Wanabodi,
Hili ni bandiko elimishi kuhusu uendeshaji wa vyama vya Siasa nchini Tanzania, kuna vyama vinaendeshwa na viongozi kama mungu watu, na kujiendesha tuu hivyo vyama, wanavyotaka wao, kama mali yao, wakijisikia kufukuza mwanachama, hata kwa makosa ambayo sio ya msingi, wanaitana na kukaa kama Kangaroo court na kufukuza wanachama kwa kuwavua uanachama kienyeji enyeji tuu. Kufuatia kukithiri kwa tabia hii Chadema kufanya hivi bila kuhojiwa na yeyote, hatimaye sasa, tabia hii imeota mizizi na kuendana na msemo huu wa Kiswahili kuwa "Mzoea vya kunyonga, vya kuchinja haviwezi"! Chadema ilizoea kuwanyonga wanachama wake kwa kuwafukuza kienyeji enyeji na kujinga jinga, nimeisoma taarifa hii kwa faraja.
Halima Mdee ni mwanamke shujaa, msomi na mwanasheria, anaijua katiba ya Chadema, hivyo amegomea kikao kilichoitishwa kienyeji enyeji ili kumchukulia hatua yeye na wabunge 19, makandaa mashujaa wa kike wa Chadema, waliamua kutanguliza mbele maslahi ya Taifa vs maslahi ya chama.
Utangulizi: Haki ya Kujadili Mambo ya Chadema Kwa Mtu Ambaye Sii Mwanachama, Mfuasi, Mshabiki wa Chadema.
Sii wengi wanafahamu kuwa vyama vya siasa Tanzania, vyenye wabunge na madiwani, sio private parties za wanachama na viongozi, ni public parties za umma kutokana na kulipwa ruzuku ya serikali ambayo ni kodi yako wewe na mimi, hivyo Mtanzania yoyote ambaye ni taxpayers, has the right kuhoji jambo lolote kuhusu any public entity kwasababu inaendeshwa kwa kodi yake!. Hivyo nawaomba nyie manazi wa Chadema, mliotamalaki humu jf, kaeni mkijua mtoa mada ni mmoja wa wachangiaji wa fedha za kuiendeshea Chadema!, hivyo ana haki kuhoji jambo lolote kuhusu uendeshaji wa chama chochote, na ilimsidhanie nimeikamia Chadema tuu, nimeisha wahi kusema mengi kuhusu CCM, nimesema mengi kuhusu CUF, nimesema kuhusu NCCR, ACT, etc.
Kama Sio Chadema, Unahoji au Unajadili Mambo ya Vikao vya Ndani vya Chadema na Maamuzi ya Chadema ili Iweje?.
Hapa naomba kujitambulisha kama mwandishi wa habari wa kujitegemea. Fani ya uandishi nayo ina specializations, kama ilivyo ualimu, kuna waalimu wa somo la hesabu, Kiingereza, Sayansi, Jiografia etc, na kwenye Udakitari kuna madakitari wa meno, wafamasia, wapasuaji, madakitari wa watoto, kinamama etc, hivyo kwenye uandishi, kuna maripota, maproducers, ma presenters, news readers, wahojaji, yaani wafanya mahojiano, mimi nime specialize kwenye kufanya mahojiano, hivyo my area of specialization ni kuhoji tuu!. Kufuatia kazi yangu ni kuhoji tuu, nikikutana na jambo lolote ambalo sio la kawaida, kazi yangu ni kuhoji. Katika pitia pitia zangu Katiba za vyama, kuna siku nikakutana na kitu cha ajabu kwenye Katiba ya Chadema, nilipohoji kuhusu hicho kitu, na jibu ninilojibiwa na uongozi wa juu wa Chadema, ndipo nikagundua kuwa kumbe kuna viongozi hadi wa ngazi za juu za vyama ni ma mbumbumbu kuhusu baadhi ya vipengele vya katiba za vyama vyao, tangu pale nikajikuta kila Chama kikifanya uamuzi wa ajabu ajabu kinyume cha utaratibu wa katiba zao, mimi huwa naibuka na kukemea kwa kuwasisitiza waheshimu katiba zao. Hoja ya viongozi wa juu wa Chadema, kuwa mbumbumbu kuhusu katiba zao, tembelea uzi huu...https://www.jamiiforums.com/threads/tuhuma-hii-chadema-kendeshwa-kwa-katiba-fake-ikithibitishwa-chadema-inaweza-kufutwa.543947/
Kwa Vile Kamati Kuu ya Chadema Imewaita Kina Halima Mdee ili Iwahoji, na Wamegomea Mwito, Naomba Kuwaletea Vifungu vya Mamlaka ya Nidhamu Kwa Mujibu wa Katiba ya Chadema.
6.5 Taratibu zifuatazo lazima zizingatiwe katika kuchukua hatua za kinidhamu:-
6.5.1 Kila tawi litaweka kumbukumbu/orodha ya wanachama wanaokoma kuwa wanachama Uongozi na Vikao vya Tawi. Kumbukumbu itaonyesha jina kamili la mwanachama katika rejista ya wanachama tarehe aliyokoma kuwa mwanachama wa Tawi na sababu za kukoma kuwa mwanachama.
6.5.2 Kwa mujibu wa Ibara 5.4.3 na 5.4.4 ya Katiba, mwanachama yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama kuachishwa ama kufukuzwa uanachama bila kwanza:
(a) Kujulishwa makosa yake kwa maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili.
(b) Kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.
(c) Mwanachama atajulishwa kwa maandishi uamuzi wa kikao mnamo wiki mbili baada ya kusikilizwa.
(d) Kamati Kuu inaweza kuchukua hatua za dharura bila kuzingatia utaratibu wa kifungu (a) na (b) hapo juu kama itaona maslahi ya Chama kwa ujumla yanaweza kuathiriwa isipokuwa mwachama au kiongozi anayelalamikiwa atalazimika kuitwa kwenye kikao husika.
6.5.3 Mtu yeyote aliyepoteza uanachama wake kwa mujibu wa Ibara ya 5.4 ya Katiba atapoteza haki zake zote za uanachama na hatarudishiwa ada, zawadi au ruzuku yeyote aliyokwishaitoa kabla ya kupoteza uanachama wake.
6.5.4 Mwanachama aliyepewa adhabu na kikao kimoja cha kikatiba atakuwa na haki ya kukata rufani kwa kikao cha ngazi ya juu ya kile kilichompa adhabu.
6.5.5 Mwanachama aliyewahi kuachishwa ama kufukuzwa uanachama anaweza kuomba kurejea kwa maandishi kupitia ngazi iliyomfukuza akieleza sababu za kutaka kurejea. Maombi yake yatachunguzwa kwenye ngazi hiyo na kutolewa maamuzi na vikao vya ngazi moja ya juu inayofuata. Aliyesimamishwa au kufukuzwa na Kamati Kuu ataweza tu kurejeshwa na Baraza Kuu. Watakaofukuzwa na Mkutano Mkuu hawatakuwa na chombo kingine chochote kitakachotengua uamuzi huo.
6.5.6 Kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashitaka kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashitaka kwa maandishi.
6.5.7 Kiongozi mhusika, zaidi ya utetezi wa maandishi, atapewa nafasi ya kujieleza bayana mbele ya kikao cha mamlaka ya nidhamu.
6.5.8 Kiongozi aliyeadhibiwa atapewa taarifa ya misingi ya maamuzi ya mamlaka ya nidhamu ili kumwezesha kuamua kukata rufani au
6.5.9 Mwadhibiwa atakayeamua kukata rufani atatakiwa kufanya hivyo katika muda wa siku thelathini baada ya kuarifiwa uamuzi wa adhabu.
6.5.10 Baada ya kutoa uamuzi kikao husika kinalazimika kuandaa taarifa kamili ya mwenendo wa shauri na kuwasilisha ngazi ya juu. Taarifa hiyo lazima ifike katika muda wa siku kumi na nne baada ya kikao cha maamuzi.
Sasa kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, ili kumvua mtu uanachama kuna mlolongo wa kanuni na taratibu za kufuatwa kama nilivyo zianisha hapo juu, jee zilifuatwa?
- Kwa nini CC ya Chadema, inawaita watu kihuni huni tuu, bila kuandaa hati ya mashtaka kwa maandishi yenye tuhuma zote ambazo mtuhumiwa anakabiliwa nazo. Jee hati hizi za mashitaka kimaandishi ziliandaliwa?.
- Hati hiyo ya mashitaki kimaandishi inatakiwa ikabidhiwa kwa mtuhumiwa kwa "despatch" ili kuthibitisha imemfikia. Je, hili lilifanyika? Nimesikia kuna watu waliitwa kwa simu, je huu ndio utaratibu kwa jambo zito kama hili?
- Mtuhumiwa atatakiwa kuzijibu tuhuma za mashitaka hayo ndani ya kipindi cha siku 14 tangu tarehe aliyopokea barua ile ili apate muda wa kutosha kutafakari, je hili litafanyika?
- Baada ya majibu ya hati ile ya mashitaka kurejeshwa, ndipo mamlaka ya nidhamu ingepaswa kuitisha kikao rasmi kwa mujibu wa katiba na kumwalika mtuhumiwa kwa barua ili kuwapa nafasi ya kujieleza na kumsikiliza kabla ya kufikia maamuzi!. Jee this time Chadema itafuata taratibu?
Halima na genge lake they are very right, Chadema ilizoea kufanya mambo kienyeji, leo imekutana na kisiki cha mpingo!
Chadema sasa lazima ijifunze kufanya mambo kwa kufuata katiba yake, sheria, taratibu na kanuni!, kufanya mambo kwa kienyeji enyeji kwa mtindo wa zimamoto, sasa basi!
Hongera sana Kamanda Mhe. Halima Mdee na makamanda makomandoo wa kike kwa kuifunza nidhamu chama chenu cha Chadema.
Paskali
Update:
Mkuu mode, bila kuingilia uhuru na mamlaka yako wewe mode ku edit bandiko lolote na heading yoyote, ila heading inapotumia tamathali za semi, methali au nahau, neno hilo linapaswa kuwa vile vile lilivyo kwa sababu tamathali za semi, zinatumia vina, ukibadili kitu, vina havizami!. Mode hapaswi kulibadili!. Nimetumia neno
"Mzoea vya kunyonga, vya kuchinja haviwezi", hivi ndivyo neno rasmi lilivyo, ni tofauti na neno ulilotumia wewe.
Naomba neno rasmi lirudishwe!.
P