Naanza kuamini tetesi uwanja uliofanyiwa marekebisho umewakataa simba kiroho, ndumba kuu za simba zilifukuliwa na kuchomwa, tutaona mengi sana

Naanza kuamini tetesi uwanja uliofanyiwa marekebisho umewakataa simba kiroho, ndumba kuu za simba zilifukuliwa na kuchomwa, tutaona mengi sana

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Na hakuna asiejua kwamba hizi timu mbili zote simba na yanga zina kamati maalum za wataalam wa mambo ya kiroho ila simba huwa inafanya wazi.

Tetesi zilizopo ni kwamba katika marekebisho ya uwanja, Yanga walitumia mwanya huu kupenyeza wataalam kubaini na kuziondoa ndumba za Simba,

magreda yalitumika kuzifukua zilizofukiwa uwanjani ikiwemo ndumba mama ambayo ilikuwa ni roho ya ndumba zote za simba hapo uwanjani, power tiller nazo zilitindua sakafu kuzitoa zile za vyumbani, n.k.

Kamati ya ufundi ya Simba walistukia mchezo ila hawakuwa na la kufanya, wataalam wao hawakuruhusiwa kuingia hata kwa gia ya vibarua wa kusaidia kazi.

Kilichofanyika ni kuitoa ndumba mama ya Simba na kwa sasa imebaki nduma mama ya yanga pekee ambayo imeongezewa zege zito na kusakafiwa vilivyo, kwa sasa ni kwamba bila ndumba mama ya simba zile ndumba zingine za wachezaji wa simba kuzivaa viunoni, kuweka golini, mashabiki kuingia nazo, wachezaji kutumwa kuziweka kabla ya mechi, n.k. hazina tena connection ya ndumba mama ili zifanye kazi, zote zitadidimizwa na ndumba mama ya Yanga.

Kuitoa ndumba ya Yanga sio suala la siku 1, yaweza chukua hata wiki nzima na kibali inabidi kiwepo cha kuingiza greda kubwa chimba na kuanza kutindua zege nene, hapa ndipo penye shida.
 
wataalam walipenyezwa kubaini na kufukua ndumba nzito kwenye uwanja wa taifa, hizo ndumba zilikuwepo kwa muda mrefu sana na zilichimbiwa haswa, waweza kuziita mitambo mikuu..
Upload hapa picha za hizo ndumba ili kudhihilisha unachoeleza hapa.
 
Na hakuna asiejua kwamba hizi timu mbili zote zina vitengo vya wataalam wa mambo ya kiroho ila simba huwa inafanya wazi wazi bila uoga.

Tetesi zilizopo ni kwamba katika marekebisho ya uwanja kuna wataalam walipenyezwa kubaini na kufukua ndumba nzito kwenye uwanja wa taifa, hizo ndumba zilikuwepo kwa muda mrefu sana na zilichimbiwa na kusakafiwa haswa.

Simba bado inahaha kurudisha hio mitambo lakini sio rahisi, baada ya ndumba za simba kufukuliwa, kuna ndumba nzito zaidi zimefukiwa kuharibu ndumba za simba watazojaribu kuweka upya uwanjani.
Hakuna uchawi kwenye soka! Kushindwa na kushinda ni sehemu ya mchezo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utoto raha sana......

Hakuna sehemu ya uwanja iliyochimbwa mtadanganywa hadi lini watanganyika?

Ule uwanja upo hatua ya kwanza ya ukarabati. Na bado kuna awamu tatu za ukarabati.

Sehemu iliyokarabatiwa ni majukwaa tu.

Kama una vieo au picha greda ikipita kung'oa majani unaweza uka update kwa ushahidi zaidi.

Kama uchawi ungekuwa unafanya kazi nigeria angekuwa bingwa wa kombe la Dunia.
 
Hakuna uchawi kwenye soka! Kushindwa na kushinda ni sehemu ya mchezo

Sent using Jamii Forums mobile app
Uchawi upo kwenye NN tu??kama kwenye soka haupo basi hâta kwenye mambo mengine pia haupo.. Reasons zinazotumika kwenye mambo mengine Ili kutumia Uchawi ndio hizo hizo zinazotumika kwenye Soka
 
Na hakuna asiejua kwamba hizi timu mbili zote zina vitengo vya wataalam wa mambo ya kiroho ila simba huwa inafanya wazi wazi bila uoga.

Tetesi zilizopo ni kwamba katika marekebisho ya uwanja kuna wataalam walipenyezwa kubaini na kuzifukua ndumba za simba, kuna ndumba zenye nguvu kubwa zilifukiwa na kusakafiwa vilivyo.

Baada ya kuzitoa ndumba hadi sasa pamewekwa ulinzi mkali sana dhidi ya wataojaribu kuweka ndumba zingine, huo ulinzi nao ni ndumba kubwa imefukiwa na kusakafiwa vilivyo.

Ni mpaka marekebisho yajayo ama Simba wahonge sana hapo uwanjani waruhusiwe kuleta greda litindue sakafu ya kutoa ulinzi unaowazuia kufanya yao.


Acheni kusajili na kuamini ujinga
 
Uchawi upo kwenye NN tu??kama kwenye soka haupo basi hâta kwenye mambo mengine pia haupo.. Reasons zinazotumika kwenye mambo mengine Ili kutumia Uchawi ndio hizo hizo zinazotumika kwenye Soka
Kwa sisi watu tuliosoma Elimu ya Astrology tunakuthibitishia kwamba Uchawi hauna nguvu kwenye Soka kwasababu Kwanza uchawi ni Long term Process Na pia katka kikundi uchawi huwa haufanyi kazi kwa watu wote hata kam watu wote hamna Kinga yoyote ya kiroho,

Unaweza ukaroga wachezaji 11 ila uchawi ukawachagua wachezaji wawili tu ama mmoja ndo ndumba ikafany kazi kwake na athari zake ni huw zinaonekan kweny maisha ya kawaida not in Match,

kwasabb Timu huundwa na kikosi cha watu wengi hivyo Nyota za wachezaji wote zikiunganika pamoja na Mfumo wa sayari utakavyokuwepo ndo Inaamua nani awe mshindi wa mechi husika, na hii huwa hakuna mchawi awezaye kubadilisha kitu,

Kitu pekee ambcho wachawi hukifanya kweny Soka ni kusababisha tu Mchezaji fulani labda aumie au Atolewe kwa kadi Nyekundu ili ile nyota ya pamoja ya Timu ambyo inapelekea (POF) kumbeba Mshindi,

Ipungue nguvu kidogo na kufanya labda badala ya kufungwa Tano basi timu ifungwe Moja au mbili tu,

ila kiufupi km ambavyo Hakun mchawi awezaye kubadilisha Mzunguko wa mwezi au nyota bas ndivyo Hivyo hivyo hakuna Mchawi anayeweza kubadilisha Matokeo ya mchezo kinachofanyika huwa n kupunguza athari tu za mchezo.
 
Na hakuna asiejua kwamba hizi timu mbili zote zina vitengo vya wataalam wa mambo ya kiroho ila simba huwa inafanya wazi wazi bila uoga.

Tetesi zilizopo ni kwamba katika marekebisho ya uwanja kuna wataalam walipenyezwa kubaini na kuzifukua ndumba za simba, kuna ndumba zenye nguvu kubwa zilifukiwa na kusakafiwa vilivyo.

Baada ya kuzitoa ndumba hadi sasa pamewekwa ulinzi mkali sana dhidi ya wataojaribu kuweka ndumba zingine, huo ulinzi nao ni ndumba kubwa imefukiwa na kusakafiwa vilivyo.

Ni mpaka marekebisho yajayo ama Simba wahonge sana hapo uwanjani waruhusiwe kuleta greda litindue sakafu ya kutoa ulinzi unaowazuia kufanya yao.
Sasa mbona Al Ahly alipigwa mbili tu?
 
Utoto raha sana......

Hakuna sehemu ya uwanja iliyochimbwa mtadanganywa hadi lini watanganyika?

Ule uwanja upo hatua ya kwanza ya ukarabati. Na bado kuna awamu tatu za ukarabati.

Sehemu iliyokarabatiwa ni majukwaa tu.

Kama una vieo au picha greda ikipita kung'oa majani unaweza uka update kwa ushahidi zaidi.

Kama uchawi ungekuwa unafanya kazi nigeria angekuwa bingwa wa kombe la Dunia.
una uhakika nigeria ni wachawi kuliko hao waliochukuwa kombe la dunia
 
Back
Top Bottom