona wanafukuzana wewe ni Mwanasheria ukiitwa Mahakamani ukagoma kwenda kesi inasikilizwa upande mmoja na maamuzi yanatoka
Mpaka wanaapishwa gereji MTU anaachiliwa gerezani ucku nolle inatolewa mbele ya hakimu ama judge cyo huko mtaani kuna malice
 
This man called myl a freelancer might be a g*y...
 
Kwan bado hawajafukuzwa tu?
huyu dogo ameandika hii makala siku ya ijumaa wakati huo hajui kitachotokea kwa hao COV 19 wake maamuzi yamefanyika J1 na hao wadangaji wake WAMETIMULIWA .
sasa kwakuwa dogo Pascal Mayalla anajifanya mjuaji sasa aende kuwasaidia hao wadangaji awahamishie kwenye danga lao lumumba.
 
Chadema wakubali yaishe. Walishiriki uchaguzi ili wapate kura .Wamepata wabunge 20.Si haba wawape ushirikiano wawashe moto bungeni. Waendelee kujenga chama. Na waongee hoja bungeni. Maana huku nje wakiongea wanaitwa wachochezi.
WAMETULIWA COV 19
Ssa wasidieni kudanga nyie wazoefu
 
huyu dogo ameshakata netiweki siku nyingi mbona dishi limeyumba ndo mana anamwaga utopolo tu
 

Hili litakuwa sawa tu kama kuapishwa kwao hakukuwa na forgery. Pili, uongo walioongea mbele ya spika pasipo na uthibitisho kuwa walitumwa na Mwenyekit
 
Mkuu huyo jamaa humu kishajidharaulisha kuliko mwanachama yeyote aliyewahi kutokea hapa jamvini. Hawa ndiyo watu wanajiita wasomi lakini hawakuelimika hata chembe. Upuuzi wanaouandika ambao hauingii hata akilini unashangaza sana.


Kama Halima ni mwanasheria, alitakiwa kujua mwenye mamlaka ya kisheria ya kupeleka majina tume ya uchaguzi ni KM. Huu uzi unakuchoresha tu bro.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…