Na nyie mnaamini wazazi ni chanzo kikuu cha panya road?

Na nyie mnaamini wazazi ni chanzo kikuu cha panya road?

Joined
Jul 22, 2019
Posts
10
Reaction score
27
Ni moja ya sababu lakini sababu kubwa ya kuwepo kwa panya road ni hali ngumu ya maisha, mfumuko wa bei, kukosa ajira na kunyimwa mazingira ya kujiajiri hasa 'umachinga'.

Wanaokamatwa sasa hivi siyo watoto ni vijana wakubwa na wengine ni wababa kabisa, bado tu kuna sababu ya kuwatupia lawama wazazi kuwa hawapo makini na watoto wao? Yaani hao wababa wenye maisha yao?

Wengine wanatoka jela wakirudi mtaani hawaoni cha kufanya, maamuzi mabaya wanayofanya ni kujipatia mali kwa uharaka kupitia njia isiyo halali.

Wazazi walinde watoto wao lakini mazingira mengine yawekwe sawa ili mtu asiamue kuiba. Hakuna mtu ataiba kama kuna mazingira rafiki ya kujipatia pesa.

Sijui kama unawaza kama mimi.

Photo Credits: Musa Online
19d7db1931ac396add56e25c81e6a0bd.png
 
Ni moja ya sababu lakini sababu kubwa ya kuwepo kwa panya road ni hali ngumu ya maisha, mfumuko wa bei, kukosa ajira na kunyimwa mazingira ya kujiajiri hasa 'umachinga'.

Wanaokamatwa sasa hivi siyo watoto ni vijana wakubwa na wengine ni wababa kabisa, bado tu kuna sababu ya kuwatupia lawama wazazi kuwa hawapo makini na watoto wao? Yaani hao wababa wenye maisha yao?

Wengine wanatoka jela wakirudi mtaani hawaoni cha kufanya, maamuzi mabaya wanayofanya ni kujipatia mali kwa uharaka kupitia njia isiyo halali.

Wazazi walinde watoto wao lakini mazingira mengine yawekwe sawa ili mtu asiamue kuiba. Hakuna mtu ataiba kama kuna mazingira rafiki ya kujipatia pesa.

Sijui kama unawaza kama mimi.

Photo Credits: Musa OnlineView attachment 2361943
Huna hoja
 
Panya road ni matokeo ya kukosa ajira. Ndiye lile bomu la ajira walilokuwa wanalisema. Kilimo hakilipi, bodaboda imeshajaa, umachinga umeshikwa na watu wazima na nao umejaa. Hali ni mbaya sana. serikali isipochukua hatua kutatua tatizo la ajira nchi haina muda mrefu itawaka.
 
Panya road ni matokeo ya kukosa ajira. Ndiye lile bomu la ajira walilokuwa wanalisema. Kilimo hakilipi, bodaboda imeshajaa, umachinga umeshikwa na watu wazima na nao umejaa. Hali ni mbaya sana. serikali isipochukua hatua kutatua tatizo la ajira nchi haina muda mrefu itawaka.
Tatizo la ajira ni sehemu zote. Nenda kwa majirani ujionee balaa... ajira hakuna. Vilevile panya road hawana sifa za kuajiriwa kwa sababu shule hawana. Kifo ndo halali yao.
 
JPM angeweza set mfano bora wa kazi za makundi vijana kuzalisha na kupata maarifa katika makambi. Badala yake akapalilia mtawanyo bidhaa kwa kuendeleza machinga.
Tufanye maamuzi magumu, makundi vijana ilikibi kwa lazima wakapate ujuzi na kuwezeshwa.
 
Njaa huweza kumfanya mtu afanye lolote lile hata kama atahatarisha maisha ya wengine
Ipo haja ya serikali kuangalia hili la ugumu wa maisha
Leo hii 5000 mtu anapata kilo 1.5 mchele
 
Back
Top Bottom