"....na mimi natafuta mtu wa kunipa raha"

"....na mimi natafuta mtu wa kunipa raha"

ngoshwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2009
Posts
4,131
Reaction score
937
Nilianza kumfahamu wakati huo nakwenda sana alipokuwa akifanyia kazi ambapo nilikuwa nikitaka huduma za "Internet" akaanza kuniita kaka....


Baada ya kupoteana kwa muda, wakati fulani nilikutana nae akanijulisha "kaka naolewa karibuni" nikamwambia jambo la busara, nikampa mchango wa send- off.

Hatukuwahi kuonana tena kwa muda wa zaidi ya miezi kadhaa..

Hivi majuzi akanitumia, "heri ya mwaka mpya, ..yaaani sijui kwa nini nimekukumbuka"

Nikamjibu "nawe pia...Mambo ya Mungu, Mungu kakukumbusha, salamu Mzee bhana"

Akanirejeshea: "yaani ninyi wanaume balaa..sina raha kabisa na Ndoa yangu"
Nikauliza "kwa nini??"

Akanitumia: "Huyu mwanaume mwenzio kaanza vurugu..anarejea nyumbani usiku wa manane...na mimi sana nataka nimwaonyeshe kuwa mwanamke naweza ku- revenge, na mimi natafuta mtu wa kunipa raha ":

Nilitafakari sana nikaona, moyo unanisukuma niache kutuma ujumbe, yawezekana upande wa pili nawasiliana na mwanaume mwenzangu akinitega...baadae nikaamua kutwanga na akapokea huyo dada akanieleza meengi lakini kwa umakini mkbuwa nilimsihi aendelee kuwa mvumilivu kwani ndoa ni ndoano, kutoka nje ya ndoa kwa mwanamke sio suluhu ya mamatizo ya ndoa. Ilinichukua kama dakika ishirini hivi kueleweka akasema nitaangalia kaka.

Baada ya kumaliza maongezi hayo, akanitumia ujumbe mfupi: "Nashukuru sana kaka umenipa ushauri mzuri sasa najisikia amani ..nipo nakunywa wine..." nikamjibu: "Ndio suluhu...asante".

..akajibu: 'vipi wewe?...nikualike lini kwangu..."

Mh:....nikajibu "nitakujulisha''


Leo nimepokea ujumbe,ananiambaia " ..yaani kaka mambo yamekuwa makubwa sana . jamaa amenipiga sana usiku..sasa nifanyeje??"

Nilishindwa kujibu huo ujumbe...moyoni bado natafakari ni nini hii....??
 
Huyo yupo directly anatafuta mwanaume wa kujivinjari naye kwa muda ili asahau shida zake kwa muda. na katika kuchanganua hapa na pale ameona akushike wewe, na nakueleza ukiendelea kujimeseji meseji ooh sijui hivi na vile lazima akunase na hapo ndo utajikuta kwenye dimbwi la ulimwengu mwingine...wajanja wengi, hapo kakueleza tu kupigwa sijui anarudi usiku wa manane , bado za chumvi , sukari, mafuta etc
 
Mwambie awajulishe ndugu wa mumewe pamoja na ndugu zake watamwambia cha kufanya kwa sasa. Awaite pia wasimamizi wake wa ndoa watamsaidia!
 
Kaa mbali nae vinginevyo na wewe utasema "Kwa herini wana JF wenzangu" kama TMK DAR.
 
hawana wazazi????

au watu wakubwa kwao wenye busara wakawashirikisha????

mana mkuu ukihusika hapo jumba bovu litakuangukia na utaonekana ka source ya yote.
 
Hapo wewe hujajua tu. Huyo dada anakutaka kimapenzi ila ameona atumie njia hiyo labda utamhurumia. Mie ninavyofahamu mambo ya ndoa huwezi kumwambia kila mtu ilikuwaje wewe hujaonana nae kwa muda mrefu mmetumiana msg za mwaka mpya halafu ghafla analeta mada za matatizo ya ndoa? hapo kaka unaombwa gemu kaa chonjo wewe mwanaume.
 
huyo mwanamke anakutaka. Dah! wanawake wa siku hizi si wavumilivu kabisa kwenye ndoa.
wana vimbelembele vya kuolewa, maranyingine hata hawajamfaham mwanaume vizuri, inasikitisha sana!

unapoingia kwenye ndoa inabidi huingie na miguu yote na umwambie mungu wako upo tayari kwa lolote na umuombe akusaidie na uhaidi kuwa muaminifu. Ivi hizi ahadi watu wanazitafakari kweli??? mara nyingine tunajilaani wenyewe kwa kusema uongo mbele za mungu.
whatever happens in marriage you should never ever think of cheating because it is never a solution.
 
kijana changamkia tenda bana....nothing beats the feeling u get wen u sleep with anada mans woman....ila usijedakwa tuu
 
......hata picha huelewi?kaa mbali,hana wazazi?
 
Mnh!..! Sasa nimeshafahamu kwa ninh ukimwi unashambulia sana walio kwenye ndoa!
 
Nilianza kumfahamu wakati huo nakwenda sana alipokuwa akifanyia kazi ambapo nilikuwa nikitaka huduma za "Internet" akaanza kuniita kaka....


Baada ya kupoteana kwa muda, wakati fulani nilikutana nae akanijulisha "kaka naolewa karibuni" nikamwambia jambo la busara, nikampa mchango wa send- off.

Hatukuwahi kuonana tena kwa muda wa zaidi ya miezi kadhaa..

Hivi majuzi akanitumia, "heri ya mwaka mpya, ..yaaani sijui kwa nini nimekukumbuka"

Nikamjibu "nawe pia...Mambo ya Mungu, Mungu kakukumbusha, salamu Mzee bhana"

Akanirejeshea: "yaani ninyi wanaume balaa..sina raha kabisa na Ndoa yangu"
Nikauliza "kwa nini??"

Akanitumia: "Huyu mwanaume mwenzio kaanza vurugu..anarejea nyumbani usiku wa manane...na mimi sana nataka nimwaonyeshe kuwa mwanamke naweza ku- revenge, na mimi natafuta mtu wa kunipa raha ":

Nilitafakari sana nikaona, moyo unanisukuma niache kutuma ujumbe, yawezekana upande wa pili nawasiliana na mwanaume mwenzangu akinitega...baadae nikaamua kutwanga na akapokea huyo dada akanieleza meengi lakini kwa umakini mkbuwa nilimsihi aendelee kuwa mvumilivu kwani ndoa ni ndoano, kutoka nje ya ndoa kwa mwanamke sio suluhu ya mamatizo ya ndoa. Ilinichukua kama dakika ishirini hivi kueleweka akasema nitaangalia kaka.

Baada ya kumaliza maongezi hayo, akanitumia ujumbe mfupi: "Nashukuru sana kaka umenipa ushauri mzuri sasa najisikia amani ..nipo nakunywa wine..." nikamjibu: "Ndio suluhu...asante".

..akajibu: 'vipi wewe?...nikualike lini kwangu..."

Mh:....nikajibu "nitakujulisha''


Leo nimepokea ujumbe,ananiambaia " ..yaani kaka mambo yamekuwa makubwa sana . jamaa amenipiga sana usiku..sasa nifanyeje??"

Nilishindwa kujibu huo ujumbe...moyoni bado natafakari ni nini hii....??

...usijali kaka...amekukumbuka ila nawe jitahidi usimkumbushe mengineyo.
Achana nae haraka iwezekanavyo!...
 
Ucje ukathubutu kufanya hilo lililokusukuma mpaka kuja kuomba ushauri huku..
 
Kaa pembeni mapema, kumbuka ni mke wa mtu huyo.Utakuja kuweka mikono kichwani
 
Back
Top Bottom