Naanzisha kampeni na programu ya kumlinda na kumhifadhi(protect) mwanamke mweusi anayeelekea kupotea duniani

Naanzisha kampeni na programu ya kumlinda na kumhifadhi(protect) mwanamke mweusi anayeelekea kupotea duniani

Kilimbatzz

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2023
Posts
9,134
Reaction score
14,593
Mwanadamu tangu kuumbwa kwake Kwa kudhamiria au bahati mbaya ameshaharibu viumbe wengi amabao Kwa sasa hawapo kabisa(extinct)

Mifano ipo mingi,nikihamua kuiandika hapa nitaijaza JamiiForums nzima

Karma ya kuangamiza viumbe wengine sasa imemugeukia binadamu mwenyewe

Mwanamke mweusi siku hizi kumuona ni nadra sana,Unaweza shinda siku nzima kati ya wanawake mia moja,mweusi ukamuona mmoja au wawili

Tunaenda wapi!!?

Hivi ni kweli huko wodini watoto kike wanaozaliwa wote ni wa maji ya kunde na weupe!?

Usasa wa kutumia losheni zinazomweupisha mwanamke zinatokomeza kiumbe hiki adimu Kwa sasa kama faru kule polini

Naomba maoni na ushauri,nifanyeje Ili niweze kufanikisha adhima yangu!!?

NB:
Popote utakapomuona mwanamke mweusi usiache kumpongeza na kumpa moyo
 
Mwanamke kama aliwafanyia vitimbi na hakuwasikiliza Mitume na Manabii wa mwenyezi mungu, Kina Adam na Lut (Loot). Na wakanyoosha mikono kushindwa kuwalinda na kuwaongoza hao wanawake.

We nani mpaka uweze?
 
Mwanamke kama aliwafanyia vitimbi na hakuwasikiliza Mitume na Manabii wa mwenyezi mungu, Kina Adam na Lut (Loot). Na wakanyoosha mikono kushindwa kuwalinda hao wanawake.

We nani mpaka uweze?
Mwanamke kafanyaje!?
 
Mwanamke kafanyaje!?
● Mwanamke aitwae Hawa (Eve) alimshawishi Adam kumukosea mungu kwa kula tunda alilokatazwa na mungu asile, wakati yupo mbinguni. Adam akamuasi mungu akala.

● Mwanamke aitwae Waliha (Ado/Edith), aliekua mke wa Nabii Lut (Lot) ndio aliokua mwenyekiti wa ushenzi wa watu wa Sodoma Na Gomora. Huyu mama alifikia hatua akawa ndio mchora ramani za mkuu wa kumtia mashakani Nabii Lut (Lot) kwenye kazi alizokua akipewa na mungu wake.

Siku Lut alitembelewa na Malaika wawili nyumbani kwake, walikwenda kwa umbile la kibinaadamu la kiume (Kama wanaume wawili). Lut aliwaingiza nyumbani kwake kuwaficha na kisha kufunga milango ya nyumba yake, aliwakaribisha chakula muda ulipofika wa kula, waligoma kula.

Kwa hekima alizopewa na mungu wake akajua moja kwa moja kwamba hawa viumbe sio binaadamu. Wakati anaongea nao sebuleni, mkewe Waliha (Ado/Edith) alikua kajificha akiwasikiliza na kuwatazama kwa umakini. Akatoka kimya kimya kupitia mlango wa nyuma ya nyumba na kwenda kumsagia Nabii Lut (Lot) kunguni kwa vidume huko mitaani, Malika (Ado/Edith) "Oya kuna mchongo, jamaa yenu anaejiita Nabii wa mungu ameleta mali safi huko, za ukweli kinoma. Kazi kwenu!"

Vidume wakajikusanya kikundi, basi kukukuru kakara mpaka nyumbani kwa Nabii Lut (Lot), wakamgongea mlango Nabii Lut na alipofungua mlango akawaona kikundi cha njemba kubao zipo nje ya nyumba yake zimekuja kuwachukua wageni wake ili waende wakawa lawiti na kuwafanyia ushenzi mwingine huko.

Nabii Lut presha ikapanda, akawaambia "Jamani hawa ni wageni wangu, chukueni mabinti zangu kama vipi hawa muwaaache, msiwaguse". Vidume wakakaza, "Babu sisi hatuwataki hao mabinti zako, kwani hatuwajui mabinti zako? Sisi tunawataka hao wageni wako wa kiume! Fanya ututolee hapa!".

Nabii Lut (Lot) presha ikazidi kupanda zaidi, basi mbio akafunga mlango na kuanza kusali "Eeh mungu wangu, huu mtihani sasa, hawa watu wangu wamekufanyia maasi muda mrefu, ila sasa wanavuka mipaka, wanataka mpaka wageni wangu. Naogopa sitoweza kuwalinda! Naomba msaada wako na ulinzi wako!"

Wageni wawili wale walimuona Nabii Lut (Lot) alivokua akihangaika huku na kule, na ndio wakamuita, kumkalisha chini na kumwambia "Mzee wetu, fungua huo mlango, wewe ondoa shaka. Sisi ni malaika tumetumwa na mungu wako kuja kufanya kazi yetu. Kazi yako sasa imekwisha! Wachukue watu wako na uondoke nao! Na wala msigeuke nyuma huko muendako!"

Nabii Lut (Lot) akaongea na watu wake, wakasepa zao. Na bado ukitaka kujua mwanamke ni kiumbe gani, licha ya vuta nikuvute na mkewe mpaka kukubali kuondoka, ila njiani wakati wanaondoka basi mke wake akashindwa kuvumilia kutaka kujua nini kinaendelea kwa wale jamaa wawili! Akageuka nyuma licha ya kukatazwa asigeuke!
 
Kwahiyo kisa hiki ndo tusiwaokoe!?
● Mwanamke aitwae Hawa (Eve) alimshawishi Adam kumukosea mungu kwa kula tunda alilokatazwa na mungu asile, wakati yupo mbinguni. Adam akamuasi mungu akala.

● Mwanamke aitwae Waliha (Ado/Edith), aliekua mke wa Nabii Lut (Lot) ndio aliokua mwenyekiti wa ushenzi wa watu wa Sodoma Na Gomora. Huyu mama alifikia hatua akawa ndio mchora ramani za mkuu wa kumtia mashakani Nabii Lut (Lot) kwenye kazi alizokua akipewa na mungu wake.

Siku Lut alitembelewa na Malaika wawili nyumbani kwake, walikwenda kwa umbile la kibinaadamu la kiume (Kama wanaume wawili). Lut aliwaingiza nyumbani kwake kuwaficha na kisha kufunga milango ya nyumba yake, aliwakaribisha chakula muda ulipofika wa kula, waligoma kula.

Kwa hekima alizopewa na mungu wake akajua moja kwa moja kwamba hawa viumbe sio binaadamu. Wakati anaongea nao sebuleni, mkewe Waliha (Ado/Edith) alikua kajificha akiwasikiliza na kuwatazama kwa umakini. Akatoka kimya kimya kupitia mlango wa nyuma ya nyumba na kwenda kumsagia Nabii Lut (Lot) kunguni kwa vidume huko mitaani, Malika (Ado/Edith) "Oya kuna mchongo, jamaa yenu anaejiita Nabii wa mungu ameleta mali safi huko, za ukweli kinoma. Kazi kwenu!"

Vidume wakajikusanya kikundi, basi kukukuru kakara mpaka nyumbani kwa Nabii Lut (Lot), wakamgongea mlango Nabii Lut na alipofungua mlango akawaona kikundi cha njemba kubao zipo nje ya nyumba yake zimekuja kuwachukua wageni wake ili waende wakawa lawiti na kuwafanyia ushenzi mwingine huko.

Nabii Lut presha ikapanda, akawaambia "Jamani hawa ni wageni wangu, chukueni mabinti zangu kama vipi hawa muwaaache, msiwaguse". Vidume wakakaza, "Babu sisi hatuwataki hao mabinti zako, kwani hatuwajui mabinti zako? Sisi tunawataka hao wageni wako wa kiume! Fanya ututolee hapa!".

Nabii Lut (Lot) presha ikazidi kupanda zaidi, basi mbio akafunga mlango na kuanza kusali "Eeh mungu wangu, huu mtihani sasa, hawa watu wangu wamekufanyia maasi muda mrefu, ila sasa wanavuka mipaka, wanataka mpaka wageni wangu. Naogopa sitoweza kuwalinda! Naomba msaada wako na ulinzi wako!"

Wageni wawili wale walimuona Nabii Lut (Lot) alivokua akihangaika huku na kule, na ndio wakamuita, kumkalisha chini na kumwambia "Mzee wetu, fungua huo mlango, wewe ondoa shaka. Sisi ni malaika tumetumwa na mungu wako kuja kufanya kazi yetu. Kazi yako sasa imekwisha! Wachukue watu wako na uondoke nao! Na wala msigeuke nyuma huko muendako!"

Nabii Lut (Lot) akaongea na watu wake, wakasepa zao. Na bado ukitaka kujua mwanamke ni kiumbe gani, licha ya vuta nikuvute na mkewe mpaka kukubali kuondoka, ila njiani wakati wanaondoka basi mke wake akashindwa kuvumilia kutaka kujua nini kinaendelea kwa wale jamaa wawili! Akageuka nyuma licha ya kukatazwa asigeuke!
 
mwanamke mweusi hawezi kupote kwa losheni.

DNA itasimamia ukweli kwa watakao wazaa na cycle itaendelea

labda wapake losheni na DNA zao ndio mwanamke mweusi anaweza kupotea
 
Back
Top Bottom