Naangalia mechi ya Maji maji vs Young Africans kinachoonekana sio ishara nzuri kwa wana Yanga

Naangalia mechi ya Maji maji vs Young Africans kinachoonekana sio ishara nzuri kwa wana Yanga

Uwezo Lwandamina kama kocha wa mbeya city aliyetupiwa virago, sioni jipya kwao
 
Najiona kwa mbaaali.....Ila yanga mmebebwa leo
 
Mie yanga damu ila tubishe tulete ushabiki yanga hatuna team ya ushindani kwa sasa tuombe Mungu wenzetu msimbazi wabaki hivyo hivyo na usajili wao wa pesa nyingi na kocha huyo huyo labda nasema labda itakuwa ahuweni kwetu Jangwani
 
Mie yanga damu ila tubishe tulete ushabiki yanga hatuna team ya ushindani kwa sasa tuombe Mungu wenzetu msimbazi wabaki hivyo hivyo na usajili wao wa pesa nyingi na kocha huyo huyo labda nasema labda itakuwa ahuweni kwetu Jangwani
Cdhani kama ni sahihi kumlaumu kocha yeyote kwa mpira utaochezwa kwenye viwanja vya Njombe Mji na Majimaji. Timu nzuri hutegemea kiwanja tambarare (plane), chenye nyasi zilizotandawaa na kilicho laini (soft) ili timu inayotandaza soka ardhini ifanye hivyo bila kuathiriwa na uwanja, inayocheza kwa mashambulizi ya kujibiza (counter-attack) imudu kufanya hivyo kwa kasi iitakayo bila ya kuziwiliwa na mabondemabonde ya uwanja, inayocheza mpira wa kutumia nguvu isiangushwe na ugumu ama mabondemabonde ya kiwanja na inayocheza mipira mirefu ama ya juu isiathirike kwa wachezaji wake kuhofia kuumia wanapofika chini baada ya kuwania mipira ya juu. Viwanja vya Majimaji na Njombe vina kasoro zote hizo. Kumbuka hata Cannavaro alitangulia kuelezea ugumu wa mechi ya Majimaji kutokana na hali ya kiwanja hata kabla ya siku ya mechi. Kumbuka Kamusoko ameumia nyonga kutokana na ugumu wa kiwanja cha Njombe. Kumbuka hata ikiwa na Pluijm Yanga iliambulia sare mara kadhaa kiwanjani hapo. Kumbuka hata ikiwa na Pluijm Yanga haikufanya vizuri kwenye kiwanja chengine chenye hali kama hiyo cha Ndanda. Angalau wenyeji wa viwanja hivyo wana ka-natija (advantage) kadogo ka kuwa wameshavizowea. Lakini kwa timu zilizo kwenye daraja moja, ushindi kwenye viwanja kama hivyo unategemea bahati zaidi kuliko uwezo. Na huenda ndio kichocheo kimojawapo cha rushwa kutumika ili timu ijihakikishie ushindi.
 
kocha habadilishwi na hata nyinyi mashabiki wa mpira nchii mpira hamuujui mmebakia na midomo yenu michafu na yakipumbavu
 
Back
Top Bottom