Naanzaje kupata talaka?

muima

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2014
Posts
276
Reaction score
66
Nimeolewa miaka minne iliyopita na Nina watoto wawili,miaka miwili iliyopita tulihitilafiana na mume wangu tukatengana baada ya pale alisusa kuhudumia watoto kwa kilakitu ninaishi na watoto wangu bila msaada wowote kutoka kwake...
Naomba wakuu mniongoze katika kupata talaka ili nianze upya nikijua Niko huru kuliko kuishi kwa mashaka hivi kwa kivuli cha Ndoa ambayo haiexist. Msaada wenu Tafadhali.
 
Kama mlienda kanisani nadhani ulisikia ALICHOKIUNGANISHA MUNGU BINADAMU HATA KITENGANISHA ila kama mlienda serikalini fanya hivi nenda mahakama ya wilaya kaandikishe unadai taraka nenda na barua ya mwenyekiti wa mtaa pamoja na cheti cha ndoa mumeo atapelekewa wito wa mahakama nadhani nimekujibu!! Isipokua kabla ya yote fikilia watoto wanahitaji malezi ya wazazi wote kama sio kubwa lilowatenganisha itisha kikao cha wanandugu msuruhishane waislam japo kwao taraka ruksa ila wanasemaga ALLAH hapendi
 

Wacha maneno mengi wewe uwe mkweli,la hasha naona kuhitilafiana kwenu kuna husika na uzinzi, vinginevyo eleza vizuri. Hizo red hapo umejichanganya inaonekana mtoto wa pili si wa huyo bwana.
njoo na maelezo mazuri kwanza tuelewe huyo mtoto ulimpataje wakati mlishatengana miaka miwili kabla????
 

Ni Ndoa ya kanisani, mahakama haivunji Ndoa ya kanisa mkuu?lengo langu ni official divorce mkuu.
 
Pole dada, fuata maelekezo uliyopewa hapo juu. Kama ni mkristo nakushauri kabla ya talaka washirikishe viongozi wako wa dini pamoja wazazi na wasimamizi wenu wa ndoa ili wajatibu kuwasuluhisha kama chanzo cha ugomvi si kubwa. Ila kama mmeshashindwana kabisa nenda mahakamani na cheti cha ndoa ueleze nia yako. Umesema una watoto wawili inaonesha mtoto wa pili si wa huyo jamaa au ulimpata wakati mnagombana ukaondoka na mimba? Funguka kidogo upate ushauri mzuri.
 

Uzinzi haukuhusika na hitilafu ile mkuu watoto wote ni wake bila doubt...wakwanza tulimpata kabla ya kufunga Ndoa hiyo na wa pili no baada ya kufunga hiyo ndoa.... Uzizi ilikuwa ni muendelezo baada ya kutengana.
 
Sasa nimekuwa kwamba watoto wote ni wakwake. Kwahiyo hauna nia ya kurudiana naye au naye ameshapata mwingine nawe umepata mwingine?
 

anayekudanganya akili nae atakuacha tu na yeye
 

Asante mkuu, nina watoto wawili,kinachofanya nifocus kwenye talaka ni baada ya kuhitilafiana mwenzangu hakuona umuhimu wa kukaa kikao badala yake yeye na mama yake wakaungana kunishambilia Mimi kwa maneno,na kushauriana atafute m/mke mwingine na alifanya hivyo..kwa miaka hiyo miwili ameshaishi na wanawake watatu na kuachana nao...sioni kama kuna umuhimu wa kusuruhisha kwa sasa.
 
Sasa nimekuwa kwamba watoto wote ni wakwake. Kwahiyo hauna nia ya kurudiana naye au naye ameshapata mwingine nawe umepata mwingine?

Sijui huko aliko kama amepata mwingine ukiacha wale aliokuwa nao,me nimechoshwa na kivuli hiki nataka kuwa huru tena.
 
Cjadanganywa mkuu, we unaspoti kuendelea kuwa kwenye kivuli hiki?

kwa kuwa upo peke yako unaongea hapa ndio utaonekana upo sahihi kabisa akija wa upande wa pili akitoa hoja sijui itakuwaje ndio maana wanasema ndoa ni kifungo wewe endelea upate taraka uleee matoto yasiyokuwa na malezi ya baba
 
kwa kuwa upo peke yako unaongea hapa ndio utaonekana upo sahihi kabisa akija wa upande wa pili akitoa hoja sijui itakuwaje ndio maana wanasema ndoa ni kifungo wewe endelea upate taraka uleee matoto yasiyokuwa na malezi ya baba

Asante mkuu?
 
Uzinzi haukuhusika na hitilafu ile mkuu watoto wote ni wake bila doubt...wakwanza tulimpata kabla ya kufunga Ndoa hiyo na wa pili no baada ya kufunga hiyo ndoa.... Uzizi ilikuwa ni muendelezo baada ya kutengana.

Kizazi hiki!!!!Huwa napata shida sana kushauri watu wa aina yako (waliofunga ndoa kimyakimya halafu wakaenda kuhalalisha kanisani nafikiri unanielewa) Sasa kwa vile mlipata kibali kanisani hebu soma hapa: mathayo 19:6. Kwa andiko hili naamini hakuna kiongozi wa dini atakayekwambia achana na mumeo.
 

Ila nifanye nn mkuu?
 
Ila nifanye nn mkuu?

Kinachowasumbua ninyi ni utoto na ujana tu hakuna sababu yoyote hapo.Watumie wazazi wako na viongozi wa dini yenu wawashauri mkae mlee watoto wenu. Napata picha kwamba mlilazimisha kuoana ndo maana hamkufuata taratibu mkaamua kupeana mimba ili ndo kiwe kibali cha ninyi kuoana, na matokeo yake ndo haya.
 
Ndoa ya kanisani inaweza kuvunjwa na Pope peke yake Kama ni katoliki sijui lutheran!! Na pope anaweza kuvunja hio ndoa endapo kuhitilafiana kwenu kumetokana na uzinzi!! Huyo mumeo Kama anasikiliza mama yake atapoa tu Kama ameshaishi na wanawake watatu na wameenda ujue mke wake ni wewe atarudi tu!! Itisha kikao nenda kanisani watakusaidia
 
kwa kuwa upo peke yako unaongea hapa ndio utaonekana upo sahihi kabisa akija wa upande wa pili akitoa hoja sijui itakuwaje ndio maana wanasema ndoa ni kifungo wewe endelea upate taraka uleee matoto yasiyokuwa na malezi ya baba

Mpaka sasa hawamjui baba yao it makes no difference.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…