"Mzoea vya kunyonga vya kuchinja Haviwezi". Hongera Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji

Chadema wakubali yaishe. Walishiriki uchaguzi ili wapate kura .Wamepata wabunge 20.Si haba wawape ushirikiano wawashe moto bungeni. Waendelee kujenga chama. Na waongee hoja bungeni. Maana huku nje wakiongea wanaitwa wachochezi.
Thubutu hatutaki kukaa meza moja na wauaji , wamwaga damu , blood suckers .
 
Angekufa wasingefanya uchunguzi?
Shahidi wa kwanza ni dereva wake. Kwanini hataki kuja kutoa ushahidi? Hapa kuna harufu ya kutulaghai? Mleteni dereva tupate wapi pakuanzia ili maisha mengine yaendelee. Wewe Babati nineshakwambia nenda kalime msimu wa kilimo ndiyo huu, ndg wakigombana.....
 
Haiwasaidii chochote hao wasaliti, kufukuzwa kuko palepale
 
Mnyika vs serikali. Ajabu serikali imetumia nguvu kubwa Sana kuhakikisha upinzani hawaingii bungeni leo serikali inatumia vyombo vyake kuhakikisha upinzani wanaingia bungeni. Je serikali inavuta bange?
Mgonjwa wa bipolar disorder anatafuta tilioni mbili akisaidiwa na kina Mayala .
 
Sasa anaogopa nini kwenda kwenye kikao kueleza hayo?
 
Leo unahangaika sana kuanzisha thread, tulia dawa itakuingia tu na hao unaowatetea lazima wafukuzwe
 
Paskali kama jike hivi, sijui unatumia kiungo gani cha mwili kufikiri !!, miaka ya nyuma (kabla hujalishwa limbwata na ccm) ulikuwa ukiandika makala fikirishi, leo hii (Paskali) yule tuliyedhani atakuja kuacha historia ya uandishi nguli anaamua kutumia ujinga badala ya hekima kunadika mada mitandaoni ili kufurahisha serikali dhalimu ya chama cha mapinduzi, kilichofanyika Paskali ni kitu cha kufurahia kweli ???!!!
 
😂😂😂😂😂 leo hii ni shujaa na msomi???🤦‍♀️
 
Hata Kama hupendi kuwaita Hawa chadema wa mtandaoni nyumbu , kwa akili zao inabidi wait we nyumbu tuu maana hawaelewi na Hawana kumbukumbu kabisaaa.
 
Kama Halima ni mwanasheria, alitakiwa kujua mwenye mamlaka ya kisheria ya kupeleka majina tume ya uchaguzi ni KM. Huu uzi unakuchoresha tu bro.
Mkurugenzi wa NEC kasema mnyika alipeleka majina yao tarehe 19, Sasa huelewi Nini tena?
 
Tangu umejiunga ccm waziwazi imekuwa ngumu kukutofautisha na akili za akina james delicious...so sad Paskali.
 
Rubbish from lumumba
 
Kuna wakati napata tabu sana kuamini kwamba bandiko zingine huwa unaziandika ukiwa "in your real senses".
 
Paskali mara nyengine huwa unanishangaza na matumizi ya maneno yako hasa ukizingatia fani yako ya kazi. Hivi itakuwaje mkutano wa chama unauita mkotano wa kienyejienyeji? Hivi hapo ni vipi hasa? Wewe ulitaka waitwe vipi ikiwa chama kinataka kujua ni vipi waliweza kwenda kula viapo vya ubunge?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…