Na je! Imekufikia hadithi ya Musa? (Alipotumwa Kwa Firauni)

Na je! Imekufikia hadithi ya Musa? (Alipotumwa Kwa Firauni)

Meneja CoLtd

Senior Member
Joined
Mar 6, 2021
Posts
122
Reaction score
143
Habari zenu wana JF leo nimeona sio mbaya nikiwaletea hadithi fupi ya Mussa alivyo tumwa Kwa Firauni na Majibizano kati ya Mussa na Mungu wake juu ya mikakati ya kumkabili Firauni,

Mungu hakumuacha Nabii wake Mussa hivi hivi alimpa miujiza Ili akakabiliane na mwamba Firauni, Shuka nayo sasa..

MUSSA: .......Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto.

Basi alipo ufikia akaitwa na MUNGU: Ewe Musa!

MUNGU: Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la T'uwa.

Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa.

Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi....

Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?

MUSSA: Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine

MUNGU: Akasema: Itupe, ewe Musa!

MUSSA: Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio

MUNGU: Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza.

MUNGU: .....Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka.

REF: QUR'AN 20:9-24
 
Habari zenu wana JF leo nimeona sio mbaya nikiwaletea hadithi fupi ya Mussa alivyo tumwa Kwa Firauni na Majibizano kati ya Mussa na Mungu wake juu ya mikakati ya kumkabili Firauni,

Mungu hakumuacha Nabii wake Mussa hivi hivi alimpa miujiza Ili akakabiliane na mwamba Firauni, Shuka nayo sasa..

MUSSA: .......Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto.

Basi alipo ufikia akaitwa na MUNGU: Ewe Musa!

MUNGU: Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la T'uwa.

Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa.

Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi....

Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?

MUSSA: Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine

MUNGU: Akasema: Itupe, ewe Musa!

MUSSA: Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio

MUNGU: Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza.

MUNGU: .....Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka.

REF: QUR'AN 20:9-24
Kiukweli inabidi uiisome biblia ndipo utakielewa kisa cha Musa ila huku kwingine hakueleweki kabisa
 
Back
Top Bottom