Mpe machine tu hata tiGo mjiexpress tu, dunia yenyewe imekwisha hii!
Laana laana....aachane na hayo mambo kabisa...kama ameshatubu....akatae kabisa maana dawa dhambi ni kuikataa si kuiendeleza kwa mitego kama hiyo>>>>
Asithubutu kufanya hicho kitu na mama mkwe akimtishia zaidi amdanganye kuwa mkewe alijua UHUSIANO WAO na mdogo wake na alimuomba radhi yakaisha na kuwa akiendelea amtishie kuwa atamwambia mkewe,kwakuwa anaongopa ili kulinda ndoa yake na kutomuudhi muumba mungu atamsaidia, huyo mama ni fisadi! hifai hata kuendelea kuwa nae hapo nyumbani na kama ana mumme aambiwe kuwa na mume wake atajulishwa.Msaidieni Jamaa yangu huyu, aliponiomba ushauri nilimwambia anipe mwezi mmoja nifikirie:
Jamaa yangu anaitwa Sam(si jina la kweli) ni kijana mwenye mafanikio kimaisha,anafanya kazi katika kampuni moja ya mafuta hapa Tanzania. Ameoa na ana watoto wawili wemye miaka 5&2. Mwaka jana alikuja kutembelewa na shemeji yake ambaye ni mdogo wa kuzaliwa na mkewe. Binti huyo mwenye umri wa miaka 22 alikuja kupumzika huku akitafuta nafasi ya chuo kikuu dar baada ya kumaliza masomo yake ya kidato cha sita huko nyumbani kwao Tanga. Wakati fulani nyumbani kwao mkewe walipata matatizo yaliyo lazimisha mkewe kurudi nyimbani kwa wiki mbili, kipindi hiki jamaa yangu anasema shetani au ibilisi alitembelea nyumba yake na yeye na shemeji yake wakaanza mahusiano yasiyofaa. Baada ya wiki mbili mkewe alirudi na mama yake wakati huo jamaa yangu na shemejiye uhondo umewanogea. Siku moja usiku jamaa alichomoka chumbani na kukutana na shemeji yake sebuleni wakiwa katika hali mahaba mama mkwe akawaona kwa bahati mbaya hakupiga kelele wala kuwasemesha.Asubuhi yeye na mwanawe mdogo yaani yule shemeji wakaaga huku mkewe akishangaa kwa ughafla wa safari. Mamamkwe hakuthubutu kusema kwa mtoto wake kisa kilicho waondoa. Hata baada ya miezi mitatu yule binti alirudi kusoma chuo UDSM jamaa yangu alimfuata kumuuliza kilichotokea lakini yule binti kagoma hata kumuangalia na hajawahi hata kuisikia sauti yake, kifupi jamaa kabakia gizani. Hivi karibuni mama mkwe alikuja kuwa tembelea na wakati huohuo mama yake mzazi na jamaa yangu akapata maradhi kalazwa nyumbani kwao hukohuko Tanga.Kwa maana hiyo nyumbani amebakia jamaa yangu na watoto pamoja na mama mkwe. Sasa kasheshe mama mkwe anamkomalia jamaa ampe naye vitu na akikataa anamueleza mkewe kilichotokea usiku ule. Jamaa amekwisha tubu mara kadhaa na hataki kabisa kuchezea ndoa yake kwani anampenda mkewe sana. Ila mama mkwe yupo determined kabisa na mara kadhaa amekwisha mfuata bafuni uchi...Ushauri please!!!!
Ila mama mkwe yupo determined kabisa na mara kadhaa amekwisha mfuata bafuni uchi...Ushauri please!!!!
Bafu halina mlango nini?, nadhani huyo Mama Mkwe ana matatizo ya akili. Muhimu kumpeleka Mirembe. Lakini vyovyote iwavyo hilo suala ni aibu kubwa si kwa huyo Mama tu, hata kwa jamaa yako, manake inaonekana haridhiki mpaka kula shemeji yake. Dawa aende angaza, akirudi amuoneshe awe na mawazo kibao, then Mama mkwe atamuuliza vipi?, amwambie nimeathirika, aone kama Mama Mkwe hatapoa. Kama hata hapo atahitaji, awahishwe Mirembe huyo.
Yaani watu wengine wa ajabu sana kama uhuni fanya nje tena mbali,uhuni unafanyia nyumbani kwako na shemeji na mama mkwe?
Mh kweli dunia imefika ukingoni.......... badala ya mama kuwa mwongozo wa ndoa njema ndo mharibifu!! Shemeji mwambie tu dada kuwa mama simwelewi kabisa ananifanyia manyang'unyang'u nisiyoyaelewa (amweleze kabisa kuwa anamtokea uchi sasa sijui ana maana gani) Jihami shem, maana akianza mama kusema hutaaminika. Hii itakusaidia kwani ukishasema unamtolea uvivu mama tena wamwambia ntakusemea kwa mwanao afu aende akashtaki we utakuwa tayari ushasafisha njia-
Kama wifi ataambiwa na mama mkwe kuwa ulitoka na binti kuwa mkali tena mshutumu kwa kukukosea heshima tena mchimbe mkwara kuwa akiendekeza mambo ya uwongo utamfungasha arudi kwao. USIKIRI kuwa umetembea na mdogo mtu lol kosa la jinai hilo ndugu yangu huwa halitoki ndani ya mioyo yetu, ni ndugu huyo na si shoga (ya shoga haiumi kama ya ndugu)
Lakini nawe shem umeshindwa kumpunga shetani wako (mbona revola zimejaa madukani jamani?) Ona sasa umejitia matatani......... pole
Ndugu yangu...
Utahalilisha haramu kwa namna hii? HAPANA! HARAMU NI HARAMU TU.
Hebu mfikirie yule mama yako aliyekuzaa halafu pata picha kuwa huyu naye ni mama..... bado utatafuta kuhalalisha?
khee DDD umefika hukuNdugu Burn huyo jamaa yako kesha tafuna vifaranga viwili dugu moja na kumfata shemejie Chuo ili aendelee kutafuna,nahisi muda huu tunalumbana hapa jamaa atakuwa amesha mla kuku mama wa vifaranga.